Thursday, January 30, 2014

UKOSEFU WA VYOO WASABABISHA WANAFUNZI ZAIDI YA 300 KUJISAIDIA VICHAKANI

UKOSEFU WA VYOO WASABABISHA WANAFUNZI ZAIDI YA 300 KUJISAIDIA VICHAKANI

ZAIDI ya wanafunzi 300 kutoka katika shule ya msingi Engatani iliopo Kata ya MakibaWilayani Meru Mkoani Arusha wapo hatarini kupata magonjwa ya mlipuko kutokana na kuwa shule hiyo haina vyoo na hivyo wanafunzi wa shule hiyo wanalazimika kujisaidia kwenye vichaka.

Aidha tatizo hilo la ukosefu wa vyoo katika shule hiyo umedumu kwa miaka miwili sasa mara baada ya mvua kubwa kufukia matundu ya vyoo katika shule hiyo.

Akiongea na “majira “shuleni hapo mapema jana Mkuu wa shule hiyo Adamu Kapaya alisema kuwa shule hiyo haina vyoo kabisa na hivyo wanafunzi wanapojisikia kujisaidia wanalazmika kwenda kwenye vichaka au kwenye mazingira ambayo yamejificha kwaajili ya kuweza kujisaidia

Alidai tatizo hilo limeanza mwaka 2012 ambapo mvua kubwa ya masika ilionyesha iliweza kuziba matundu ya vyoo na hivyo kusababisha kutitia kwa vyoo hivyo na mpaka sasa hakuna huduma ya vyoo hali ambayo imesababisha madhara makubwa sana kutokea katika shule hiyo.

“baada ya kuona kuwa mvua zimesababisha shule yetu kukosa vyoo niliandika barua kwa mkurugenzi ambapo naye alihaidi kushugulikia tatizo hili na kwa uongozi wa serikali ya kijiji nlakini mpaka sasa hali ndio kama hii hakuna choo wanafunzi wanakimbilia zaidi kwenye Vichaka”alisema Adamu

Pia aliongeza kutokana na hali hiyo imesababisha hata mazingira ya shule kuwa machafu sana pamoja na kuwepo kwa hewa chafu kutokana na vinyesi ambavyo vimezagaa kwenye mazingira ya shule hiyo na pembezoni mwa shule hiyo hivyo jitiada za haraka sana zinatakiwa kufanyika

Awali diwani Viti maalumu wa Kata hiyo ya Makiba.Bi Joycye Odoko alisema kuwa ukosefu wa choo kwenye shule hiyo umesababishwa na baadhi ya watendaji kukwepa kuombea bajeti shule hiyo kwa lkuwa ipo mpakani mwa wilaya ya Meru hali ambayo inasababisha wanafunzi waishi mazingira magumu sana

Bi Joyce amesema kuwa asilimia kubwa ya wananchi katika eneo hilo ni wafugaaji lakini hawana uwezo kitu ambacho kama wangekuwa na uwezo basi wangeweza kuwasaidia wanafunzi hao

“wananchi wa hapa hawana uwezo ingawaje kwa sasa wameshaweka utartibu hata wa kukusanya mawe , na mchanga ili kuuanza rasmi zoezi hilo japokuwa bado hawataaweza kujenga mpaka kumalizika kwa matundu ya vyoo sassa tunaomba kuwepo  naushirikiano madhubuti baina yetu sisi viongozi ili tuweze kuwasaidia wanafunzi hawa kwani wapo kwwenye hatari kubwa sana ya kuweza kupata magonjwa ya mlipuko hasa kipindupindu”aliongeza Jocye

Akiongelea sakata hilo kwenye baraza la madiwani wa halmahauri ya Meru Mwenyekiti wa baraza hilo ambaye Goodson Majola alisema kuwa kwa sasa bajeti ya Halmashauri hiyo imelenga kutatua sehemu mbalimbali zenye kero na hivyo pindi watakapopata fedha kutoka Serikali kuu basi wataweza kutatua changamoto mbalimbali

Mwisho

No comments:

Post a Comment