Tuesday, February 12, 2013

TFDA YATEKETEZA BIDHAA ZA MILION SABA HUKU BAADHI YAKE ZIKIWA NI BIDHAA AMBAZO ZINAWAFANYA WANAWAKE WAONEKANE WANENE KUMBE NI UGONJWA

TFDA ARUSHA YATEKEZA BIDHAA ZA MILIONI SABA

Na Queen Lema,Arusha


MAMLAKA ya Chakula na Dawa nchini TFDA, jana imeteketeza tani moja na robo ya Shehena kubwa ya bidhaa mbalimbali zenye thamani ya shilingi milioni 7 ambazo zimekwisha muda wake wa matumizi na zingine hazijasajiliwa na pia hazionyeshi lini muda wake wa matumizi utakwisha.

Akizungumza katika zoezi hilo la kuteketeza biddhaa hizo kwenye Jalala kuu , lililopo eneo la Muriet, halmashauri ya Jiji la Arusha, Meneja wa kanda ya Kaskazini, wa Mamlaka ya Chakula na Dawa, TFDA, ,Damas Matiko, amesema bidhaa hizo zimekamatwa katika msako uliofanyika ndani ya wiki moja katoka maduka ya Vyakula na Super market.jijini Arusha.

Amezitaja bidhaa hizo zilizoteketezwa kuwa ni  Mafuta ya vyakula, Juice, Soda aina ya Pepsi zilizoko kwenye makopo, Majani ya Chai, Dawa za miswaki za Kichina, Sukari, Maji ya Chupa, Unga wa maziwa wa uji wa watoto uliopo kwenye makopo, Vinywaji vikali, (Pombe)

Matiko, amesema kuwa bidhaa hizo hazikidhi viwango vuinavyotakiwa ,hazijasajiliwa na Shirika la Viwango nchini TBS, na zingine zimeandikwa lugha isiyofahamika ,zingine zimeghushiwa tarehe ya mwisho ya kutumika, hivyo zina madhara makubwa kwa watumiaji na pia hazimhakikishii Usalama mlaji.

Amesema zoezi hilo la kukamata bidhaa hizo bandia limefanyika kuanzia Februari 4 hadi February 8 mwaka huu ,ambapo Mamlaka hiyo imelazimika kuendesha msako huo kwenye maduka baada ya kubaini kuwepo kwa bidhaa zisizokuwa na viwango na hivyo kuathiri afya za walaji.


Matiko alitoa wito kwa  wananchi wanaonunua bidhaa zao kwenye maduka makubwa ya kuuza vyakula,{Super market}, kusoma maelezo ya bidhaa wanazonunua ili waelewe muda wa matumizi badala ya kununua kwa haraka na kwenda kutumia wakati mwingine wanaweza kununua bidhaa ambazo muda wake umeshakwisha na zikawa ni madhara kwao.

"wananchi wawapo na mashaka na bidhaa hizo zilizoko kwenye maduka zikiwemo ambazo lugha na maelezo yake hayaeleweki watoe taarifa kwa Mamlaka hiyo ya chakula na dawa TFDA, au Idara ya afya halmashauri ya jiji la Arusha,lengo ni kulinda afyas za walaji" alisisitiza Matiko.


Ameyataja baadhi ya madhara hayo kuwa ni pamoja na kupata magonjwa kama vile Saratan, kuharisha ,maumivu ya tumbo ,kupata mzio unaotokana na kula vyakula vya aina Fulani, wengine hunenepa na kuwa na miili mikubwa mfano kwa wanawake.

Kwa upande wake kaimu afisa afya mkuu wa jiji la Arusha, Alan Sumari, mewataka wafanyabiashara kuingiza nchini bidhaa zenye viwango ili kuepuka hasara ya bidhaa hizo kuteketezwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA.

No comments:

Post a Comment