Thursday, April 26, 2012

WAJASIMALI 70 WA KKKT WAPATIWA MAFUNZO


Wajasiriamali wanawake zaidi ya 70 kutoka kanda ya kaskazini na kati ya dayosisi  za kanisa la kilutheri wamepatiwa mafunzo ya ujasiriamali ya siku nne yaliyolenga kuwajengea uwezo ufahamu, na elimu ya kujikomboa na umaskini.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo mkurugenzi wa mpango  wa kazi za wanawake na watoto kkkt makao makuu arusha Bi Rachel Ramadhani alisema kuwa licha ya changamoto zinazowakabili ikiwemo ya fedha lakini mafunzo hayo yatawatoa katika utegemezi na kuweza kujiendesha na kuandaa semina nyingine kama hizo. kwani wanawake wengi wameathiriwa na mfumo dume.

alisema bi ramadhani kuwa ukosefu wa elimu ya darasani na elimu ya mazingira kutokana na mfumo dume kumewaacha kinamama wakiwa hawana mtegemezi na kuishi kwenye lindi la umaskini na hili kanisa imeliona ndiyo maana likaanza kupigana na umaskini wa kinamama na vijana ilikuondokana na taifa tegemezi.

alisema bi Rachel kuwa dayosisi zaidi ya 7 zinashiriki  zikwemo dayosisi ya kaskazini,dayosisi ya Pare,dayosisi ya kaskazini kati,dayosisi za Mbulu,Meru,kaskazini mashariki,na kati na kuwataka wakinamama kufahamu kuwa kitu ulichonacho kiwe halali kitawafanya kuondokana na umaskini wa kujitakia hata mchicha ni biashara halali isiyohitaji fedha za kukopa kwenye asasi za kifedha unapatikana kwa njia ya kujituma na kujiamini aliongeza bi ramadhani

Kuwa wanachangamoto nyingi kubwa ni fedha lakini elimu hii itasaidia kuondokana na kuomba omba au kutafuta wafadhili wa kusaidia semina kama hizo na kuwataka angependa kuwaambia biashara si lelemama biashara ni nia na wazo lakujenga na ni kitu chochote halalikinachoweza kuuzika tufanye sasakwani tunamazingira yetu yanakila kitu cha kuweza kutusaidia.

Nae mjasiriamali aliyepata mafunzo hayo bi Elizabeth Ngoi alisema kuwa anamshukuru mama ramadhani kwani hapo mwanzo hakuwa anajua kuwa kunapato la kwanza na patozalishi linaloweza kumuendeleza mtu na kuondokana na lindi la umaskini na kuwa akifika nyumbani atakuwa balozi mzuri wa kuwafundisha wengine na kuwa atakuwa na uwezo wa kubuni biashara nyingi zaidi kutakana na mafunzo aliyopata.
MWISHO.

chanzo cha habari na Queen Lema,

0758907891

Arusha

No comments:

Post a Comment