Wednesday, July 24, 2013

MSISUBIRI MSIMU WA NANE NANE UFIKE NDIO MUANZE KUWEKA VIPANDO MNAWANYIMA WAKULIMA NA WAFUGAJI HAKI ZAO-MAGESA MULONGO



Halmashauri za kanda ya kaskazini zimetakiwa kujiwekea utaratibu wa
kuweka vipando na mashamba darasa katika viwanja vya maonesho ya
wakulima na wafugaji(TASO)kila wakati na kuachana na tabia ya
kustawisha pamoja na kuweka vipando hivyo mwezi mmoja kabla ya
maonesho hali ambayo wakati mwingine inasababisha maana halisi ya
kilimo kwanza kufa.

Wito huo umetolewa Jana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Bw Magesa Mulongo
wakati akiongea na wadau wa kilimo wa chama cha wakulima na wafugaji
kanda ya kaskazini (TASO) kwenye maandalizi ya maonesho hayo
yanayotarajiwa kuanza hivi karibuni

Alisema Halmashauri za kanda ya kaskazini zinakabiliwa na changamoto
hiyo hivyo jitiada mbalimbali bado zinahitajika ili kuweza kuboresha
kilimo kwanza hususani kwenye suala la vipando ambavyo baadhi yake
hufanywa kama mazoea tu

Alizitaja changamoto kubwa ambazo zinafanya halmashauri kupanda
vipando hivyo kwa mazoea ni pamoja na kutojua maana halisi ya chama
hicho pamoja na maonesho kwani asilimia kubw ya watu wanafikiri kuwa
viwanja hivyo vinaweza kutumika kuanzia Agust Moja hadi kumi kwwa kila
mwaka

Mbali na hayo alisema kuwa katika kipindi hiki cha kuelekea katika
maonesho ya wakulima na wafugaji pia kila Halmashauri zinatakiwa
kujituma kwa bidii na kuachana na tabia ya kulalamika kuwa hawajapata
zawadi

Alifafanua kuwa,tabia ya kutojituma ipasavyo na kutotumia mbinu bora
za kilimo kwanza kwa watazamaji ndio inayochangia kwa kiwango kikubwa
Halamashauri zilizokosa zawadi kuona kuwa walionewa na majaji

Akifunga kikao hicho Mwenyekiti wa TASO bw Athur Kitonga alisema kuwa
lengo la chama hicho ni kuendeleza sekta ya Kilimo na wafugaji kwa
kila mwaka lakini Halmashaauri bado hazipeleki wafugaji na wakulima
kujifunza katika mabanda yao mpaka ifike msimu wa maonesho ya Nane
Nane.

MWISHO

No comments:

Post a Comment