Wednesday, March 5, 2014

MADIWANI 23 MERU WATISHIA KUJIUZULU NA KUKUSANYA KADI ZA CCM NA WANACHAMA WAKE.

MBUNGE WA JIMBO LA ARUMERU MASHARIKI JOSHUA NASSARI



MADIWANI 23 MERU WATISHIA KUJIUZULU NA KUKUSANYA KADI ZA CCM NA WANACHAMA WAKE.


KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida madiwani 23 kutokaa katika Halmashauri ya Meru mkoa wa Arusha wametishia kujiuzu wote katika nyadhifa zao lakini pia kukusanya kadi zote za chama cha mapinduzi sanjari na kuongoza maelfu ya wananchi kwenda kuchukua ardhi yao ambayo imetekwa kinyemela,endapo kama Halmashauri hiyo haitatoa tamko rasmi dhidi ya migogoro ya mashamba inayoendelea Wilayani Humo.

Aidha pia kadi ambazo zitakusanywa zitaweza kuwekwa chini ya uangalizi maalumu ikiwa ni pamoja na kutojihusisha na kazi yoyote ile ya chama cha mapinduzi ikiwa ni fundisho kwa serikali dhidi ya vigogo wake wa Wizara ya Ardhi ambao wanatumika katika migogoro ya ardhi katika Halmashauri Mbalimbali.

Madiwani hao waliyasema hayo ijumaa iliyopita katika baraza la madiwani lililofanyika katika Halmashauri hiyo ambapo agenda ya migogoro ya ardhi ilifanya baraza hilo kujikuta likiwa linatoa tamko na vitisho vikubwa kwa watumishi wa Halmashauri hiyo.

Akiongea kwa niaba ya madiwani wa Halmashauri hiyo bi Mwanaidi Kimu alisema kuwa wameschoshwa kila siku kujadili agenda za migogoro ya ardhi lakini hakuna utendaji wowte na badala yake wanabaki wakiwa na kumbukumbnu ya vikao katika vichwa vyao hali ambayo kwa sasa imefika mwisho

Akitolea mfano moja yashamba lenye migogoro katika Halmashauri hiyo,shamba la  Madira lililopo katika maeneo ya Seela Singisi ambalo  ni mali halisi ya Halmasahuri hiyo lakini kwa sasa kuna migogoro ambayo inasababishwa na baadhi ya viongozi jambo ambalo wamedai kuwa hawataweza kuvumilia bali wataingia katika vita kwa mara nyingine

“kwa mfano hili shamba la Seela Singisi ni mali ya wananchi wote wa Meru na hadi Raisi ameshaweka saini yake jamani litumike kwa ajili ya matumizi ya kata zote za Meru lakini vigogo wanasema ni mali yao alafu bado tumenyamaza tu haitawezekana tunaachia udiwani alafu htunaingia katika Vita kwa mara nyingine”aliongeza Kimu

Katika hatua nyingine akiongea kwa niaba ya madiwani wanaume ,Wilson Nyitti alisema kuwa hali hiyo imesababisha kila wanpopita walazimke kujikuta wakiwa wanazomewa ovyo na wananchi kwa kuwa wananchi wanafikiri kuwa wao wananufaika na migogoro hiyo ya ardhi

Nyitti alisema wamechoka na hali hiyo ya kudhomewa na kuabishwa mara kwa mara wakati hawausiki na kutokana na hilo sasa wamejipanga kushirikiana na wananchi kurudi kwanye vita kwa mara nyingine kwa ajili ya kuchukua ardhi yao lakini kupigana hata ikiwezekana kabisa.

