Saturday, March 9, 2013

ARUSHA YAKAMILISHA MPANGO MKAKATI WA UENDELEZAJI WA MAENEO MBALIMBALI YA MIJI


ARUSHA YAKAMILISHA  MPANGO MKAKATI WA UENDELEZAJI WA MAENEO MBALIMBALI YA MIJI


MKOA wa Arusha, umekamilisha mpango mkakati wa kuyaboresha na kuyaendeleza maeneo yote ya miji midogo ambayo hayajaharibiwa kutokana na ujenzi holela ili yawe ni ya mfano.

Hayo yamo katika taarifa ya Utafiti iliyotolewa na mtaalam wa mipango miji kutoka Taasisi ya kimataifa ya maendeleo ya miji, (IIUD) inayoongozwa na Profesa mstaafu wa Chuo kikuu cha Havad, nchini Marekani, Mona Serageldin kutoka nchini Misri ,aliyoiwasilisha kwenye kikao cha pamoja cha watendaji wa jiji la Arusha, Halmashauri ya Meru na halmashauri ya Arusha DC,mwishoni mwa wiki.

Profesa huyo amesema kuwa mpango huo unafadhiliwa naChuo kikuu chaAghakhan, una lengo la kuondoa tatizo la ujenzi holela ambalo halizingatii  ramani ya mipango miji na imesababisha miji mingi duniani kuwa na makazi holela hali ambayo inaharaisha usalama na amani ya wananchi .

ProfesaMuna amesema kupitia taasisi hiyo maeneo mengi ambayo ameshayafanyia utafiti na kukuta hayajaharibiwa hayataharibiwa tena kwa sababu sasa yatajengwa majengo ya mfano .

Amesema anasikitishwa na kushangazwa  na ujenzi holela ambao unaendelea kushika kasi katika maeneo mbalimbali hasa katika miji inayokua huku mamlaka husika zikishindwa kuzuia na kukomesha hali hiyo

Ameongeza  kuwa tayari taasisi hiyo imeshakamilisha kazi hiyo ya utafiti kwa Asilimia 70 kuhusu ujenzi na uboreshaji wa miji inayokuwa bila kuzingatia  mipango mipango miji na matokeo yake ni kuwepo uyoga wa nyumba  ambazo hazikupangiliwa.

Alifafanua kuwa kupitia mpango huo ujenzi holela utakwisha na wananchi watajenga kwa kuzingatia taratibu lengo ni kuwepo na miji iliyopangiliwa ambayo itakuwa ni kivutio.

Kwa upande wake Kaimu mkuu wa mkoa wa Arusha, Nyerembe Mnasa, amesema mara baada ya kukamilika kwa hatua hiyo ya mpango huo itafuatiwa na hatua ya kuwepo na Mapango mkakati (MasterPlan) ya jiji la Arusha na miji mingine mifdogo iliyopo halmashauri za Meru na Arusha Vijijini ambazo zitakuwa na maeneo ya mfano.

Nyerembe, amesema watendaji hawana budi kuunga mkono mpango huo ambao unakusudia kuondoa tatizo la ujenzi holela katika miji mingi nchini ambalo limekuwa ni sugu na kero ya muda mrefu .
 MWISHO

No comments:

Post a Comment