Saturday, May 12, 2012

WAPO WATU AMBAO HAWATAONA UFALME WA MUNGU KISA SIMU


Wakristo wametakiwa kuwa makini sana na matumizi ya simu za mikononi kwa kuwa asilimia kubwa ya wakristo wanadanganya watu bila kujua na kutambua kuwa wana muasi mungu wao

Asilimia kubwa ya watu wanadanganya na kisha wanakuja makanisani wakijua kuwa wapo sawa lakini hakuna dhambi ndogo hata kidogo

Hayo yameelezwa na mchungaji Joseph moto wa kanisa la antiokia reviaval church liliopo sombetini jijini hapa wakati akiongea na waumini wa kanisa hilo hivi karibuni

Mchungaji Moto alisema kuwa kila mahala wakristo wanajiwekea utaratibu wa kuongea uongo wakati wa kiwa wanaongea na simu na badala yake wanashindwa kujua kuwa kwa mungu hakuna dhambi ambayo ni ndogo

Alieleza watu hao wanaongea uongo kwa njia ya simu mara nyingi sana huwa wanadhamiria huku wakiwa makanisani mwao wanaonesha kuwa wanapinga dhambi ya uongo

‘napenda kuwasihi wakristo kuhakikisha kuwa duniani hakuna dhambi ndogo na badala yake wajue kuwe mungu hapendi na wakicheza wapo baadhi ambao hawataweza kuona ufalme wa mungu ktokana na simu”alisema mchungaji huyo

Katika hatua nyingine aliwatahadharisha wakristo kuhakikisha kuwa wanajua matumizi ya simu kwa kuhakikisha kuwa wanakuwa na ukweli hasa kwa wenza wao

Aliongeza kuwa hakuna jambo jema kwenye simu kama kuongea kwa mwenza wako au ndugu yako wa karibu ukweli kwa kuwa hali hiyo itachangia kwa kiwango kikubwa sana hata kujenga jamii

‘leo  unakuta watoto wetu wan waangalia masuala mbalimbali na wananakili sana wazazi wao wanchokifanya sasa kwa hali hii kama wazazi wataangalia zaidi kuongea uongo wanawafundisha nini watoto wao"aliongeza mchungaji huyo
 MWISHO

CHANZO CHA HABARI NA QUEEN LEMA

ARUSHA 

0758907891

No comments:

Post a Comment