Wednesday, July 24, 2013

NGORONGORO YATOA MICHE LAKI TATU KWA AJILI YA SHULE ZA SEKONDARI NA MSINGI



Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro (NCAA)imetoa miche ya miti laki tatu
kwa shule za Sekondari na Msingi ambazo zinapakana na Mamlaka hiyo
huku lengo halisi likiwa ni kuwafundisha wanafunzi umuhimu wa misitu
pamoja na kuhifadhi mazingira

Akiongea na waandishi wa habari mwisho wa wiki Afisa Misitu wa mamlaka
hiyo ambaye Ni Bw Naaman Naaman alisema kuwa huo ni mpango mojawapo wa
mamalaka hiyo wa kuhakikisha kuwa wanafunzi wanakuwa na elimu ya
misitu ili wawe mabalozi wazuri wa mazingira

Bw Naaman alisema kuwa mradi huo wa kutoa miche ya miti ambayo ni ya
matunda, mbao, na vivuli ulianza rasmi mwaka 2009 na mpaka sasa baadhi
ya shule za sekondari na msingi zimeshanufaika huku shule nyingine
zikianza rasmi kuzalisha miche yao

Alifafanua kuwa toka kuanza kwa mradi huo ambao mpaka sasa umegharimu
kiasi chazaidi ya Milioni mbili umeweza kuwa na faida kubwa sana
tofauti na hapo awali ambapo mradi huo haukuwepo kwenye mpango wa
mamlaka hiyo

Akitaja faida hizo alisema kuwa ni pamoja na wanafunzi kuanza
kiujifunza aina mbalimbali ya miti toka wakiwa shuleni huku hali hiyo
ikiweza kuwafanya wao waweze kudyahifadhi mazingira na kuona kuwa kuna
umuhimu wa kuhifadhi mazingira

Faida nyingine aliyoitaja ni pamoja na kuanza kujijengea tabia ya kuwa
na misitu ya kifamilia ili kuweza kukabiliana na tatizo la mabadiliko
tabia Nchi ambayo limeathiri sana eneo hilo la Ngorongoro.

Wakati huo huo alisema kuwa mpaka sasa mradi huo unakabiliwa na
changamoto kubwa ya uharibifu wa misitu hasa  kwa upande wa wafugaji
kwani bado mifugo yao inaharibu misitu ambayo imeoteshwa na mamlaka
hiyo.

Kutokana na Changamoto hiyo alisema kuwa ni vema kama viongozi wa
Kijiji wakajiwekea utaratibu wa kuelezea jamii umuhimu wa mradi huo
lakini pia umuhimu wa kuhifadhi mazingira ili kuepusha eneo hilo na
ukame .

MWISHO

No comments:

Post a Comment