Tuesday, April 9, 2013

TUMIENI KAMUSI HATA MNAPOKUWA MADHABAHUNI-JOKA KUU


TUMIENI KAMUSI HATA MNAPOKUWA MADHABAHUNI-JOKA KUU

Na Bety Alex,Arusha

Mchungaji Herbert Anthony”Joka kuu”amewataka watumishi wa Mungu kuhakikisha kuwa wanafundisha masomo yao ya kila siku kwa waumini wakiwa na uhakika wa maneno lakini kama hawana uhakika basi wahakikishe kuwa wanatumia kamusi ili kujiepusha na tabia ya kupotosha maana ambazo wakati mwingine zinachangia sana kumtukuza Shetani kwa siri.

Kwa sasa hata unaposema neno unatakiwa kujua maana ya lile neno ambalo umelisema kwa kuwa maneno ya sasa yanachukuliwa kivingine kabisa  lakini kama mtumishi wa  Mungu unashindwa kujua na kutambua  maana basi tumia hata kamusi

Joka kuu aliyasema hayo jijini hapa wakati akiongea na waumini wa kanisa hilo mapema wiki hii  katika somo lilolokuwa lina husuurejesho wa afya ambapo alidai kuwa hata maneno ya sasa yanatakiwa kuchunguzwa kabla ya kutamkwa

Alidai kuwa kwa kutumia kamusi kutaweza kuwafundisha wakristo  maneno ambayo yana maana lakini kama watumishi wa mungu watakuwa wanachukua maneno bila ya kuyachuja kutasababisha mafundisho ambayo wanayatoa kwenye ibada zao  ya bure huku watu wakizidi kuangamia zaidi katika dhambi

“dunia ya sasa kwa kweli imebadilika sana hivyo basi kuliko uhubiri neno ambalo hujui maana yake ni bora unyamaze kimya kabisa unakuta mtumishi anasema kuwa ninyi ni wajanja akijua kuwa mjanja ni mtu mwenye kiwango bora kumbe neno mjanja linamaanisha mtu tapeli tapeli,sasa hapa unaona kuwa shetani anaweeza kutawala badala  Mungu aweze kutawala”aliongeza Joka kuu

Awali akiongelea  somo hilo la Urejesho wa afya ndani ya jamii ya sasa alidai kuwa Tanzania ya leo imekumbwa na magonjwa mengi sana kwa kuwa wengi wamesahau kweli ya Mungu tofauti na Miaka iliyiopita ambapo magonjwa hayo wakati mwingine chanzo chake kikubwa ni Dhambi

Alifafafnua kuwa dhambi zinapozidi maali basi kinachofuata hapa ni magonjwa  na mateso ya kila siku lakini kwa sasa wakristo pamoja na watanzania kwa ujumla wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanarejea katika torati ya bwana ili bwana mwenyewe aweze kupunguza kasi ya magonjwa ambayo ndio umaskani wa baadhi ya watu.

“ukiangalia kwenye vyombo vya habari ubakutana na mambo na unyama wa hali ya juu sana ambao unafanywa na watu ambao mwisho wake huishia kusababisha kilema cha ugonjwa sasa  inabidi wakristo tuamke na tukatae hali kama hizi na badala yake turudi katika torati’aliongeza Joka kuu

Alimalizia  kwa kuwataka wakrsito wahakikishe kuwa wanafanya urejesho na kuachana na tabia ya kuchukulia  lugha na mambo mengine kiraisi bali wahakikishe kuwa wana ishi vema ikiwa ni pamoja na kutojihusishaa na dhambi ambazo ambazo ndizo zinazozaa maovu katika dunia

MWISHO

No comments:

Post a Comment