Wednesday, February 20, 2013

TANZANIA INAHITAJI NYUMBA MILIONI TATU –NHC


TANZANIA INAHITAJI NYUMBA MILIONI TATU –NHC

Na Queen Lema,Arusha

TANZANIA ina mahitaji ya Nyumba Milioni Tatu ambapo kwa  sasa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limeweka mikakati ya kuhakikisha kila mwaka inajenga nyumba zaidi ya elfu tatu ili kupunguza tatizo hilo hapa Nchini

Hayo yamelezwa na Waziri wa Ardhi,nyumba, na maendeleo ya makazi,Profesa Anna Tibaijuka leo wakati akizundua mradi wa nyumba za makazi katika eneo la Levolosi ambazo zimejengwa chini ya Shirika la nyumba

Tibaijuka alisema kuwa  mahitaji hayo ya nyumba kila mwaka yanaongezeka kwa kiasi cha nyumba laki tatu lakini ongezeko hilo ni lazima liweze kupunguzwa tena kwa haraka sana kwa kubuni aina mbalimbali ya nyumba ambazo zitarahisisha makazi bora na imara

Aliongeza kuwa Hitaji ni kubwa sana la nyumba hapa nchini hivyo jitiada za haraka sana zinahitajika katika kuhakikisha kuwa hata nyumba ambazo zinajengwa ziweze kuwa imara na ziweze kuwasaidia hata zaidi wananchi wa vijiijini ambao mara nyingine wanaonekana kukosa nyumba bora na imara

Alisema kuwa kama Shirika hilo amblo kinaendeshwa lenyewe litaweza kuwa bunifu na kujenga nyumba nyingi zaidi basi litachangia kwa kiwango kikubwa sana ongezeko hilo la nyumba zaidi ya Laki tatu kwa kila mwaka kuweza kupungua na hata baadhi ya miji kuweza kupangika kwa uraisi sana

“Tanzania kwa sasa tunakabiliwa na changamoto hii lakini ni vema sasa Shirika kwa kushirikiana na wadau mbalimbali tukahakikisha kuwa tunasonga mbele zaidi na hata kuangalia jinsi ya kupunguza tatizo hilo ambalo kama halitaaweza kutatuliwa kwa uraisi basi litasababisha madhara kwa kuwa wapo baadhi ya watu ambao watakosa sehemu za kuishi’aliongeza Tibaijuka

Katika hatua nyingine alisema kuwa nao wanasiasa wana nafasi kubwa sana ya kushirikiana na Shirika hilo kwa kuwa bado shirika hilo linakabiliwa na changamoto mbalimbali kama vile kushindwa kujenga kutokana na Ardhi ambayo inauwza kwa bei ya juu sana lakini kama watasaidiana basi wataweza kutatua changamoto hiyo ambayo nayo inafanya shirika hilo kushindwa kuendelea kujenga nyumba nyingi zaidi

Awali mkurugenzi mkuu wa Shirika hilo Nehemia Mchechu alisema kuwa ili kukabiliana na tatizo hilo la ongezeko la mahitaji ya Nyumba  hapa Nchini Shirika hilo limeweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha kuwa mpaka 2014 watakuwa tayari wameshajenga nyumba elfu kumi na tano huku kila mwaka wakijenga nyumba elfu tatu

Mbali na hayo alisema kuwa kwa Mkoa wa Arusha wanatarajia kuanza kujenga nyumba za garama nafuu katika wilaya ya Arumeru pamoja na Arusha huku lengo halisi likiwa ni kuhakikisha kuwa mji wa Arusha unaendelea kuboreka zaidi kwenye hadhi za kimataifa na kuachana na ujenzi holela ambao mara nyingine unasababisha ukosefu wa nyumba

MWISHO

No comments:

Post a Comment