Tuesday, February 12, 2013

ASKOFU ASHANGAZWA NA MANABII WANAOENDESHA MAISHA YAO KWA KIFAHARI ILIHALI WAUMINI WAO NI MASKINI


ASKOFU ASHANGAZWA NA MANABII WANAOENDESHA MAISHA YAO KWA KIFAHARI ILIHALI WAUMINI WAO NI MASKINI 

Na Bety Alex,ARUSHA

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida askofu wa kanisa la uzima na ufufuo jijini Arusha Stanley Kilima amewataka baadhi ya manabii wa mkoa wa Arusha ambao wanasindikizwa na kulindwa na mapolisi wakiwa barabarani(ESCORT)wakristo wawaogope sana kwa kuwa inadhirisha wazi kuwa wapo kimaslahi zaidi


Kilima aliyasema hayo Jumapili iliyopita wakati akiongea na waumini wa kanisa la uzima na ufufuo lilipo Maua Ungalmtd Jijini hapa ambapo alidai kuwa wapo wakristo ambao wanachekwa na shetani bila kujua kuwa shetani anawacheka

Alisema kuwa kwa sasa wakristo ambao wanakwepa neno la mungu ndio wanaodanganywa kwa kuwa watu wanaojiita ni Manabii wanatumia vibaya hilo jina na kisha wanajisafisha hata kwa majeshi mbalimbali kwa kuomba Escort bila kujua kuwa wanafanya vibaya sana kwa kuwa kama Mungu amewaita basi wasingeitaji Ufahari ambao hauna maana


Pia alisema kuwa kwa sasa wakristo wanapaswa kuwajua na kuwatambua wanaojiiita manabii kwa kuomba hekima kutoka kwa Mungu na kisha kuwachunguza kwa kuwa asilimia kubwa ya wanaojiita wao ni manabii wapo kifedha zaidi ambapo kwa sasa wengi sana wanashindania mambo ya kifahari yakiwemo magari ya kisasa

Aliongeza kuwa hali hiyo ya wakristo kufumba macho na kisha kuwatambua watu hao kama manabii kumbe ni wapenda fedha ndio inayozaa zaidi fedha chafu za nchi pamoja na mateso yasiyoisha ndani ya makanisa kwa kuwa shetani anawacheka badala ya kuwaogopa watu hao kama wana wa mungu


Alimalizia kwa kutoa hata wito kwa viongozi wa makanisa kuhakikisha kuwa kamwe tamaa ya vitu vya misaada haiwangilii kwa kuwa napo kwa sasa wapo baadhi ya watumishi wa Mungu ambao wanakwenda nje ya nchi na kuomba misaada ambayo wakati mwingine si kwa ajili ya utukufu wa Mungu bali ni kwa ajili ya maitaji yao binafsi


MWISHO

No comments:

Post a Comment