Wednesday, February 20, 2013

WATUMIENI MAAFISA VIJANA MUEPUKANE NA KERO ZA VIJANA MITAANI- DKT FENELA



WATUMIENI MAAFISA VIJANA MUEPUKANE NA KERO ZA VIJANA MITAANI- DKT FENELA

Na Queen Lema, Arusha

WAZIRI  wa habari,michezo na Utamaduni,Dkt Fenela Mkangara amezitaka Halmashauri zote ndani ya mkoa wa Arusha kuhakikisha kuwa zinajiwekea utaratibu wa kuwa na maafisa Vijana kwa kuwa kama wataweza kufanya hivyo basi watachangia kwa kiwango kikubwa sana kuweza kujadili kwa pamoja changamoto mbalimbali ambazo zinawakabili vijana

Zipo Halamshauri ambazo zinakabiliwa na masuala ya changamoto za Vijana lakini hakuna afisa yoyote ambaye  ana uwezo wa kutatua kero za vijana hivyo asilimia kubwa ya vijana wanabaki wakiwa  wanalalamika ovyo juu ya Serikali

Waziri huyo aliyasema hayo Jana Jijini hapa wakati akiongea na viongozi mbalimbali wa Jiji la Arusha akiwemo Mkuu wa Wilaya kuhusiana na maendeleo ya Vijana pamoja na changamoto,utatuzi wake kwa kipindi miaka iliyopita.

Dkt Fenala alisema kuwa endapo kama Hallkmashauri zote za Jiji la Arusha zitaweza kuwatumia vema hao maafisa Vijana basi zitachangia sana maendeleo ya Vijana kwa kuwa asilimia kubwa ya vijana wa sasa wanabaki wakiwa wanalamikia Serikali  kwa kushindwa kuwajua na kuwatambua jambo ambalo si la kweli

Alisema kuwa kupitia Maafisa Vijana hao ambao wataweza kutatua changamoto ikiwa ni pamoja na kuweka mikakati mbalimbali ya vijana lakini kwa kuwa  kwa sasa hakuna maafisa hao basi Halmashauri zinasema kuwa zinawasaidia vijana huku mitaani vijana bado wakiwa wanakabiliwa na changamoto nyingi sana.

“Wizara yangu imeweka mikakati ya kuondoa matatizo ya vijana lakini halmashauri pekee haziwezi hii kazi ni nzito jamani ni lazima mtekeleze ahadi Raisi ya kuwa na maafisa Vijana ambao wataweza kutukusanyia hawa vijana na kisha hata kama tunakitu cha kuwapa tuweze kuwapata kwa ukaribu sana na pia hii itasaidia sana vijana hawa waache kulalamika ovyo:”aliongeza Dkt Fenela

Awali Mkuu wa Wilaya ya Arusha, John Mongela alisema kuwa tatizo kubwa la vijana hasa wa mkoa wa Arusha wanachokitaka kikubwa sana ni Pesa na wala sio mawazo mazuri ya upataji  wa pesa na mitaaji imara hivyo bado asilimia kubwa sana ya Vijana wanabaki wakiwa wanalalamikia Serikali

Mongela alisema kuwa hali hiyo inasababisha vijana kuona kuwa Serikali haiwathamini,lakini bado Jiji la Arusha limeweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha kuwa inawapa fursa vijana wa mkoa wa Arusha sanjari na kuwaboreshea mazingira mazuri na imara ya kufanyia biashara zao pamoja na shuguli za kila siku.

MWISHO

No comments:

Post a Comment