Friday, July 20, 2012

MARUFUKU MASHOGA WA KIKE KUONGOZA FAMILIA ANAYEONGOZA FAMILIA HATA KAMA NI DUNI NI MWANAUME PEKEE – ASKOFU NGOY NGOY



HABARI NA QUEEN LEMA,Arusha

WANAWAKE wa kikristo wametakiwa kuacha tabia ya kuwatumia marafiki kwenye ndoa zao kwani takwimu zinaonesha kuwa ndoa nyingi sana za kikristo zinakufa kutokana na marafiki kuwa ndio vichwa badala ya Mume

Hayo yamebainishwa na Askofu Nassor Ngoy Ngoy wa kanisa la Reboth Victory Church lilopo Maeneo ya Mianzini wakati akiongea na waumini  wa kanisa hilo katika ibada ya ndoa iliyofanyika kanisa hapo jumapili iliyopita

Askofu huyo alisema kuwa wanawake wanapswa kujua na kutambua kuwa hakuna kichwa cha familia bila ya mwanaume na kutokana na hali hiyo alisema kuwa kwa sasa ndoa nyingi zinaongozwa na marafiki wa kike hali ambayo inachangia sana kuvunjika kwa ndoa.

Alifafanua kuwa hali hiyo ambayo ni chukizo na ndio chanzo kikubwa sana cha kuvunjika kwa ndoa zilizo nyingi zinapswa kuachwa mara moja na badala yake wanawake wakahakikisha kuwa wanakuwa na vifua ambavyo vitatunza Siri,

“inasikitisha sana kuona marafiki wanakuwa wao ndio baba na wao ndio mama kwenye ndoa wakati hata maandiko hayasemi hivyo sasa hali hii inachangia kwa kiwango kikubwa sana baadhi ya watoto kuteseka na wengine wanakesha wakiwa wanamtafuta shetani wakati shetani wanamkaribisha wao wenyewe”aliongeza Askofu Ngoy Ngoy

Pia aliongeza kuwa endapo hata kama ndoa ina shida kwa kiasi kikubwa sana basi siri ya ndoa ile anatakiwa kuijua na kutambua ni baba mlezi ambaye ni mchungaji na wala sio Shoga kwani ataweza kukupitisha katika mpango wa Mungu  ambapo ndiko kuna chimbuko kubwa sana la misingi ya ndoa

Aliongeza kuwa ili ndoa idumu ni lazima kila mwanandoa hasa wanawake wawe na uwezo wa kujiwekea tabia ya siri sanjari na kutafuta kweli ya mungu na wala sio kuongea ili kuweza kuwafuraisha marafiki walio wengi wakati ndio msingi wa kuvunjika kwake

Aidha aliwataka wana ndoa ambao wanatofauti za kidunia kuendelea kuwaombea wenzao kwa maombi ambayo yatasababisha imani zao za kidunia kubalika na kuja kwenye mfumo wa kimungu kwa kuwa chanzo cha ufalme wa mungu pia kinaanzia kwenye ndoa

“ndani ya ndoa unaweza kukuta mtu mmoja ameokoka lakini kwa kuwa mwenzako wako bado hajamjua Mungu kila mara unamdharau na kumuona hafai au unakuta hata wengine wanadiriki kuwakimbia na kutaka wapate wake au wanaume waliokoka sasa hii siyo suluhisho la ndoa ambazo ni imara bali ndoa imara ni ile inayomjua na kumtafakari zaidi Mungu”aliongeza Askofu Ngoy Ngoy.

MWISHO

No comments:

Post a Comment