Wednesday, July 24, 2013

NGORONGORO YATOA NGOMBE 20 ZENYE THAMANI YA MILIONI 20 KWA WANACHI WA WILAYA YA KARATU



Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro(NCAA)imefanikiwa kutoa Ngombe 20 wa
kisasa wenye thamani ya zaidi ya milioni 20 kwa vijiji vinne vya
Wilaya ya Karatu kwa madhumuni ya kuendeleza Uhifadhi wa maliasili
ndani ya Vijiji hivyo.

Akiongea na waandishi wa habari mapema wiki hii Afisa Ugani wa Mamlaka
hiyo ambaye ni Bw Salustin Hallu alisema kuwa huo ni moja ya miradi
inayotekelezwa na mamlaka hiyo

Alisema kuwa mradi huo ambao hapo awali ulianza rasmi na Ngombe wa
kisasa 20 uliweza kuwa na manufaa makubwa sana kwa Vijiji vya Troma,
Ayalabe, lositete,na Upperutele ambapo hapo awali baadhi ya wafugaji
kwenye vijiji hivyo walikuwa wanalazimika kuchunga ndani ya hifadhi

Alifaafanua kuwa mpaka sasa zaidi ya familia 98 kwenye mradi huo
tayari wameshanufaika kwa kuwa kila familia moja sasa ina ngombe wa
kisasa mmoja na lengo halisi likiwa ni kuhakikisha kuwa kila familia
inajijengea uwezo wa kuchunga ndani na wala sio kutoa mifugo kwenda
kutafuta malisho nje

“Ngorongoro inalinda sana ujirani mwema na wananchi wake na ndio maana
tukaona kuwa badala ya kuwakataza tu wananchi wasiingie kwenye pori
ambapo ni hatari kwa maisha yao wao pamoja na mifugo lakini pia tuwape
mbinu mbadala za kuhakikisha kuwa wanajikomboa ndio maana tukaanzisha
huu mpango ambao umeonekana kuwasaida sana wananchi wa hivi
vijiji”aliongeza bw Hallu

Awali alisema Mamlaka pia bado ina mkakati mbalimbali wa kuhakikisha
kuwa wanaweza kufikia familia zote sanjari na kuwapa elimu mbalimbali
juu ya umuhimu wa kufuga ndani laki ni pia kuwapa mbinu imara ambazo
zinatakiwa kutumiwa na wafugaji wa kisasa zaidi

Akiongea kwa niaba ya familia 98 ambazo zimenufaika na mradi huo wa
ngombe wa kisasa kutoka Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro bi Emirita
Martin alidai kuwa pamoja na kuwa wamepata Ngombe lakini bado Mradi
huo unapaswa kuongezewa ngombe ambao wataweza kuwanufaisha wanawake

Bi Emirita alibainisha kuwa kama kila Boma na familia zitapa Ngombe
mmoja ambaye atazaliana basi wakina mama wataondokana na dhana ya kuwa
tegemezi kwenye maisha ya kifamilia kwani ufugaji unabadilisha maisha
duni na maskini ambayo wanayo baadhi ya wanawake katika Wilaya hiyo ya
Karatu

MWISHO

No comments:

Post a Comment