Thursday, March 14, 2013

WANAWAKE 33 WAPEWA ELIMU ILI WAJIKOMBOE


WANAWAKE wapatao 33 kutoka tarafa ya Manyara, wilayani Monduli, mkoa wa Arusha wamenufaika na elimu ya ujasiliamali, Afya ya uzazi, stadi za maisha na ukimwi iliyotolewa na shirika lisilo la kiserikali kutoka nchini Ujerumani liitwalo DSW.

Mafunzo hayo ya siku tano yalifanyika kwenye eneo la Mto-wa-Mbu, na kuwashirikisha wataalam kutoka Mradi wa Kuwawezesha Wanawake na Wasichana (WOGE)

Akizungumza juzi, mmoja wa wakufunzi kutoka mradi wa WOGE, Daudi Tano alisema: “Lengo la mafunzo hayo ni kumjengea uwezo mwanamke ili aweze kujitambua yeye kama yeye,mambo muhimu ya kufanya kwenye jamii,pamoja na jinsi ya kujikinga na maambukizi ya Ukimwi


Mtaalam huyo alisema mafunzo hayo yalilenga kumkomboa mwanamke kutokana na changamoto nyingi anazakabiliana nazo katika maisha yake ya kila siku.

Alifanunua kuwa WOGE ni mradi wa kikanda ambao unatekelezwa kwenye nchi za Tanzania, Kenya, Uganda na Ethiopia ukilenga zaidi kuwakwamua wanawake na wasichana walioko pembezoni hasa wale wa vijijini. Nchini Tanzania

“Mradi unawalenga zaidi wanawake wa vijijini walio na umri kati ya miaka 16 na 55, ambao wapo kwenye ajira isiyo rasmi na ambao hawapo shuleni ama hawana ajira,” alisema,

Pia aliongeza  kuwa madhumuni ya mradi huo ni kutoa mchango katika jitihada za kupambana na umaskini kwa kuwawezesha wanawake na wasichana ili waweze kusimama wao wenyewe kichumi na kutokuwa wategemezi.


Naye Afisa ustawi wa jamii Tarafa ya Manyara, Denis Magiye alilishukuru shirika la DSW kwa elimu hiyo na kuyataka mashirika mashirika mengine kuiga mfano huo ili kumkomboa mwanamke na msichana wa Kitanzania.

Alisema elimu ya uzazi inahitajika sana katika nyakati hizi kwani uzazi wa mpango humpatia mwanamke uhuru wa kufanya shughuli zake za kuinua kipato cha familia.

“Kuzifahamu njia za uzazi wa mpango kutawasaidia hata kupunguza idadi idadi ya watoto ambao hawajatarajia kuwapata na pia kupunguza vifo vinavyotokana na masuala ya uzazi,” alisema.

MWISHO

No comments:

Post a Comment