Tuesday, July 17, 2012

ACHENI KUWAZIA UTAJIRI NA MALI ZA KIDUNIA BALI ANGALIENI UTUKUFU WA MUNGU KWANZA



IMEBAINIKA kuwa asilimia kubwa ya wakristo wanashindwa kufikia malengo yao mbalimbali kwa kuwa wameweka mawazo yao zaidi kwenye vitu vya kidunia kuliko kwa Mungu  hali ambayo inachangia kwa kiwango kikubwa sana Umaskini wa leo

Hayo yameelezwa na Mchungaji Japhet Nanyaro wa kanisa la T.A.G Patmo Nkoanekoli  wilayani Meru  mkoani hapa wakati akiongea na waumini wa kanisa hilo wiki iliyopita

Alisema kuwa asilimia kubwa ya watu wanawaza sana fedha na utajiri wa dunia kuliko kuwaza na kutafakari utukufu wa Mungu hali ambayo inachangia sana kushindwa kusonga mbele zaidi katika matarajio yao mbalimbali

Aliongeza kuwa zipo hasara ambazo zinachangia kwa kiwango kikubwa sana ambazo zinatokana na kutafakari maisha ya kimwili kuliko maisha yale ya kiroho ambayo ndiyo yanayodumu zaidi hata baada ya maisha ya hapa duniani.

“ndani ya maisha ya leo unakuta kila mtu anatafakari jinsi atakavyoweza kupokea mali na fedha lakini hata kuchukua dakika moja na kumrudishia Mungu utukufu hamna sasa je tunasahau kuwa ambaye ametupa nguvu zaidi ya kuwaza tunamuacha wakati yeye ndiye muamuzi wa kila kitu ni vema sasa tukabadilika”alisema Mchungaji Nanyaro.

Awali alisema kuwa ni vema kama mawazo ya watu wa sasa wakabadilisha mtizamo wao na kumrudia mungu kwani hata hali ambazo zinawakabili watu wengi kwa sasa  kama vile Umaskini zinachangiwa  sana na kutafakari maisha ya kimwili kuliko yale ya Kiroho

Pia alisema kuwa ukiwa unataka utajiri wa kudumu hapa duniani ni lazima kwanza umtumike Mungu kwa moyo wako wote ili uweze kuzidishiwa yale yote ambayo unayataka ambapo ndio kusudio la mungu kumbariki yeyote yule ambaye analenga kumtegemea katika maisha yake yote ya hapa duniani

“Maandiko yanasema kuwa tunapswa kujua na kutambua kuwa tunatakiwa kusumbukia kwanza ufalme wa Mungu ili mengine yote tuweze kuzidishiwa na unapomsumbukia Mungu unapata hata kwa njia ambazo hauzijui sasa kwa nini usumbukie maisha yako wakati Mungu anaweza kukusumbukia kwa moyo wake wote”aliongeza Mchungaji Nanyaro

MWISHO

No comments:

Post a Comment