Tuesday, March 26, 2013

UGONJWA WA MAHINDI KUTOKA KENYA WAWAATHIRI WANANCHI KATA YA KIKWE MERU


UGONJWA WA MAHINDI KUTOKA KENYA WAWAATHIRI WANANCHI KATA YA KIKWE MERU

ZAIDI ya Hekari 300 kutoka katika kata ya Kikwe Wilayani Meru mkoania Arusha zimeharibiwa vibaya na ugonjwa mahindi kutoka Nchini Kenya unaojulikana kama ugonjwa wa kusinyaa kwa mahindi hali ambayo itafanya wakulima washindwe kupata mahindi wakati wa mavuno

Akiongea na “patapata”mapema jana diwani wa kata hiyo bw Emanuel Silayo alisema kuwa hali hiyo ya ugonjwa ambayo imekumba kata hiyo ya Kikwe inaashiria njaa kubwa sana kwa kuwa mazao ya mahindi shambani hakuna huku wakulima wakiwa wameshapanda

Silayo alisema kuwa Miezi michache iliyopita wakulima waliweza kupanda mazao ya nafaka hasa mahindi lakini baada ya mahindi kuchomoza yalianza kushambuliwa na ugonjwa hadi kufa

Alisema kuwa pamoja na kuwa mahindi hayo yamekufa wakati wakulimna wengi wamepanda kwa ajili ya mategemeo ya chakula katika eneo hilo la Kikwe lakini mahindi machache sana yameweza kusalia hali ambayo bado ni kiashirio kikubwa sana cha Njaa


Alifafanua kuwa kama tahadhari haitaweza kuchukuliwa kwa haraka sana basi huenda wakati wa mavuno ndani ya mwaka huu kusiwe na mavuno kabisa hivyo baa la njaa kuweza kutawala katika Wilaya hiyo ya Meru.

Akiongelea Ugonjwa huo wa mahindi kutoka nchini Kenya Afisa Kilimo Wilaya ya Meru,Grace Solomoni alisema kuwa ugonjwa huo ni hatari sana kwa kuwa unashambulia zao la mahindi hadi kufa lakini bado mkulima anaweza kupata angalau kiasi kidogo

Grace alisema kuwa kwa mujibu wa taararibui za kilimo mara baada ya shamba kuathiriwa na ugonjwa huo shamba linapswa kupumzishwa kwa kipindi cha miaka mitatu ili vijidudu vife lakini kama wakulima wataendelea kulima basi watasababisha  vijidudu hivyo kuzaliana kwa wingi sana

No comments:

Post a Comment