Monday, May 6, 2013

WANANCHI WALALAMIKA KIJIJI KUKOSA MAPATO KWA MIAKA MITANO MWENYEKITI ADAI KUWA ANAONEWA VWIVU NA WANANCHI

Na Queen Lema,ARISHA

WANANCHI WALALAMIKA KIJIJI KUKOSA MAPATO KWA MIAKA MITANO MWENYEKITI ADAI KUWA ANAONEWA VWIVU NA WANANCHI

Wanananchi wa Kijiji cha Ilikirioti Kata ya Moivo Wilaya ya Arusha wamemuomba Mkuu wa wilaya  Munasa Nyirembe  kuingilia kati kwenye uongozi wa kijiji hicho kwa kuwa uongozi huo unadai kuwa toka mwaka 2009 mpaka sasa hawajafanikiwa kupata mapato ya aiana yoyote ile.

Wananchi hao waliyasema hayo jana katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na Mwenyekiti wa kijiji hicho Bw Prosper Steven ili kujadili ili kuweza kusoma matumizi ya kijiji hicho.

Wananchi hao walidai kuwa ni aibu kubwa sana kuona kuwa kila siku ndani ya kijiji hicho wanapata asilimia kumi ya mashamba yanaouzwa lakini pia hata michango lakini uongozi wa kijiji unadai kuwa hauna fedha yoyote ile toka mwaka 2009

Aidha walidai kuwa kwa kukosa kijiji kukosa mapato huku wananchi wakiwa wanashangishwa fedha mbalimbali kunaashiria harufu ya Rushwa lakini pia harufu ya ukandamizaji wa hali ya juu jambo amblo kama Mkuu wa Wilaya hataingilia kati basi huenda liksababisha matatizo makubwa sana

“tunamuomba Mkuu wa wilaya hii pamoja na mkurugenzi waje hapa Kijijini waje wajione hali ilivyo hatuna hata barabara lakini tunaambiwa kuwa eti mapato hayapo na sisi tunachanga kila siku na mtu akija kununua shamba ni lazima atoe asilimia kumi sasa kama hali itaendelea hivi je mwisho wake utakuwa ni upi kama sio kudodondosha damu?walihoji wananchi hao.

Lakini mbali na hayo walidai kuwa ndani ya Kijiji hicho hakuna ulinzi pamoja na usalama wa mali zao kutokana na kituo cha polisi kuwa mbali na makazi yao hali ambayo inatakiwa kutatuliwa kwa haraka sana

Walifafanua kuwa umbali ambaop upo ndani ya Kijiji hicho unasababisha baadhi ya waahalifu kuiba huku wakiwa wanajiamini kabisa kwa kile ambacho wanakifanya kwa kuwa mpaka polisi watoke mjini na kufika katika eneo hilo watakuwa wameshamaliza kuiba wananchokitaka jambo ambalo wakati mwingine linasababisha Umaskini wa kutisha.

Awali Mwenyekiti wa Kijiji ghicho Prosper Steven alidai kuwa kinachoendelea kijijini hapo wivu kwa kuwa amejenga nyumba kubwa nay a kifahari lakini kijiji hakina mapato ya iana yoyote ile hivyo wananchi hawapswi kukosa imani nae

“nawashangaa sana hawa wananchi wanaosema kuwa kijiji hakina mapato kwa miaka mimi najua kuwa hii ni roho ya wivu kwa kuwa nimejenga nyumba ya kifahari kuliko wao na ndio maana wanaongoza kwa kudai kuwa ningatuke kwa kuwa ninachakachua mapato ya Kijiji”alisema Prosper.

Mwisho

No comments:

Post a Comment