“hili ni tamko rasmi tunatoa tunataka majibu ya migogoro hii rasmi kama hatupewi itakuwa ni vita baina ya Wameru na hawa wanaojichukulia ardhi kinyemelea, pia itakuwa ni huzuni kubwa kwa CCM  manake kwanza sisi wote hapa tunatokea CCM uzalendo umetushinda kabisa”aliongeza Nyiti

Naye Mwenyekiti wa Halmasahuri hiyo ya Meru, Goodson Majola alisema kuwa tamko hilo la kutaka kujiuzulu kwa madiwani 23 wote wa halmashauri hiyo lipo sawa kabisa kwa kuwa migogoro yote ya ardhi inasababishwa na Viongozi wasio waadilifu kuanzia ngazi ya Halmashauri hadi Wizara

Akiongelea suala la shamba hilo la Madira alisema kuwa Raisi Kikwete tayari ameshatoa ardhi hiyo yenye jumla ya Hekari 360 lakini bado hawajaweza kulitumia kutokana na vitisho ambavyo walikuwa wanavipata kutoka kwa vigogo

“mimi nasema kuwa tutajiuzulu wiki chache zinazokuja baada ya kujiridhisha juu ya maangaiko haya ya ardhi ambayo yamedumu toka karne hadi karne na ninasiistiza kuwa itakuwa ni kilio kwa CCM kwa kuwa wanchama wetu nao tutaweka chini ya ulinzi hadi tutakapowaambia hawatajishugulisha na shuguli yoyote ya chama”alisema Majola.

Majola alisema kuwa kujiuzulu kwao lakini pia kuondoka na wanachama wote wa CCM katika Wilaya hiyo ni uzalendo wao kwa wananchi na hivyo Hata CCM nao hawapaswi kuumia kwa hilo.

Hataivyo Halmashauri hiyo inaoongozwa na madiwani wote wa CCM lakini pia kwa upande wa wapinzani inaongozwa na Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki Joshua Nassari.

MWISHO

MSIAMBUKIZE VIRUSI KWA MAKUSUDI-RC MULONGO

MKUU WA MKOA WA ARUSHA, MAGESA MULONGO.



mkuu wa mkoa wa Arusha magesa mulongo amewataka baadhi ya wagonjwa
wanaoishi na virusi vya ukimwi kuhakikisha kuwa wanaishi kwa kufauta
masharti ya wataalamu wa afya lakini pia kuachana  na dhana ya
kuambukiza magonjwa hayo kwa makusudi hasa kwa wale ambao bado hawana
maambukizi

mulongo aliyasema hayo wakati akiongea kwenye uzinduzi wa chanjo kwa
kina mama wajawazito mpango ambao unatekelezwa chini ya Shirika la
Egpaf

Alidai kuwa kwa sasa wapo baadhi ya wagonjwa ambao wanatumia mwanya
huo kuwajerui wale ambao hawana ugonjwa jambo ambalo sio jema kwenye
jamii

alifafanua kuwa wagonjwa hao wanapaswa kuhakikisha kuwa wanafuta
taratibu za wataalamu wa afya lakini pia wahakikishe kuwa kamwe
hawaongezi idadi ya wagonjwa zaidi

"jamani ni lazima tufike mahali tuwe na tabia ya uzalendo lakini pia
tuhakikishe kuwa tunajiengua kwa kusababisha mtikisiko kwenye taifa
kwa ajili ya makusudi tuawalinde wale ambao hawana na wala makusudi
kamwe hayawezi kutusaidia sisi bali yanachangia sana
kutuangamiza"aliongeza Mulongo

Naye mganga mkuu wa mkoa wa arusha Frida Mokiti alisema kuwa pamoja na
jitiada mbalimbali ambazo zinaendelea kufanyika lakini bado kasi ya
maambukizi kwa mkoa wa Arusha ipo juu sana.

Mokiti alifafanua kuwa mkoa umeweza kuweka mikakati mbalimbali ya
kupambana na ugonjwa huo ingawaje nao wagonjwa nao wanatakiwa
kuepukana na kusambaza kwa makusudi bali wanatakiwa kuchukua tahadhari
tena kwa haraka sana.

