Tuesday, January 15, 2013

MAASKOFU WATAKIWA KURUHUSU WALIMU KUFUNDISHA NYIMBO ZA KUSIFU NA KUABUDU NDANI YA MAKANISA YAO

BAADHI YA WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI JIJINI ARUSHA WAKIIMBA  NA KUTUMBUIZA KATIKA MKUTANO WA INJILI




Na bety alex,Arusha

MAASKOFU WATAKIWA KURUHUSU WALIMU KUFUNDISHA NYIMBO ZA KUSIFU NA KUABUDU NDANI YA MAKANISA YAO

MAASKOFU wa makanisa mbalimbali ambao hawana uwezo wa kutunga nyimbo mbalimbali za kusifu na kuabudu wametakiwa kuhakikisha kuwa kamwe hawaachi makanisa yao yakiendelea kupoteza uwepo huo bali wanatakiwa kuwatumia zaidi walimu ambao wana uwezo wa kufundisha nyimbo za kusifu na kuabudu.

Kauli hiyo imetolewa na askofu Aminiel Mgonja wa kanisa la Arusha Praise Centre la jijini hapa wakati akiongea na “MALKIA WA MATUKIO”mara baada ya kutambulisha rasmi Album yake ijulikanayo kama Ueponi mwako

Askofu Mgonja alisema kuwa kipajin cha kutunga kuimba nyimbo za kusifu na kuabudu si watumishi wote ambao wana uwezo wa kufanya hivyo lakini kutokana na kushindwa kufanya hivyo si sababu pekee ambayo itaweza kuyafanya makanisa kushindwa kusifu na kuabudu

Alisema kuwa kama watumishi wa Mungu wataweza kuwapa fursa baadhi ya walimu kuweza kufundisha na kutunga nyimbo mpya za kusifu na kuabudu hali ambayo itawafanya Uwepo wa Mungu kuweza kusogea tena kwa haraka sana tofauti na sasa ambapo baadhi ya makanisa yanashindwa kufungulia huduma hiyo.


Pia alisema kuwa hata kwa wale ambao wana uwezo wa kutunga nyimbo za kusifu na kuabudu bado wana uwezo mkubwa sana wa kuendelea kuwa wabunifu tena wa hali ya juu sana  kwa kuhakikisha kuwa nyimbo ambazo wanazitunga zinakuwa ni njia mojawapo ya kuwasogeza watu uweponi mwa Bwana.

Katika hatua nyingine Mgeni Rasmi katika uzinduzi wa Album hiyo ya Uweponi mwako,Askofu Olam Mustapha kutoka katika kanisa la Gloryland,alisema kuwa mtumishi wa mungu anapofanya Jambo zuri hata watumishi wengine nao wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanafuraia jambo hilo na Kumuunga mkono na kuachana na tabia ya kuchukiana ovyo

Olamu alisema kuwa wapo baadhi ya watumishi wa Mungu pamoja na Wakristo ambao kila mara wanachukiana kwa ajili ya mafanikio ya Mtu lakini hali hiyo ni mbaya sana na ndio inayomtukuza shetani badala ya Mungu.


Pia katika uzinduzi huo wa Album hiyo zaidi ya Milioni tisa zilikusanywa kutoka kwa watu mbalimbali huku  lengo halisi likiwa ni kumuunga mkono Askofu huyo.

MWISHO

No comments:

Post a Comment