Wednesday, February 20, 2013

WATENDAJI WA SACCOS WASIOKUWA NA ELIMU YA MAHESABU CHANZO CHA SACCOS KUFA


Na Queen Lema,Arusha

WATENDAJI WA SACCOS WASIOKUWA NA ELIMU YA MAHESABU CHANZO CHA SACCOS KUFA


IMEELEZWA kuwa kutokana na baadhi ya watendaji pamoja na viongozi wa vyama vya kuweka na kukopa(SACCOS) kukosa eliumu ya mahesabu kumesababisha sana baadhi ya vyama hivyo kushindwa kufikia malengo yake mbalimbali ambayo yamekwa huku pia hali hiyo ikisababisha migogoro

Hayo yameelezwa na Afisa ushirika jiji la Arusha Bw Huruma Kibwendwa wakati akiongea na wanachama wa Saccos ya Balimi ya jijini hapa mapema jana mara baada ya Saccos hiyo kufikia malengo yake mbalimbali

Huruma alisema kuwa kwa sasa ndani ya mkoa wa Arusha tatizo kubwa sana ni ukosefu wa elimu ya mahesabu kwa kuwa viongozi wengi wanaochaguliwa hawana elimu hiyo hivyo kusababisha madhara makubwa sana ndani ya vyama hivyo vya kuweka na kukopa

Alitaja madhara hayo kuwa ni  pamoja na migogoro ya mara kwa mara ambayo wakati mwingine husababisha hata kufa kwa vyama hivyo, huku madhara mengine ni pamoja na kusababisha utoaji wa mikopo ambayo haikidhi vigezo hali ambayo nayo inachangia sana hasara kubwa sana  kwenye mitaji ya vyama hivyo

“haya madhara ni makubwa sana na kwa hali hiyo basi napenda kusema kuwa hawa viongozi wa vyama hivi wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanatafuta elimu hii ili kuweza kunusuru vyama vya kuweka na kukopa ndani ya Jiji la Arusha lakini kama watakuwa wanaendesha vyama vyao kwa mazoea kutasababisha kukithiri kwa udanganyifu wa mahesabu ndani ya vyama hivyo” aliongeza Huruma

Akiongelea maendeleo ya Saccos hiyo ya Balimi Mweka hazina wake,Bw Gerald Kazungu alisema kuwa mpaka sasa wamefanikiwa kuwa na mtaji wa kiasi cha Milioni 73 ambapo kwa kipindi cha mwaka huu 2013 wameweza kugawa Gawio la kiasi cha zaidi ya  Milioni nane kwa wanachama wake mara baada ya kutengeneza faida ambayo imetokana na wanachama wake

Huruma alisema kuwa malengo halisi ya Saccos hiyo ni kuhakikisha kuwa wanaendelea kukopesha zaidi wanachama walio wengi zaidi ambapo kama watakuwa na wanachama wengi zaidi basi wataweza kuchangia kwa kiwango kikubwa sana kuokoa wananchi wa Jiji la Arusha dhidi ya Umaskini ambao unatokana na ukosefu wa Mitaji.

Awali Mwenyekiti wa Saccos Hiyo Bw Richard Mugyabuso alisema kuwa pamoja na kuwa wamefanikiwa kupata faida ya zaidi ya Milioni kwa kipindi cha Miaka miwili lakini bado wakopaji walio wengi wanakabiliwa na changamoto ya mautumizi mabaya ya mikopo hali ambayo inafanya wanakopa washindwe kurudisha fedha hizo huku vyama navyo vikiwa vinategemea marejesho kwa ajili ya kujiendeleza

Mugyabuso alisema kuwa wapo baadhi ya wakopaji katika baadhi ya vyama vya kuweka na kukopa wanakopa kwa malengo kama vile kufanya sherehe,kufikiria zaidi maisha ya kifahari,starehe huku hali hiyo ikisababisha kushindwa kulipa hasa wanapotakiwa kulipa,huku hali hiyo ikisababisha shuguli mbalimbali za vyama kukwama kutokana na Mtaji kupungua badala ya kuongezeka.

MWISHO

No comments:

Post a Comment