Monday, March 4, 2013

KESI YA MWANDISHI WA HABARI ZA UCHUNGUZI ALIYEUWAWA BURKINAFASO KUANZA KUSIKILIZWA KATIKA MAHAKAMA YA AFRIKA


KESI YA MWANDISHI WA HABARI ZA UCHUNGUZI ALIYEUWAWA BURKINAFASO KUANZA KUSIKILIZWA KATIKA MAHAKAMA YA AFRIKA

Na Queen Lema,Arusha.

Mahakama ya  juu ya haki za binadamu inatarajia kuanza kusikiliza rasmi kesi iyaokabili Serikali ya bukinafaso juu ya mauaji ya Mwandishi wa habari za Uchunguzi Nobert Zongo pamoja na  wenzake watatu wakati wakiwa kazini December 13 mwaka 1998


Akiongea na Vyombo  vya habari mapema jana jijini hapa Afisa habari wa mahakama hiyo Bw jean Pierre alisema kuwa Kesi hiyo itaanza kusikilizwa kuanzia March saba na nane mwaka huu

Jean alisema kuwa kesi hiyo ambayo inaikabili Serikali ya burkinafaso itaweza kusikilizwa na Majaji 11 wa mahakama hiyo huku upande  kwa Upande wa wanasheria  wakitoka katika Nchi za Nigeria na Burkifaso ambao wanasimama kama wanasheria wa walalamikaji

“kesi hii itaendeshwa kisasa zaidi ambapo jopo la majaji wetu watasikiliza na kisha kuharisha kwa mujibu wa sheria za mahakama yetu  hivyo mara baada ya kuhairisha kesi hiyo basi watataja siku nyingine ya kusikilizwa tena’aliongeza Jean

Katika hatua nyingine alisema kuwa pia mahakama hiyo kupitia kwa Raisi wake Sophia Akufye inatarajia kumuapisha jaji Aba Kimelabaou kutoka Burkinafaso kama Jaji wa mahakama hiyo mara baada ya jaji Nyamihala Mulenga wa nchini Uganda kufariki dunia

Alisema kuwa Raisi wa Mahakama hiyo atapisha jaji huyo March 4 katika mahakama hiyo na kisha kuhudhuriwa na majaji 10 kutoka nchi mbalimbali duniani huku lengo likiwa ni kuongezea nguvu mahakama hiyo.

“March 4 mwaka huu tutamuapisha jaji huyu rasmi kama jaji halali kwa ajili ya shuguli mbalimbali za mahakama yetu hivyo pia wadau mbalimbali wa mahakama hii nao watakuwepo pamoja na viongozi wengine ili kuweza kushuhudia kitu ambacho kinaendelea siku hiyo”aliongeza Jean

MWISHO

No comments:

Post a Comment