Wednesday, March 5, 2014

DC ARUSHA AWATAKA WANANCHI KUTOPENDELEA KUWAPELEKA WANFUNZI NJE YA NCHI

MKUU WA WILAYA YA ARUSHA AKIAPA KUWATUMIKIA WANANCHI WA ARUSHA,PICHA NA MAKTABA YETU


NA ,MWANDISHI WETU, ARUSHA
Watanzania wametakiwa kuondokana na dhana ya kuwwapeleka watoto wao
nje ya nchi kwa ajili ya kuweza kupata elimu jambo ambalo hata kwa
shule za Tanzania wana uwezo huo wa kuboresha zaidi elimu

Asilimia kubwa ya watanzania wanadhani kuwa kumpleka mtoto au
mwanafunzi nje ya  nchi ndio kumjenga jambo ambalo halina hata ukweli
ndani yake

hayo yameelezw ana mkuu wa Wilaya ya Arusha John Mongela kwa niaba ya
mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo wakati akiongea na umoja wa
wamiliki wa shule na vyuo binafsi kwa mkoa wa Arusha(TAMONGSCO) mapema
jana.

Mongela alisema kuwa dhana hiyo imeshapitwana wakati na hivyo wananchi
wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanaboresha shule zao na hivyo kuweza
kutoa fursa

Aisha alisema kuwa fedha ambazo wanazitumia nje ya nchi zingeweza
kusaidia baadhi ya shule katika michango na hivyo basi wanatakiwa kuwa
wazalendo

Amedai kuwa mzalendo wa nchi ni pamoja na kuhakikisha kuwa kwanza
unatoa vipaumbele kwa vitu ambavyo vipo ndani ya nchi lakini pia
unaweza kuvipenda

"pendeni sana shule za hapa tanzania kwani zipo baadhi ambazo kwa
kweli zinatoa elimu kwa wakati sana na zinafaa kuliko zile za nje ya
nchi, nakama mkiziboresha basi nanyi mtapata hata wanafunzi wenyewe
kutoka nje ya nchi na kwa hali hiyo mtakuwa mmenda sanjari na soko la
nchi za EAC'aliongeza Mongela

naye Mwenyekiti wa umoja huo Ester Lema alisema kuwa pamoja na kuwa
wana uwezo wa kuwasiaida wananchi kupunguza tatizo la kwenda nje ya
nchi lakini bado wanakabiliwa na changamoto nyingi

Ester alitaja changamoto ambazo wanakabiliana nazo kuwa ni pamoja na
kodi kubwa ambayo wanatozwa, lakini hata riba ambayo inatolewa na
asasi mbalimbali za kifedha.

No comments:

Post a Comment