Saturday, March 9, 2013

WAMILIKI WA SHULE BINAFSI WATAKIWA KUWAANGALIA YATIMA NA WALE WANAOTOKEA KATIKA MAZINGIRA MAGUMU


Na Queen Lema,Arusha

WAMILIKI WA SHULE BINAFSI WATAKIWA KUWAANGALIA YATIMA NA WALE WANAOTOKEA KATIKA MAZINGIRA MAGUMU

IMEELEZWA kuwa endapo kama Wamkiliki wa shule binafsi  wataweza kusaidia jamii za watoto yatima na wanaotokea katika mazingira magumu katika shule zao basi watachangia kwa kiwango kikubwa sana kupunguza tatizo la watoto wa mitaani.

Asilimia kubwa ya watoto wanaokimbilia mitaani wanakwena huko kwa kuwa baadhi ya familia zao hazina uwezo wa kuwasaidia katika masuala ya elimu hali ambayo nayo kwa wakati mwingine inasababisha wimbi la watoto hao.

Kauli hiyo imetolewa na  Bi  Isabela Daniel ambaye ni  Mkurugenzi wa Shule ya Upendo Friends iliopo Matevesi Jijini hapa mapema jana wakati akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea shule hiyo kwa malengo ya kutambua nafasi ya Watoto Yatima ndani ya shule Binafsi.

Isabela alisema kuwa kwa sasa kutokana na hali ya Maisha sio wanafunzi wote ambao wana uwezo wa kwenda shule hasa za binafsi na hata zile za Serikali hivyo basi kama wamiliki wa shule watakuwa wanaaacha kuliangalia suala hilo kwa undani ongezeko la watoto wa mitaani litakuwa ni kubwa sana.

Alifafanua kuwa wamiliki wanatakiwa kujiwekea utaratibu wa kuhakikisha kuwa kila mara wanaweka utaratibu wa kuwachukua japo kidogo na  kuwapa elimu wanafunzi ambao wanatokea katika makundi maalumu japo kwa uchache ambapo pia hali hiyo itachangia sana nafasi ya maendeleo katika taifa la Tanzania.


Awali Mkurugenzi huyo alisema kuwa nayo Serikali kwa kushirikiana na Shule Binafsi zinatakiwa kuhakikisha kuwa zinaweka utaratibu wa kutambua vipaji vya baadhi ya watoto kwani kwa sasa wapo baadhi ya watoto ambao wanavipaji lakini wanashindwa kuendelezwa

Alisema kuwa hali hiyo ya kuendeleza vipaji vya watoto itafanya baadhi yao waweze kujiimarisha zaidi hivyo hata kwa nyakati zijazo pia watachangia sana kupunguza tatizo la wataalamu ambalo kwa sasa linaikabili sana Nchi ya Tanzania.

MWISHO

No comments:

Post a Comment