Wednesday, July 24, 2013

UKOSEFU WA GARI LA KUBEBEA MAZIWA WASABABISHA MAZIWA LITA 700 KUSHINDWA KUUZIKA KILA SIKU WILAYANI KARATU



Kiwanda Cha Ayalable Dairy kilichopo katika Wilaya ya Karatu Mkoani
Arusha kinakabiliwa na changamoto ya usafiri hali ambayo inasababisha
waweze kupokea maziwa lita 800 kwa siku badala ya lita 1500 kwa siku
moja kutoka kwa wafugaji jambo ambalo wakati mwingine linasababisha
hasara kubwa sana kwa wafugaji pamoja na matumizi mabaya ya maziwa

Akiongea na Waandishi wa habari wiki hii wilayani humo mtaalamu wa
maziwa wa wilaya hiyo ambaye ni Care Elias alisema kuwa changamoto
hiyo inasababisha madhara makubwa sana kwa wafugaji

Alifafanua kuwa hapo awali walikuwa wanapata maziwa machache sana
kutoka kwa wafugaji lakini kwa sasa maziwa ni mengi sana katika wilaya
hiyo ya Karatu ingawaje sehemu nyingi sana zenye maziwa bado zipo
mbali na eneo la mji hali ambayo inasababisha maziwa yashindwe kufika
katika kiwanda hich

Kutokana na changamoto hiyo alidai kuwa maziwa yanayopatikana kwa
ajili ya matumizi ya kiwanda ni machache sana ingawaje kwa huko
viijijini zaidi maziwa yanazalisha lakini yanashindwa kufika kiwandani


Akiongelea hali ya uzalishaji wa maziwa katika Wilaya hiyo ya Karatu
alidai kuwa uzalishaji wa maziwa umeongezeka sana tofauti na Miaka ya
nyuma ambapo Wilaya hiyo ilikuwa inapata maziwa kidogo sana

Alisema kuwa kwa sasa kiasi cha lita zaidi ya elfu nne kinazalishwa na
wafugaji wa Wilaya hiyo ya Karatu lakini hapo awali kiasi cha lita
elfu moja pekee ndicho kilichokuwa kinazalishwa hali ambayo wakati
mwingine ilikuwa inasababisha uhaba wa maziwa

Alimalizia kwa kusema kuwa pia kituo hicho kilijengwa kwa ufadhili wa
Mamlaka ya Ngorongoro hivyo basi ili kuweza kuokoa kiasi kikubwa cha
maziwa ambacho kinapotea kila siku ni vema kama mamlaka hiyo ingeweza
kuangalia upya tena namna ya kuwapa gari ambalo litaweza kubeba maziwa
hayo kutoka Vijijini zaidi na kuleta katika kiwanda hicho cha Ayalabe

Mwisho

No comments:

Post a Comment