Wednesday, March 5, 2014

KANISA LAAZISHA UTARATIBU WA KUOMBEA UCHAGUZI WA MWAKA 2015

Raisi Jakaya Kikwete



KANISA la T A G Patmo nkoanekoli lilopo Wilayani meru mkoani arusha limeweka mikakat mbalimbali ya kuombea uchaguzi wa taifa la  Tanzania ambao unatarajiwa kufanyika mapema mwakani 2015

Aidha uamuzi huo wa kufanya maombi ambayo yanafanyika kila mwanzo wa mwezi ili kuweza kuraishsisha uchaguzi huo wa wabunge pamoja na madiwani wa kata zote

 Akiongea kanisani hapo kwenye ibada ya siku ya jumapili ambayo iliongozwa na neno la mungu la kuwahimiza wakristo kutojiinua mchungaji kiongozi wa kanisa hilo Japheti Nanyaro alisema kuwa utararibu huo utaweza kuwasaidia sana taifa

nanyaro alisema kuwa,maombi hayo ambayo yanafanywa na kanisa hilo yanalenga sehemu mbalimbali ambazo ni muhimu sana kwenye maisha ya kiroho ya mkristo wa sasa


alitaja kuwa wakati wa uchaguzi na kampeni mbalimbali za nchi panakuwa na roho lukuki za kishetani ambazo zinaibuka ambapo pia wakati mwingine roho hizo husababisha hata baadhi ya damu ambazo hazina hatia kuweza kuibuka na kufanya kazi

aliongeza kuwa mbali na roho hizo kuweza kuibuka lakini pia wakati mwingine kuna kuwa na maroho ya kuwanyima haki wanyonge hasa wale ambao wameitwa na Mungu kutokana na watu ambao wapo kuweza kutumia veo vyao kuiba haki


pia aliongeza kuwa nayo makanisa mengine yanatakiwa kuhakikisha kuwa yanaweka utaratibu wa kuweza kuomba juu ya matukio ya kitafia ndanui ya nchi kwani wakati mwingine roho za kujiinua nazo zinachangia sana hata wananchi kukosa haki zao za msingi

mbali na hayo pia aliwataka nao wakristo kuhakikisha kuwa wananchana na tabia ya kujiinua kutokana na vyeo vyao vya kanisa lakini hata vile vya kidunia kwani hali hiyo imesababisha walio wengi sana hasa wale wenye tabia hizo kuangamia bila kujijua

"nawasihi sana hakikisheni kuwa kamwe hamujiinui bali mnainuliwa na bwana mwenyewe ili msiweze kushuka ila mkjiinua na kutumia njia za mkato kwenye maisha au uongozi wa maisha yenu ya kila siku ni lazima mtapata shida na mtadhalilika sana subirini neema ya bwana iweze kukufika kwenye kila jambo"aliongeza Nanyaro

MWISHO

No comments:

Post a Comment