Tuesday, August 27, 2013

WAKULIMA WATAKIWA KUTUMIA KILIMO CHA UMWAGILIAJI KULIKO KILIMO CHA MAJIRA YA MWAKA



Na Queen Lema, Arusha


Wakulima wa Kanda ya kaskazini wameshauriwa kuhakikisha kuwa wanaanzisha utaratibu maalumu wa kutegemea zaidi kilimo cha umwagiliaji kuliko kutegemea kilimo cha majira ya mwaka kwani aina hiyo ya kilimo kwa sasa inaonekana kupitwa na wakati.

Kauli hiyo imetolewa mjini hapa na Bw Elias Mshiu ambaye ni Mwenyekiti wa chama cha wakulima Tanzania(TFA)wakati akiongea na gazeti hili kuhusu hali ya kilimo kwa kanda ya kaskazini mapema jana

Aidha Bw Mshiu alisema kuwa inashangaza sana kuona kuwa asilimia kubwa ya wakulima hasa wa kanda hii ya kaskazini bado wakiwa wanategenea kilimo cha mvua za Vuli lakini pia mvua za masika hali ambayo ndiyo chanzo cha ukame

Alibainisha kuwa endapo kama wakulima watatumia zaidi aina ya kilimo cha umwagiliaji ni wazi kuwa hata mazao nayo yatawweza kuongezeka tofauti na sasa ambapo wapo baadhi ya wakulima ambao wanafanya kama kubahatisha tu

Alisema, Kilimo cha umwagiliaji kina tija kubwa sana kwa wakulima wa kanda hii hivyo basi ni vema hata kama nayo wizara ikahakikisha kuwa inatoa elimu zaidi  na fursa mbalimbali ili wakulima wazoeee kuliko kutumia kilimo cha majira ya mwaka ambacho wakati mwingine kinakataa kabisa.

Pia alisema katika Chama hicho cha TFAkwa sasa wameweza kugundua changamoto hiyo ya wakulima wengi kutegemea zaidi kilimo cha majira ya mwaka hivyo wamebuni mbinu na njia mbadala ambazo zitaweza kuifanya jamii iweze kuondokana nacho kwa malengo ya kuongeza zaidi chakula

Alitaja Mikakati hiyo kuwa ni pamoja na kuweza kuwakopesha lakini pia kuwawezesha wakulima vifaa mbalimbali kwa ajili ya umwagiliaji ili waweze kufikia malengo yao ambayo wamejiwekea.

“tulikaa na kisha kuona kuwa kuna umuhimu wa kuwasaidia hawa wakulima ili wawe na elimu hii ya umwagiliaji lakini waweze kukopa hata vifaa kwa ajili ya umwagiliaji katika mashamba yao na kwa kweli kama wote wataitiika hata kuja kuchukua elimu hii basi kilimo kwa kanda hii kitaimarika sana”aliongeza Bw Mshiu.

Alimalizia kwa kusema kuwa nao wakulima wanatakiwa kubadilika na wanatakiwa pia kuachana na kilimo cha mazoea ambacho mara kwa mara ndiocho kinachisababisha waonekane ni wakulima lakini faida hawana na badala yake wafuate sheria,kanuni, na taratibu mbalimbali za Kilimo.

MWISHO

No comments:

Post a Comment