Friday, December 2, 2011

NYIE MNAOTOA MISAADA KAMWE MSIIKUMBUKE

Mchungaji Mama furaha Simtenda kutoka Tanga amewataka wakristo
mbalimbali hapa nchini kuhakikisha kuwa kamwe wanapotoa msaada
mbalimbali kamwe hawakumbuki misaada au sadaka hizo kwa kuwa kwa njia
ya kukumbuka ni wazi kuwa wanajionesha kwamba hawajatoa kwa moyo.

Mama furaha aliyasema hayo katika kanisa la Anglican st James wakati
alipokuwa akifundisha semina  kwa waumini na wakristo mbalimbali juu
ya umuimu wa kutoa kwa moyo

Alisema kuwa ustaarabu ambao upo kwenye makanisa ndio unaotakiwa
kuwepo kwenye utoaji wa misaada mbalimbali kwa kuwa mungu anapenda
mtoaji asikumbuke kamwe ambacho amekitoa

“unakuta mtu anampa mtu hata nguo alafu akisha muona amependeza bila
kujali anaanza kusema kuwa ni mimi ndiye niliyempa sasa makanisani
mlishaona mtu akitoa zaka anaongea inakuwaje misaada inakuimbukwa ,huo
sio utoaji”aliongeza Mama furaha

Pia alisema kuwa kila mkristo anatakiwa kuhakikkisha kuwa analipa
garama mbalimbali ambazo zilitolewa na bwana yesu mslabani kwa kuwa
yesu alilipa garama za kila kizazi bila kujali itikadi za dini wala
rangi

Aliongeza kuwa kupitia garama ambazo zimelipwa na bwana yesu kila
mwenye mwili anatakiwa kuwa mna moyo wa kujitoa sana kwa kuwa kwa sasa
bado wapo baadhi ya watu ambao hawajitoi hata katika machangizo
mbalimbali hali ambayo si sahihi mbele za mungu.

Alisema kuwa ili uweze kutoa michango mbalimbali ndani ya makanisa
unatakiwa kuhakikisha kuwa unakuwa na tabia ya imani kwa kuwa suala
zima la utoaji lina sanjari na imani ‘ambayo ndiyo msingi imara.

“kama hauna imani ni wazi kuwa kila utakalo kuwa unalifanya ni bure ni
sawa tu  na umesogeza kitu mbele yako lakini kama una imani basi
utaweza kupokea kile lunachokitaka kwa maana hiyo nawasihi muwe na
imani kwa kuwa imanik ndio msingi mkuu”aliongeza Mama furaha


Hataivyo aliwataka wakristo kuhalkikisha kuwa wanatoa bila kuangalia
mifukoni mwao kilichobakia kwa kuwa biblia imeonesha wazi  mungu akiwa
upande wa mwanadamu hakuna ambaye atakuwa juu zaidi kwa maana hiyo
kila kitu kinawezekana kwa mungu.

CHANZO CHA HABARI NA QUEEN LEMA
ARUSHA
0758907891

No comments:

Post a Comment