Tuesday, July 17, 2012

WANANCHI WAGOMEA MRADI WA BENKI YA DUNIA


MRADI wa ujenzi  dampo la kisasa wenye thamani ya shilingi bilioni 3 unofadhiliwa na benki ya dunia katika jiji la Arusha, upo hatari  kuyeyuka kufuatia wananchi wa kata ya Muriet manispaa ya Arusha kugoma kupisha eneo la  mradi huo licha ya kulipwa stahili zao .

Aidha mradi huo ambao ulikuwa uanze tangu april mwaka jana umeshindwa kuendelea kutokana na mvutano mkali ulipo kati ya wananchi zaidi ya 200 na manispaa ya jiji la Arusha ,ambapo wananchi hao wameilalamikia manispaa hiyo kwa kushindwa kuwalipa fidia ya maeneo yao waliyoyaendeleza ,huku manispaa hiyo ikidai imeshawalipa.

Akizungumzia swala hilo , Mkurugenzi wa manispaa ya Arusha, Bw Estomih Changa’h alikiri wananchi hao kuwa kikwazo cha kuanza kwa mradi huo huku akidai kuwa wafadhili wa mradi huo ambao tayari walionyesha nia na kuja na kupima katika eneo hilo wameanza kukata tamaa.

Alifafanua kuwa , baada ya kufanya tathmini ya awali mwaka jana walibaini kuwa wananchi 42 ndio  waliopo ndani ya  eneo husika la mradi ,hivyo manispaa ya Arusha ilifanya tathimin na kukubali kuwalipa  kiasi cha shilingi milioni 252 kama fidia ya makazi yao.

‘’tulipofanya tathimini ya makazi yao tulikubaliana kuwalipa wakazi hao 42,na kila mtu alipigwa picha akiwa amesimama mbele ya eneo ama nyumba yake,sasa tunasikitika sana kuona wakiendelea kunga’ng’ania huku kundi lingine la watu zaidi ya 200 wakiibuka kutaka nao walipwe fidia’’alisema Bw Chang’ah

Alisisitiza kuwa,tayari manispaa imeshawalipa wananchi 33 kati ya 42 kwa kiwango tofauti na kubaki wananchi tisa tu ambao walikuja kurubuniwa na kugomea malipo hayo.


Aliongeza kuwa, wananchi hao wamekuwa wakifika katika ofisi ya manispaa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha kudai fidia zao ambapo wamekuwa wakijaribu kuwaelewesha na uendesha vikao kadhaa, lakini wamekuwa wagumu kuelewa .


Mwenyekiti  wa kamati ya waathirika hao ,Jackson Japhet alisema kuwa, wao wanachotaka ni kutaka kulipwa fidia stahili ya makazi yao kwani  wengi wa wananchi wamekuwa wakiishi hapo muda mrefu na wamekuwa na makazi ya kudumu ,hivyo ni ngumu sana wao kuondoka katika eneo hilo.

Wakizungumza katika kikao cha hadhara katika eneo hilo la Muriet mwishoni mwa wiki, wameazimia kwenda mahakamani kusimamisha uanzishaji wa mradi huo  hadi manispaa hiyo itakapofanya tathimini upya kwa kuwashirikisha wananchi hao na kuwalipa fidia stahili bila kuwapunja.

Mwisho
SERIKALI imesema kuwa ipo kwenye mchakato wa kuviboresha viwanja mbalimbali vya ndege hapa nchini ukiwemo uwanja wa ndege wa Arusha kwa kuufanyia matengenezo makubwa uweze kuruhusu kutua kwa ndege kubwa za kimataifa.

Waziri wa uchukuzi ,dkt Harisson Mwakyembe aliyesema hayo jana baada ya kupokea taarifa fupi wakati akiongea na wafanyakazi wa kiwanja cha ndege cha Arusha baada ya kufanya ziara fupi mkoani hapa.

Dkt Mwakyembe alisema kuwa uwanja wa ndege wa Arusha unaumuhimu wa kipekee katika kuendeleza utalii wa ndani na kueleza kuwa serikali itafanya kila njia kuhakikisha kuwa uwanja huo unapanuliwa na kuwa na uwezo wa kutua ndege kubwa.

Alisema amekuwa akipata malalamiko mengi kuwa uwanja huo umekuwa ukitumika kunyangánya wateja wa uwanja wa kimataifa wa Kilimanjaro(KIA) huku maombi hayo yakitaka uwanja huo ufungwe.

‘’nimepata taarifa za kutaka kufungwa kwa  uwanja huu wa ndege wa Arusha kwa kuwa unatumika kunyangánya abilia wa uwanja wa KIA ,nimejiridhisha kuwa kiwanja hiki kina umuhumu wa kipekee na serikali itaangalia uwezekano wa kukiboresha’’alisema Mwakyembe.

Alisema serikali itatenga fedha zaidi  kwa ajili ya kukiboresha kiwanja hicho ili kiwe cha kisasa zaidi ,ikiwa ni pamoja na kuviboresha viwanja vingine vya Songwe,Kigoma na Mwanza.

Awali Kaimu mkurugenzi wa kiwanja cha ndege cha Arusha,Mhandisi Suleiman Suleiman alisema kuwa kiwanja hicho kinakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo ukosefu wa eneo la maegesho ya ndege, jengo la abilia na jengo  la zima moto.

Alisema changamoto zingine ni pamoja na kutokuwa na taa zinazowaka majira ya usiku hivyo kutoruhusu ndege kutua ama kuruka nyakati za usiku,kituo cha umeme ,Mnara wa kuongozea ndege ,Jengo la hali ya hewa ,jengo la Mizigo  pamoja na miundombinu yake.

Aidha alisema kuwa ukarabati wa kiwango cha lami wa barabara ya kuruka na kutua yenye urefu wa mita 420 uliogharimu kiasi cha shilingi bilioni  1.7umefanya urefu wa barabara hiyo kufikia mita 1620 hivyo kuwezesha  ndege zenye ukubwa wa kubeba abilia 70 kuweza kutua katika kiwanja hicho.

Mhandisi Sulemeni aliongeza  kuwa kwa sasa kiwanja hicho kinahudumia wastani ndege 1700 kwa mwaka na abilia wanaohudumia kwa mwezi ni 12,000.

Alisema kuwa mpango wa sasa ni kuhamisha barabara ya Arusha Babati na tayari wamemweleza wakala wa barabara mkoani Arusha(Tanroads).

Aliongeza kuwa hatua hiyo itasaidia kuondoa msongamano uliopo sasa, pamoja na kuhamisha barabara ya sasa ya kuingia kiwanjani hapo kwani inaingiliana na maegesho.

No comments:

Post a Comment