Wednesday, July 24, 2013

MAAFISA MAENDELEO YA JAMII 120 WAFUNDWA


ZAIDI ya maafisa maendeleo ya jamii 120 wa halmashauri za wilaya na
wakuu wa Vyuo vya maendeleo ya wananchi wapatao 36 katika mikoa
mbalimbali nchini wamepewa mafunzo malumu  yanayohusu haki za watoto
,ikiwemo Uhsai, Ulinzi, Maendeleo  Ushiriki wa bila kubaguliwa ili
waweze kuzilinda na kuhakikisha hakuna mtoto anayenyanyaswa.

Hayo yamo katika hotuba ya mkuu wa mkoa wa ARusha, Madesa Mulongo,
aliyoyatoa hivi karibuni katika maadhmisho ya siku ya mtoto wa afrika
ambazo kimkoa zimeadhimishwa katika kijij cha Kikatiti wilayani
Arumeru.

Ameseema kuwa katika kuhakikisha haki za watoto zinalindwa na
kupatikana tayari wlaya 84 zimeshaunda mabaraza ya watoto ikiwemo jiji
la Arusha, kwa ajili ya kulinda na kusimamia haki mbalimbali za watoto
.

Magesa Mulongo, amesema katika kuhakikisha haki hizo zinapatikana
tayari serikali imeingiza kwenye mitaala ya Vyuo vya maendeleo ya
jamii sanjari na kuwepo kwa sera  ya maendeleo ya mtoto nchini
masuala ya haki za watoto ili kuepuka utumikishwaji  wa watoto kwenye
kazi zenye madhjara katika mazingira hatarishi .

Aidha amesema kuwa katika juhudi hizo za kuhakikisha haki za watoto
zinalindwa zaidi ya watoto 720 mkoani Arusha, waishio kwenye mazingira
 magumu wameondolewa kwa ushirikiano na mashirika yasiyokuwa ya
kiserikali likiwemo shirika la Mkombozi ambalo limeweza  kuondoa
watoto 29 na kuwaunganisha katika mfumo rasmi wa elimu ikiwemo Ufundi

Amesema kuwa watoto 6 wameunganishwa na familia zao ,watoto 8
wameunganikatika familia zao na kupatiwa elimu ya kujitegemea, watoto
20 wamepelekwa kwenye kituo kingine cha Mkombozi kilichopo Moshi
mkoani Kilimanjaro na kuunganishwa kwenye mradi wa bustani 40 sanjari
na kuhudumiwa i  elimu wakiwa katika familia zao

Ameongeza kuwa katika mlolongo huo familia 60 kutoka kata za Unga
limited na Ngarenaro, zimewezeshwa kiuchumi ili ziweze kumudu kulea na
kutunza watoto wao

Amesema kuwa pia Shirika lingine la Action for Children, limeweza
kutoa  elimu  katika shule 12 mbalimbali ambayo inahusu utetezi na
ushawishi ,haki za watoto na kutoa msaada wa kisheria kwa wananchi
21,  katika halmashauri 3 za Jiji la Arusha, Halmashauri ya Meru, na
Arusha DC.

Amesema kuwa mkoa huo unaendelea na vita dhidi ya dawa za kulevya na
utumikishwaji wa watoto kwenye mazingira hatarishi  kupitia Idara za
maendeleo ya jamii katika halmashauri mbalimbali kwa kushirikiana na
mashirika yasiyokuwa ya kiserikali ambapo elimu ya madhara ya dawa za
kulevya imekuwa ikitolewa .

No comments:

Post a Comment