Sunday, September 22, 2013

HASARA NYINGI ZA WAKRISTO ZINATOKANA NA UBAGUZI WA HUDUMA ZA KANISA

HASARA NYINGI ZA WAKRISTO ZINATOKANA NA UBAGUZI WA HUDUMA ZA KANISA

Na Mwandishi wetu. Arusha


Wakristo wanakabiliwa na changamoto ya ubaguzi wa ibada hali ambayo wakati mwingine ndiyo chanzo cha wao kwenda makanisani kwa mazoea bila kufanikiwa katika maisha yao huku wengine wakiwa wnaaambulia hasara za mali na hali zao kila siku

Asilimia kubwa ya wakristo wana ubaguzi wa huduma za ibada kama vile Maombi,utoaji wa mafungu ya kumi,harambee za kila siku na michango ya hiari hali ambayo ni kikwazo kikubwa cha maendeleo ya kanisa.

Hayo yameelezwa na Mchungaji Steven Laizer  wa kanisa la Bethel  Kishore  lilopo maeneo ya Kishore Ngaramtoni jijini Arusha mapema wiki iliyopita.

Mchungaji Steven alidai kuwa tabia hyo imekuwa na kustawi sana kwenye baadhi ya maksanisa huku baadhi ya wakristo wakiona kuwa makanisa hayo pamoja na wachungaji hawawombei kwa kutosha bila kujua na kutambua kinachowafanya wasiweze kusonga mbele ni uchoyo na ukaataaji wa huduma mbalimbali ndani ya makanisa.

Alisema kuwa wengi wanajidanganya kuwa huduma ambazo zinaweza kuwakomboa kwenye maisaha yao ni huduma za kusifu na kuabudu pekee jambo ambalo sio la kweli kwani huduma zote Mungu yupo pamoja na wanadamu

“ndani ya kanisa ukiita huduma ya kusifu na kuabudu watuw ataalikana lakini ita huduma ya maombi hata ya kufunga na kuomba uone kama utaona watu wengi watu wanashindwa kujua na kutamvbua kuwa ubaguzi wa huduma ndani ya makanisa haufai kabisa na badala yake unaddiimiza maslahi ya kanisa’aliongeza Mchungaji huyo

Wakati huo huo aliseama kuwa ndani ya makanisa wapo baadhi ya watu ambao wanaona shida kutoa sadaka kwa madai kuwa hakuna anayewaona na kisha kuingia mitini jambo ambalo ndilo chanzo cha hasara kwenye maisah yao

“chunguza sana mtu anayeshidwa kutoa sadaka kwa mungu maisaha yaklle yakoje utakuta kila siku analia mara ugonjwa, mara hasara, mara wizi sasa kama utakuwa unatoa sadaka ni wazi kuwa utakuwa unajilinda dhidi ya vitu kama hivi ambavyo vinacheza kwenye malango ya shetani’aliongeza mchungaji huyo.

Alimalizia kwa kuwataka hata Viongozi wa dini nao wahakikishe kuwa kamwe hawaoni aibu kuhubiri juu ya vitu mbalimbali ambavyo vinaweza kuwatenganisha wakristo na huduma za Mungu kwa kuhofia jambo Fulani kwenye maisha ya kibinadamu ya kila siku.

MWISHO

No comments:

Post a Comment