Wednesday, July 24, 2013

MWANDRI AWATAKA WAKRISTO KUSOMA VITABU VYA MUNGU KULIKO VENYE SIMULIZI ZISIZOJENGA JAMII

Na Bety Alex, Arusha



Waziri Agrey Mwandri amewataka wakristo kuachana na tabia ya kukwepa kujisomea vitabu mbalimbali ambavyo vinaongeza maarifa ya kiroho na kimwili kwani kwa njia ya vitabu hata maarifa juu ya ufalme wa Mungu nayo yanaongezeka sana

Mwandri aliyasema hayo wiki iliyopita katika kanisa la Winner Chapel Intrenational Arusha lililopo maeneo ya Kaloleni Mjini hapa wakati akizindua rasmi Kitabu kilichoandaliwa na Muinjilisti Paul Dickson kijulikanacho kama Ufalmwe wa Mungu hutekwa na wenye nguvu.

Alisema,kwa sasa wapo baadhi ya wakristo ambao wanapenda kujisomea vitabu ambavuyo havina maslahi na Mungu na badala yake vitabu hivyo vinahamsisha dhambi jambo ambalo kwa sasa wanatakiwa kulikataa

Alifafanua kuwa kama kila mkristo atahakikisha kuwa hapotezi muda wake mwingi kwenye vitabu hivyo a,mbavyo havijengi basi ni wazi kuwa hta dhambi ndani ya mkoa wa Arusha lakini Tanzania kwa ujmla nazo zitapungua kwa kiwango

Alibainisha kuwa kwa kusoma vitabu ambavyo vina madharai ya mwenendo wa Kimungu kunasaidia sana kuhimiza hata nguvu za Mungu kushuka na kuongoza katika mambo mbalimbali.

“jamani jiwekeeni utaratibu wa kuhakikisha kuwa mnasoma vitabu venye madhari ya Kimungu msinione hapa napambana kweli kule Bungeni lakini niwaambieni kuwa muda wangu mimi natumia hivi hivi vitabu vya mungu kujisomea na kuhakikisha kuwa naktafuta hata suluhu kule Bungeni hivyo basi igeni mfano huu “aliongeza Mwandri

Katika hatua nyingine Mwandishi wa kitabu hicho ambaye ni Muinjilisti Paul Dickson alisema kuwa lengo na maudhui ya kitabu hicho kijulikanacho kama Ufalme wa Mungu hutekwa na wenye nguvu, kina malengo ya kuhakikisha kuwa kinawakomboa baadhi ya watu katika ufalme wa Mungu

Muinjlisti huyo alidai kuwa kwa sasa wapo baadhi ya watu ambao wanatamani sana kuwa na falme wa Mungu lakini bado hawajaju hata siri za kuweza kuuteka ufalme huo hali ambayo wakati mwingine inasababisha waone kama ni wakosaji

“hiki kitabu kina siri nyingi sana za uponyaji na jinsi ya kuuteka ufalme wa Mungu hivyo basi natamani kuona kuwa watuw a sasa hususani mkoa wa Arusha na Tanzania wanaweza kuinuka  na kutoka katika hali Fulani hata za umaskini kwa kuwa ufalme wa Mungu kuuteka ni bure kabisa’aliongeza muinjilisti huyo

Alimalizia kwa kusema kuwa pamoja na kuwa vitabu vya Mungu vinaweza hata kuokoa lakini bado ipo changamoto kubwa sana kwa waaandishi wa vitabu kwa kuwa baadhi yao huandika zaidi vitabu ambavyo vinahusu mapenzi na kusahau vitabu vya kuwakomboa watu jambo ambalo si jema kwa maendeleo ya watu

MWISHO

No comments:

Post a Comment