Wednesday, July 24, 2013

UHAMIAJI YATARAJIA KUKUSANYA BILIONI 85



Na mwandishi wetu Arusha

Idara ya Uhamiaji hapa nchini inatrajia kukusanya kiasi cha zaidi ya
Bilioni 85 kwa kipindi cha mwaka 2013/2014 ambapo makusanyo hayo
yanatokana na mapato mbalimbali ya idara hiyo ambayo ipo chini ya
Wizara ya mambo ya ndani.

Hayo yameelezwa na Kamishana wa utawala na fedha katika idara hiyo
ambaye ni Bw Piniel Mgonja wakati akiongea  katika mkutano wa
tathimini wa utendaji kazi kwa wahasibu wa idara wa uhamiaji
unaondelea Jijini hapa

Piniel alisema kuwa kiasi hicho cha fedha kinaweza kupatikana na
kuvuka malengo kutokana na ukusanyaji wa Madhuhuli kuboreshwa zaidi
tofauti na miaka ya nyuma hali ambayo mpaka sasa itasaidia sana
kuongezeka kwa mapato ya idara hiyo.


Mbali na hayo alisema kuwa  hata kwa sasa vipo  baadhi ya vyanzo
vingine ambavyo  navyo vimechangia sana kuongeza mapato katika idara
hiyo ambapo vyanzo hivyo ni pamoja  vyanzo vya vibali vya kuishi
Nchini, huduma za Pasipoti, Hati za kusafiria,huduma ya uraia ,Viza
kwa wageni wanaoishi hapa Nchini

Kutokana na hali hiyo alisema kuwa bado idara ya uhamiaji hapa nchini
inakabiliwa na  changamoto kubwa ambayo ni ukosefu wa huduma za
kibenki katika baadhi ya vituo vya uhamiaji hapa nchini hali ambayo
wakati mwingine inasababisha upotevu na umanifu wa kifedha kwa
wafanyakazi pamoja na wadau wa uhamiaji

Alisema kuwa hali hiyo  si nzuri sana kwani nayo inachangia sana
kupunguza hata mapato ya Serikali kwani baadhi ya mapato huwa
yanapungua au kupotea kabisa kutokana na ukosefu wa huduma za kibenki.

Awali Akifungua mkutano huo Katibu Mkuu wa wizara ya mambo ya ndani
Nchi, bw Mbarak Abdulwakil alisema kuwa wahasibu katika wizara hiyo
wanatakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia sheria,Kanuni , na taratibu
zilizopo kwani usimamizi wa fedha unataka usimamizi wa hali ya juu
sana kwani fedha zinaushawishi mwingi sana

Alisistiza huduma ya malipo ya fedha inatakiwa kufanyika kwa njia ya
benki na kwa wakati na kwamba katika ukusanyaji wa maduhuli au katika
matumizi ya fedha na rasilimali nyingine benki ndio mahala sahihi pa
kuweka fedha hizo ili kuondo kasoro zinazoweza kujitokeza.

MWISHO

No comments:

Post a Comment