Monday, March 4, 2013

HAKIKISHENI KUWA HAMUINGILII HAMUHARIBU KAZI ZA WAFADHILI- OLE MEDEYE


HAKIKISHENI KUWA HAMUINGILII HAMUHARIBU KAZI ZA WAFADHILI- OLE MEDEYE

Na Queen Lema,Arusha


Naibu waziri wa nyumba,ardhi na makazi ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Arumeru Magharibi,Goodlucky Ole Medeye amezitaka Serikali za Mitaa ukiwemo Uongozi wa Vijiji Mbalimbali ndani ya jimbo hilo kuhakikisha kuwa kamwe hawaangilii shuguli au miradi mbalimbali ya Wafadhili ambayo ina malengo ya kuwasaidia wananchi

Medeye aliyasema hayo Jimboni humo wakati akizundua zahanati  ya Ester iliopo katika Kijiji cha Ngaramtoni ambayo ilijengwa kwa nguvu za wafadhili kutoka nchini Uingereza kwa malengo ya kudumisha sekta ya afya hasa afya ya mama na mtoto

Medeye alisema kuwa kuwa endapo kama Vijiji vitakuwa vinaingilia masuala ya Miradi ambayo imetolewa na wafadhili kwa malengo mbalimbali ni wazi kuwa malengo hayo yatakwama na badala yake umaskini ndio utakaokirhiri huku jamii ikibaki na mateso mengi

Aliongeza kuwa kazi ya Serikali ya Kijiji ni kuhakikisha kuwa miradi hiyo inafanya kazi kwenye viwango vya hali ya juu kama yalivyokuwa malengo ya wafadhili  hivyo kama Serikali za kijiji zitafanya hivyo basi zitachangia sana mabadiliko tena ya hali ya juu huku mabadiliko hayo yakichangia kupungua kwa umaskini


Awali wanawake ambao ndio walengwa wakubwa sana wa mradi huo walisema kuwa zahanati hiyo itaweza kuwasaidia kwa kuokoa afya zao kwani walikuwa wanalazimika kutembea Umbali wa zaidi ya Kilomita Kumi kwa ajili ya kutafuta huduma za afya hali ambayo wakati mwingine husababisha vifo

“kabla hii zahanati ya ester haijaja tulikuwa tunatoka hapa mpaka Selian au mara nyingine tunaenda mpaka Mjini au Kaloleni sasa wakati huo kama unaumwa sana unaweza kupoteza maisha kutokana na umbali ila kwa sasa tuna uhakika wa kupata huduma bora tena za afya ya mama na mtoto’waliongeza wanawake hao

Mwisho

No comments:

Post a Comment