Tuesday, March 26, 2013

MKAPA FOUNDATION YATOA MAFUNZO KWA TIMU ZA USIMAMIZI WA AFYA KUTOKA KATIKA WILAYA 132 HAPA NCHINI

NA MWANDISHI WETU,ARUSHA

MKAPA FOUNDATION YATOA MAFUNZO KWA TIMU ZA USIMAMIZI WA AFYA  KUTOKA KATIKA WILAYA 132 HAPA NCHINI

TAASISI ya Mkapa Foundation imefanikiwa kutoa mafunzo timu za usimamizi wa afya kwenye Wilaya 132  hapa nchini huku  mafunzo hayo yakiwa na malengi ya kuwajengea uwezo wa rasilimali watu ili waweze kutoa huduma bora zaidi za afya katika maeneo yao ya kazi.

Hayo yamebainishwa na Afisa Mpango kitengo cha uwezehsaji katika taasisi hiyo,Bi Pamela Chiwa wakati akiongea na wataalamu wa afya kutoka katika vituo vya afya ndani ya kanda ya kaskazini mapema jana

Aidha Pamela alisema kuwa timu hizo za usimamizi wa afya katika ngazi ya Wilaya ziliweza kupatiwa mafunzo hayo ya rasilimali watu  yaliweza kudumu hapa nchini kwa muda wa mwaka mmoja ambapo mpaka sasa mafanikio  makubwa sana yameshonekana katika sekta hiyo ya Afya

Alifafanua kuwa mbali na kuweza kuwajengea uwezo wataalamu hao wa afya ambao ni timu za usimamizi wa afya lakini sasa wanashuka zaidi ambapo wanalenga pia kuwapa mafunzo kama hayo hayo wataalamu wa afya kutoka katika vituo vya afya.

Alibainisha kuwa yote  hayo ambayo yanafanyika chini ya Taasisi ya Mkapa Foundation yanalenga kuhakikisha kuwa kila watanzania wanapata huduma bora na kwa wakati ili kuokoa maisha ya watu wengi zaidi ambao ndio nguvu kazi ya taifa la leo


Katika hatua nyingine alisema kuwa nao wataalamu wa afya wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanaachana na dhana inayosema kuwa wataalamu wa afya ni wachache katika vituo,na hata hospitali bali wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanafanya kazi tena kwa ubora wa hali ya juu hata kama wapo wachache

Hataivyo alisema kuwa kama wataalamu hao watafanya kazi kwa ubora ambao unatakiwa basi watachangia sana huduma za afya kuweza kuboreka zaidi ya sasa huku hali hiyo pia itachangia kwa kiwango kikubwa maendeleo ya Nchi  hivyo hata malengo ya Taaasisi hiyo ya Benjamini Mkapa nayo yataweza kufanikiwa kwa kiwango cha hali ya juu sana.

MWISHO

No comments:

Post a Comment