Friday, July 20, 2012

MAKANISA YATAKIWA KUOMBEA MASLAI YA WAFANYAKAZI WAKE



,ARUSHA

WITO umetolewa kwa makanisa mbalimbali hapa nchini kuhakikisha kuwa yanajiwekea utaratibu wa kuombea mapato ya wafanyakazi wake kwa kuwa wengi wamekuwa wakipoteza hata haki zao  za msingi

Kauli hiyo imetolewa mjini Arusha na mchungaji Joel Kessoi  katika kanisa la Ngome ya Yesu lilopo Kisongo

Aidha mchungaji huyo alisema kuwa kwa sasa maslahi ya wakristo wengi sana wanaibiwa ovyo kwa kuwa baadhi ya waajiri wanashindwa kuwalipa na baadaye wakristo hao wanaishia kuteseka

Alisema kuwa endapo kama kanisa litasimama katika nafasi yake na kuanza maombi yake basi waajiri hasa wa viwanda ambao wananyima haki zao  na badala yake kuanza kuwakata wafanyakazi makato ambayo hayastaili.

“ukiangalia hawa wafanyakazi wa Viwanda kila siku wanalia na shida lakini wa nahaki sana ya kuweza kufanya kazi zao na kupewa wanachokitaka lakini kwa sasa kazi zao nyingi sana zimeingiliwa na shetani na wanakatwa hata makato ambayo hayastaili kwa kweli”aliongeza mchungaji Joel

Pia alisema kuwa kama kanisa litaendelea kuangalia suala hilo ambalo ndilo chanzo cha umaskini wa makanisa ya leo basi nafasi ya maombi inatakiwa kuanza kutumika katika kuombea wafanyakazi na makato yao

Alifafanua kuwa kwa kuanza kanisa hilo limeanza na mchakato wakuombea  wafanyakazi wa kiwanda cha A- Z ambao nao wamekatwa sana makato mengi ambayo hayana faida na wafanyakazi

Alisema kuwa kila mara watakuwa wanaombea wafanyakazi wa makampuni na viwanda mbalimbali katika maombi maalumu ili wawezen kufikia malengo yao ya msingi ambayo wamejiwekea na kuacha kuonewa hasa wakati wa kupewa haki zao

MWISHO

No comments:

Post a Comment