Tuesday, April 9, 2013

INSERT KWA KUSHIRIKIANA NA JUKWAA LA WAZEE LATARAJIA KUJENGA KITUO CHA WAZEE WA MKOA WA ARUSHA


INSERT KWA KUSHIRIKIANA NA JUKWAA LA WAZEE LATARAJIA KUJENGA KITUO CHA WAZEE  WA MKOA WA ARUSHA

Asasi ya Informal Sector team(INSERT)Kikiana na jukwaa la  wazee wa mkoa wa Arusha wanatarajia kujenga kituo kwa ajili ya makazi ya wazee ambapo kituo hicho kitagarimu kiasi cha zaidi ya Milioni 150 huku lengo likiwa ni kusaidia wazee ambao hawana uwezo ndani ya mkoa wa Arusha

Akizungumza katika jukwaa la wazee wa mji wa Arusha (JUWA) mratibu wa  jukwaa hilo bw  Javes Sauni alisema kuwa mpaka sasa kuna mikakati mbalimbali ya kuanza marra moja ujenzi wa kituo hicho cha wazee kwa mkoa wa Arusha

Alitaja kuwa mikakayi hiyo inasema kuwa kituo hicho cha wazee kitajengwa katika eneo la Kisongo ambapo kituo hicho kwa mara ya kwanza kitaweza kuhudumia wazee zaidi ya 60  hasa wale ambao wanatoka katika mazingira magumu

Aliongeza kuwa endapo kama mpango huo wa hivi karibuni utaweza kufikiwa tena kwa haraka basi utaweza kuwa  na faida kubwa sana kwa wazee wa mkoa wa Arusha kwa kuwa baadhi yao wanakabiliwa na hali ngumu ya maisha huku wengine  nao wakiwa wanakabiliwa na ukosefu wa mahala pa kuishi

“hili jukwaa la wazee limeona kuwa upo umuhimu tena mkubwa sana wa kuhakikisha kuwa tunaangalia zaidi maslahi ya wazee hasa wale ambao wanatokea katika mazingira magumu lakini njia mojawapo ya kuweza kuwasaidia wazee hawa ni kuhakikisha kuwa kwa kiasi Fulani wanakuwa na kituo ambacho kama sio kukutanika pale na kuongea masuala yao ya wazee lakini pia kitasadiia sana kuokoa maisha ya wengi”aliongeza Sauni

Wakati huo huo alisema kuwa kwa sasa bado asilimia kubwa sana ya wazee hasa wa mji wa Arusha wanakabiliwa na changamoto kubwa sana ya matibabu hali ambayo wakati mwingine husababisha vilema vya kudumu au vifo hasa kwa wazee ambao wanatoka katika familia ambazo hazina uwezo

Pia alisema kuwa kutokana na changamoto hiyo watatumia jukwaaa la wazee kwa kuhakikisha kuwa wanatafuta mbinu mbadala ambazo zitaweza kuwaokoa wazee hasa wale ambao hawana uwezo wa kujitibu ikiwa ni pamoja na kukosa hata fedha kwa ajili ya manunuzi ya dawa

“hii ni changamoto kubwa sana ambayo inawakabili wazee wa mkoa wa Arusha lakini tutatafuta mbinu mbadala na kuhakikisha kuwa wazee wanapata matibabu kwa kuwa tayari Serikali ilishatoa Agizo lakini vituo vya afya vya  Mjini hapa bado havitekelezi sera hiyo pamoja na Tamko hilo”alifafanua  Bw Sauni

No comments:

Post a Comment