Monday, May 21, 2012

VIONGOZI WA MAKAMPUNI YA ULINZI WATAKIWA KUWA NA TAARIFAA ZA MAFUNZO YA KAZI ZAO

VIONGOZI wa makampuni ya ulinzi  mkoani arusha yametakiwa kutoa taarifa za mafunzo yanayoendana na kazi zao kwa jeshi la polisi ili kuwawezesha wafanyakazi  wao  kupatiwa mafunzo ya  kuongeza ujuzi wa kufanya kazi  wawapo katika malindo yao.

Hayo yalisemwa na mkuu wa kitengo cha polisi jamii mkoani hapa bi Mary Lugola  alipokuwa akifungua kongamano la chama  cha wafanyakazi  walinzi(TUPSE) na wadau wa ulinzi binafsi  lililofanyiika mjini hapa.

Bi Mary alisema kuwa kwa sasa jeshi la polisi liko tayari kutoa mafunzo yanayoendana na kazi zao  kwa makampuni mbali mbali hivyo  viongozi wa makampuni hayo yahakikishe kuwa yamezingatia vigezo  ili kuwawezesha wafanyakazi hao kunufaika na mafunzo hayo.

  Aidha aliwataka askari kuwa na nidhamu na kuhakikisha kuwa huduma wanazozitoa kwa wananchi ni nzuri sio za kejeli kwa kuwa wapo baadhi ya askari ambao sio waaminifu wawapo katika kazi zao.

Kwa upande wake katibu wa chama cha wafanyakazi walinzi  kit aifa bw Godiwin Mariki alisema kuwa  katika chama chao kumekuwepo na changamoto lukuki ikiwemo   ya wateja kulazimisha rushwa ya fedha kutoka kwa waajiri walipotoa tenda ya ulinzi  na pale waajiri wanapokuwa hawatoi rushwa hizo basi wateja hao huvunja lindo na kuwapatia waajiri wengine.

Alisema kuwa kupitia jambo hili wanaiomba serikali ikemee vitendo hivyo na kuagiza malindo yatolewe kwa mkataba isiyopungua mika mitatu ili kuwezesha waajiri kuwa na uwezo wa kuwahudumia walinzi wake.

Pia alitaja changamoto ingine kuwa ni pamoja  na wanawake kuachishwa kazi pale wanapopata ujauzito na kutolipwa mishahara wakati wakiwa likizo ya uzazi kwa madai kuwa ni starehe yao na haimhusu mwajiri, hivyo kuitaka serikali kukemea na kuchukua hatua kwa kuwa huo ni uonevu.

Aidha TUPSE imependekeza kuwa sera na sheria ya ulinzi binafsi iharakishwe ili kuondokana na maonezi mengi yanayofanyiwa walinzi ,waajiri,wateja na jamii inayowazunguka .
Mwisho..


chanzo cha habari na Queen Lema,

ARUSHA

No comments:

Post a Comment