Tuesday, April 29, 2014

ASKOFU ISANGYA ANENA NA VIJANA

IMEELEZWA kuwa ongezeko la vijana maeneo ya mijini chanzo chake kikubwa ni kuwa asilimia kubwa ya vijana hasa wa vijijini bado hawajaweza kutambua fursa za uchuni  walizonazo hali ambayo nayo inasababisha wimbi kubwa la watu mijini ambao hawana ajira za kutosha


Vijana wanaokimbilia mijini kutoka vijijini ni kutokana na kuwa kule vijijini hawahapata muongozo wa kutambua na kisha kutumia fursa za mali zilizopo jambo ambalo kwa sasa wadau ikiwemo serikali inatakiwa kuchukua tahadhari juu ya hilo.

Kauli hiyo imetolewa na askofu Dkt Eliud Isangya wa kanisa la Intenational evangelism Church  wakati akiongea na waandshi wa habari kuhusiana na fursa za vijana pamoja na changamoto ambazo zinawakabili vijana.

Aidha alidai kuwa inashangaza sana kuona kuwa wimbi kubwa la vijana wanakimbilia mijini wakati huko vijijini kuna fursa za kutosha na hazitumimiki wakati mijini fursa za ajira hazipatikani

Kutokana na hilo alisema kuwa kinachosabbisha waje mijini ni kuwa hawajaweza kutambua fursa zilizopo huku baadhi ya watumishi wa serikali wenye dhamana na vijana nao wakiwa wamesahu wajibu wao kwenye jamii wa kusaidia kundi hilo.

“hawa watendaji wa serikali wakati mwingine wanasahu wajibu wao hata wa kuweza kutangaza fursa za ajira kwa vijana na inasababisha vijana waweze kuona kuwa wapo pekee yao na hivyo wanaona bora waje mjini”aliongeza Dkt Isangya.

Hataivyo alidai kuwa kutokana na hilo asilimia kubwa ya vijana wanaokuja mijini wanasababisha madhara makubwa sana kwani wengi wao wajikuta wakiwa wanaangukia katika matukio ya kihalifu na matukio mabaya ya uharibifu wa amani ya nchi kwa hali hiyo ni changamoto kubwa sana kwa serikali, kwa vijana na hata wadau wa dini’aliongeza Dkt Isangya.
MWISH

No comments:

Post a Comment