Tuesday, February 12, 2013

TANZANIA YAINGIA KWENYE MAAJABU SABA YA AFRIKA



TANZANIA YAINGIA KWENYE MAAJABU SABA YA AFRIKA

Na Queen Lema,Arusha

TANZANIA kupitia shirika la Hifadhi za Taifa limefanikiwa kuingia katika maajabu saba katika bara la Afrika hali ambayo itafanya Sekta ya utalii hapa nchini iweze kukua na kuimarika sana tofauti na hapo awali.

Akitangaza Vivutio hivyo vitatiu mjini hapa mapema jana Dr Philiph Imler ambaye ni mwanzilishi na raisi wa maajabu saba barani Afrika alisema kuwa Tanzania kwa wakati huu umefanikiwa kupata vivutio vitatu

Alitaja vivutio hivyo kuwa ni Pamoja na Mlima Kilimanjaro,hifadhi ya Serengeti pamoja na bonde la Ngorongoro ambapo vivutio hivyo viliweza kupigiwa kura nyingi sana na hivyo kuvipa ushindi wa hali ya juu kwa pia ndani ya vivutio hivyo kuna maajabu ya aina mbalimbali ambayo hayapatikani popote barani Afrika na duniani kwa ujumla

“leo nina furai kutangaza kuwa Tanzania imeingia ndani ya maajabu saba na hivyo basi hii ni kama changamoto ya kuhakikisha kuwa bado mnaendelea kufanya viendelee kukua na kuinarika zaidi ili hata wakati mwingine muwe na vivutio vingi zaidi’aliongeza Dkt Imler.

Katika hatua Nyingine Waziri mkuu wa Tanzania,Mizengo Kayanza Pinda alisema kuwa bado Nchi za Afrika zinahitaji zaidi kuwekeza zaidi katika masuala ya Utalii ikiwa ni pamoja na kuongeza zaidi jitiada za utalii kwani bado kuna changamoto kubwa sana katika masuala ya utalii.

Pinda aliongeza kuwa endapo kama Nchi hizo zitaweza kufanya hivyo basi Nchi hizo zitakuwa na Vivutio venye maajabu mengi sana duniani hali ambayo nayo itachangia sana kuweza kuimarisha utalii wa ndani na hata wa nje ya nchi husika.

Aliongeza kuwa ndani ya Nchi  ya Tanzania kwa sasa wamejiwekea juhudi za makusudi kuanzia ngazi ya kitaifa ambapo kupitia ngazi mbalimbali wataweza kuharakisha maendeleo ya utalii hususani utalii ili maajabu mbalimbali ya Tanzania yaweze kufahamika duniani.

Awali mkurugenzi wa shirika la hifadhi za Taifa hapa nchini(TANAPA)Alan Kijazi alisema kuwa wanatarajia mapato kuongezeka hasa katika mlima Kilimanjaro,bonde  la Ngorongoro, na hifadhi za Serengeti kwa kuwa vivutio hivyo vimetangazwa rasmi kama vivutio venye maajabu ya kutosha

Kijazi alisema kuwa pamoja na kutangazwa kwa vivutio hivyo lakini bado TANAPA limejiwekea mikakati mbalimbali ya kuhakikisha kuwa wanaendeleza shuguli za utalii hapa nchini ingawaje bado kuna changamoto kubwa sana kwenye masuala ya utalii wa ndani

MWISHO

No comments:

Post a Comment