Tuesday, February 28, 2012

WASHAURIWA KUTUMIA NISHATI YA BIOGESI

WAFUGAJI wanaofuga mifugo mbali mbali hapa nchini wameshauriwa kutumia
nishati bora ya bioges badala ya kutumia nishati za kuni ambapo tafiti
zinaonyesha kuwa nishati za kuni zimechangia kwa asilimia kubwa uharibifu
wa mazingira ambao umesababisha mabadiliko ya tabia nchi.

Hayo yalisemwa na mkuu wa wilaya ya Mwanga bw Athuman Mdoe alipokuwa katika
ufunguzi wa teknolojia wa mtambo maalum wa bioges kwa ajili ya maeneo yenye
hali ya ukame uliozindiliwa rasmi mwanga mkoani kilimanjaro.

Aidha alisema kuwa nishati ya bioges ni nishati ya gharama nafuu
ukilinganisha na nishati nyinginezo kama vile umeme,gesiza viwandani ,mkaa
na kuni ambapo pia nishati hii inapunguza kwa kiwango kikubwa cha uharibifu
wa mazingira.

Aliongeza kuwa faida za nishati ya bioges haziishii hapo bali husaidia
katika uhifadhi wa mazingira ,hutoa mbolea bora kwa ajili ya kilimo
,hupunguza mudawa akina mama unaotumika katika utafutaji kuni na pia
hupunguza maradhi yotokanayo na matumizi ya kuni na mkaa.

Alieleza kuwa teknoloja hiyo ambayo kwa kitaalamu inajulikana kama Solid
State Biodgester(SSB)ambayo ndio iliyotumia katika ujenzi wa mtambo huo
utaweza kuwanufaisha wakazi waishio kwenye maeneo ya hali ya ukame ikiwemo
wilaya hiyo hivyo kuwataka wafugaji walioudhuria katika ufunguzi huo
kuitumia fursa hiyo pekee kuweza kjinufaisha na teknolojia hiyo..

Nae mratibu wa programu ya uenezi wa mitambo ya bioges kwa ngazi ya
kaya(TDBP)bw .Lehada Cyprian alisema kuwa programu hiyo imefanikiwa
kuhamasisha ujenzi wa mitambo katika maeneo yenye urahisi wa upatikanaji wa
maji .

Bw Cyprian aliongeza kuwa katika kipindi cha miaka mitatu kwa kushirikiana
na wadau wengine imefanikiwa kujenga mitambo 2568 katika maeneo tofauti
tofauti hapa nchini.

Alieleza kuwa pia programu imepanga kujenga mitambo 50 kwa mwaka huu w
fedha kwa kutumia teknoloja ya SSB katika maeneo tofauti hapa nchini ikiwa
ni pamoja na mwanga,arusha na hanang lengo halisi likiwa ni kuwafikia
wafugaji wa ng'ombe asili ili nao waweze kunufaika na teknolojia hiyo ya
bioges.

mwishoo

CHANZO CHA HABARI NA QUEEN LEMA

0758907891

ARUSHA 

No comments:

Post a Comment