Friday, November 3, 2017

WAFANYAKAZI WA EXIM WAHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA 27 JELA KWA KOSA LA UTAKATISHAJI NA UHARIBIFU WA NYARAKA


WAFANYAKAZI wa Benki Ya exim waliokuwa wanakabiliwa na makosa 318 ikiwa ni pamoja na kugushi,kuharibu nyaraka,na utakatishaji fedha haramu na wizi wa dola za kimarekani 521,000 wamehukumiwa kifungo cha miaka 27 jela huku wafanyakazi wengine saba wakiachiliwa huru kutokana na mahakama kushindwa kudhibitisha makosa yao


Aidha wafanyakazi hao wamehukumiwa mapema leo kwenye MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Arusha/Arumeru ambapo wamekutwa na hatia mbalimbali kinyume cha sheria.


Akisoma hukumu hiyo kwa zaidi ya masaa 5 kuanzia saa 4.30 asubuhi hadi saa 9.07 Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo Deusdedit Kamugisha aliwataja aliowatia hatiani ni pamoja na mshitakiwa namba mbili Liliani Mgeye{33},Daudi Nhosha{39},Doroth Cjijanja{50},Genes Massawe{32},Christopher Lyimo{34} na DeusdediT Chacha{35}.


Alisema watuhumiwa wengine waliokutwa na makosa ya kugushi nyaraka na kuharibu nyaraka ambao ni pamoja na Nhosha Massawe na lyimo wamehukumiwa kwenda jela miaka minne kila mmoja kwa kosa hilo.

Hakimu Kamugisha aliwataja walioachiwa huru na mahakama baada ya upande wa jamhuri kushindwa kuthibitisha katika ushahidi wao kuwa watuhumiwa hao walitenda makosa hayo ni pamoja na mshitakiwa wa kwanza katika kesi hiyo ambaye alikuwa meneja Mkuu wa  Exim Benki{T} ltd tawi la Arusha Bimel Gondaili.

Wengine ni pamoja na Livingstone Mwakihaba{37} maarufu kwa jina la ‘’stone’’,Joyce Kimaro{36},Evance Kashebo{40},Tutufye Agrey{32},Joseph Neki{30} na mfanyabiashara Gervas Lubuva{54}.

MWISHO WSA

No comments:

Post a Comment