Saturday, January 4, 2014

KIJANA MMOJA AFUKIWA NA KIFUSI,ASKARI WATATU WAJERULIWA KWENYE MAPAMBANO DHIDI YAO NA RAIA KWENYE MKESHA WA MWAKA MPYA




Na Gladness Mushi, Arusha


KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida kijana mmoja aliyetambulika kwa jina
la Joseph Solomon Mkazi wa Terrat Kwa Muorombo jijini Arusha amefariki
dunia mara baada ya kuangukiwa na kifusi cha moramu katika machimbo ya
Terrat

Akiongea na waandishi wa habari mapema leo kamanda wa polisi mkoa wa
Arusha Liberatus sabas alisema kuwa tukio hilo lilitokea leo (Jana}
majira ya saa tatu na nusu za asubuhi huko Terrat

Alidai kuwa marehemu huyo alifikwa na mauti wakati akiwa anajaribu
kukata kifusi kwa kutumia jembe la kulima ambapo pia wakati anakata
kifusi hicho Lori la kubebea mchanga lilikuja kwa nyuma na kasha
kuangusha kifusi kwa haraka

Kamanda Sabasi alifafanua kuwa wakati Lori hilo linaegeshwa ghafla
liliporomoa kifusi hicho ambacho klilimfukia kijana huyo aliyekuwa
anachimba kwa kutimia jembe na kisha kufariki dunia papo hapo



Aliendelea kwa kusema kuwa mara baada ya dereva huyo wa lori kuona
kuwa kifusi kimeanguka ndani ya machimbo hayo aliamua kugeuza gari na
kisha kukimbia huku akiwa ametelekeza mwili wa kijana huyo



“alipoona kuwa ame[egesha gari vibaya na kusababisha mauti alikimbia
lakini wasamaria wema waliweza kuokoa mwili huo ingtawaje mpaka sasa
tunamtafuta dereva wa lori hilo kwani hata namba ya gari nayo bado
hatujaweza kuijua ila jitiada za haraka zinafanyika’aliongeza Kamanda
Sabasi



Pia alidai kuwa wamiliki wa machimbo ya kuchimba Moramu ndani ya mkoa
wa Arusha wanatakiwa kuwa makini sana lakini pia hata wachimbaji ,
madereva nao wanatakiwa kuchukua tahadhari juu ya kazi hiyo kwani
wakati mwingine uzembe unachangia sana vifo visivyo na hatia.



Wakati huo huo Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha inawashikilia vijana
wanne wakazi wa Wilaya ya Meru kwa kosa la kusababishia askari polisi
majeraha pamoja na raia wema kwenye mkesha wa mwaka mpya

Sabasi alisema kuwa wanaoshililiwa ni pamoja na Selemani
Khamisi,Patrick Richard,Jabu Yasini,pamoja nha Khamisi Juma wote
wakazi wa Meru ambapo siku ya December 31 mwaka jana katika eneo la
Ngarasero Usariver,vijana hao waliweza kuongoza kundi kubwa la
wananchi katika kupingana na Serikali dhdii ya kusherkea kwa amani na
utulivu mwaka mpya

Alidai kuwa askari waliokuwa doria katika maeneo hayo walilazimika
kupambana na vijana hao lakini hawakuskia kwa kuwa tayari walikuwa
wameshawasha moto na kuhamasiaha zaidi vurugu jambo ambalo ni kinyume
cha sheria



“wakati polisi wanapambana kutuliza vurugu kundi kubwa la watu
wakiongozwa na vijana hawa walianza kuwarushia mawe polisi na kufanya
fujo kali ambazo pia zilisababisha askari weru kujeruliwa vibaya
sana”alifafanua hivyo kamanda Sabasi



Aidha aliwataja askari walijeruliwa vibaya kuwa ni pamoja na Mkaguzi
msaidizi wa polisi ambaye ni Athumani,Askari namba G 3475
D/CRamadhani,pamoja na askari mgambo ambaye ana namba 97658 Jacob
wakati kwa upande wa Raia ni Aneth Baltazar,Mary Kwayu ambapo pia
Majerui  wote  wamelazwa katika hospitali ya West Meru kwa ajili ya
matibabu



                MWISHO

No comments:

Post a Comment