Monday, March 4, 2013

FANYENI KAZI KWA BIDII ILI MUONGEZE UFANISI WA BENKI YETU-MKURUGENZI ACB


FANYENI KAZI KWA BIDII ILI MUONGEZE UFANISI WA BENKI YETU-MKURUGENZI ACB

Na MWANDISHI WETU,ARUSHA

IMEELEZWA  kuwa endapo kama watendaji wa Benki ya Akiba watafanya kazi kwa bidii basi wataweza kuruhusu ushindani wa kibenki hivyo kuweza kutoa ruhusa hasa kwa wateja wake kunufaika na huduma mbalimbali zikwemo huduma za Mikopo


Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Akiba hapa nchini John Lwande,wakati akiongea na wafanyakazi wa benki hiyo kutoka katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro mapema wiki hii

Aidha Lwande alisema kuwa  ipo haja ya wafanyakazi wa Benki kuhakikisha kuwa kamwe hawasababishi dosari zozote za kibenki kwa kuwa kwa sasa kuna wimbi kubwa sana la huduma hizo na badala yake wanatakiwa kuwafanya wateja waridhike na huduma za kibenki hasa kwenye Mikopo

Alifafanua kuwa endapo kama watafanya hivyo basi watakuwa ni miongoni mwa chanzo kikubwa sana cha kufanya mabadiliko ndani ya Nchi ya Tanzania kwa kuwa asilimia kubwa ya watanzania wataendelea kutumia huduma hizo za Kibenki kwa ajili ya maslahi ya Jamii zao


Akiongelea Suala la Mikopo kwa watanzania alisema kuwa  kwa sasa wanajiopanga kuhakikisha kuwa wanaongeza kiasi cha Mikopo ili kuweza kuwafikia watanzania walio wengi zaidi tena hasa wa Mikoa ya Dodoma na Mwanza ambapo wanatarajia kufungua matawi  mengi zaidi kwa maslahi ya shuguli za kibenki kwa wananchi wa  mikoa hiyo.

Alimalizia kwa kusema kuwa pamoja na kuweka mikakati ya kufungua matawi ambayo yataweza kuwasaidia wananchi kwenye masuala ya Kifedha lakini pia Benki hiyo kwa Mkoa wa Arusha na Kilimanjaro  kwa kipindi cha mwaka 2012 waliweza kuvuka malengo hali ambayo imeweza kuinua mapato ya Benki hiyo.

MWISHO

No comments:

Post a Comment