Monday, December 19, 2011

OLE WENU NINYI WACHUNGAJI NA MAASKOFU MNAOPINGA HUDUMA CHANGA



 Wito umetolewa kwa baadhi ya wachungaji wakubwa na wenye majina makubwa hapa nchini kuhakikisha kuwa wanaachana na tabia ya kudharau huduma ambazo ni ndogo na changa kwa kuwa mungu haangalii zaidi ukubwa wa jengo bali anaangaliwa wingi wa watu wanaomcha katika maisha yake

Hayo yamesemwa na askofu wa kanisa la international Chastmatic church,(ZION TEMPLE)Bw fitiaely urio katika ibada ya kuwaweka wakfu  sanjari na kuwaweka kazini rasmi wachungaji  nane wa kanisa hilo lilopo katika maeneo ya Ungalmtd jijini hapa.

Askofu Fitiaely  alisema kuwa ndani ya jamii ya sasa bado kuna baadhi ya wachungaji ambao mara nyingi wamekuwa wakidharau na kukataa huduma mbalimbali za wenzao kwa kuwa ni changa

Alibhainisha kuwa hali hiyo si njema na ni chukizo kubbwa sana mbele za mungu kwa kuwa mungu hana vigezo kama walivyonavyo baadhi ya wanadamu hapa duniani.

“ukiangalia utakuta maskini mchungaji kaamua kuanzisha kanisa lake na huduma yake lakini kwa kuwa mchungaji wa jirani yeye anawa umini wengi zaidi anawaacha waumini wake kuwalea kiroho na kimwili alafu eti anaangalia zaidi ile huduma changa sasa kwa maana hiyo kanisa la leo linakwenda wapi jamani’aliwahoji waumini

Katika hatua nyingine mtumishi huyo alienda mbali zaidi na kusema kuwa nao wachungaji ambao wanakuwa na waumuini wachache miaka yote nao ni wakuuliza maswali kwa kuwa miongoni mwao kutakuwa na kasoro

Alisema kuwa wanapswa kukumbuka biblia ilivyosema na kuahidi kuwa tunatakiwa kuwaleta watu wengi kwa yesu kwa maana kama mchungaji hana waumini miaka yote ni wazi kuwa anakiuka sharti hilo.

‘pamoja na kuwa wachungaji wanawakataa wenye huduma changa lakini sisi kama sisi tunatakiwa kujiuliza ina maana hata kwa mara moja huyu mchungaji hashawishiki hata kumleta mtu kwa yesu au yupo kivingine ‘alisema mtumishi huyo

Pia alianisha kuwa nao wachungaji  na wakuu mbalimbali wa idara wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanaachana na tabia ya kuweka mbele zaidi maslahi katika huduma zao kwa kuwa hayo maslahi ndiyo chanzo mojawapo cha kukataliwa na jamii

Alisiisitiza kuwa kwa mtumishi ambaye ameitwa na mungu anapaswa kujua kuwa malipo yake yapo mbinguni na wala sio hapa duaniani ambapo kuna fedha na kwa njia ya kudai malipo kwa ajili ya ukombozi wa watu ndiyo kichocheo mojawapo cha kujiunganisha na falme nyinginezo

MWISHO 

CHANZO CHA HABARI NA QUEEN LEMA
O758907891

ARUSHA 

No comments:

Post a Comment