CCM WAWAFARIJI WAGONJWA

MWENYEKITI WA CCM TAIFA, JAKAYA KIKWETE

CHAMA  cha Mapinduzi Wilaya ya Karatu mkoa wa Arusha kimefanikiwa kutoa msaada kwa wagonjwa zaidi ya 100  wa hospitali teule ya wilaya ya Karatu(DDH KARATU)huku lengo likiwa ni kuwafariji na kuanza kutangaza mkakati mpya ambao utawasaidia wagonjwa kila mara .
akiongea na waandishi wa habari wilayani humo mara baada ya kukabidhi misaada hiyo Mwenyekiti wa Wilaya hiyo Bw Mustapha Mbwambo alisema kuwa misaada hiyo imetolewa kama njia mojawapo ya kutimiza upendo
Mustapha alisema kuwa kwa sasa wameweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha kuwa inawasadia wagonjwa na hata wale ambao hawajiwezi kwa misaada mbalimbali ambayo itaweza kuwasaida na kuona kuwa bado serikali na uongozi wa wilaya unawakumbuka.
'ilani ya chama chetu inasema kuwa tuwapenda na tuwajengee mazingira ya kupona wagonjwa sasa sisi hapa Karatu tumeweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha kuwa kila mara tunatoa msaada lakini pia kuwafariji wagonjwa ambao hawana uwezo na zoezi hili halitakuwa kwenye maazimisho haya ya miaka 37 pekee"aliongeza Mustapha.

Katika hatua nyingine Katibu wa chama hicho ambaye ni Bi Elly Minja alisema kuwa kwa sasa Chama hicho kimeanza kutekeleza ilani ya Chama hicho lakini pia kuanzisha utaratibu maalumu wa kuweza kuwasaidia wananchi kwenye masuala ya msingi ambayo wakati mwingine yanachangia sana umaskini .
Alifafanua kuwa kwa mikakati ambayo inalenga kwenye masuala ya msingi yatachangia kwa kiwango kikubwa sana historia ya mji huo wa Karatu ambao kwa sasa bado unahitaji nguvu kubwa sana ya chama hicho.
"leo tumeweza kufanya mambo mbalimbali ya kichama lakini pia tumeweka malengo ya kuhamkikisha kuwa hata ilani ya chama inatekelezwa kwani kama ikifanikiwa basi itaweza kuwasaidia sana wananchi wa hapa kwetu na hivyo hata kwa mkoa wa arusha nako historia ikiwemo ya umaskini itabadilika sana"aliongeza Bi Minja.

Wakati huo huo akiongea na wananchi wa wilaya hiyo  kwenye viwanja vya Mazingira Bora Mgeni Rasmi kwenye maazimisho hayo, Daniel Awaki ambaye ni Mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa ya chama hicho kwenye Wilaya hiyo ya Karatu alisema kuwa toka kuanzishwa kwa chama hicho miaka 37 iliyopitwa kuna mabadiliko makubwa sana na mabadiliko hayo hayapaswi kupuuzwa wala kuzomewa na mtu yeyoete.
"tujiulieze kwa sasa ukitoka Arusha mpaka hapa unatumia muda gani na hapo awali ilikuwaje, na wala sio kwenye sekta hiyo pekee bali hata kwenye sekta nyingine za msingi sasa mafanikio kama haya hatupaswi kuyapuuza hata kidogo"aliongeza Awaki.
mwisho

JAMBO SQURD WAFANYA KWELI ARUSHA

WASANII WA KUNDI LA JAMBO SQUARD


WASANII maarufu ambao wamefanikiwa kufanya vizuri katika soko la muziki wa kizazai kipya maarufu kama Jambo  Squard mwishoni mwa wiki walipagawisha vilivyo mashabiki wao katika uwanja wa sheikh Amri Abeid  jijini Arusha.

Wasanii hao ambao walisindikizwa na kundi zima la Balance Diet lililopo jijini hapa walipiga shoo ya kukata na shoka wakati kituo cha redio 5 kilichopo jijini Arusha kufungua mwaka na mashabiki wao kutoka mikoa ya Arusha,Kilimanjaro na Manyara.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa kituo hicho Robert Francis meneja mbunifu wa kampuni ya Tan Communication Media Vicky  Mwokoyo alisema kuwa wameamua kufanya tamasha hilo ili kuwawezesha mashabiki wa kituo hicho na mashabiki wa Jambo Squard kupata buradani katika viwanja hivyo ambayo kwa muda mrefu hawakuipata.

Hata hivyo alisema kuwa tamasha hilo ni kama kufungua mwaka na kurudisha burudani na mapenzi yao kwa mashabiki wao kama ambavyo mashabiki wamekuwa wasikilizaji bora   kituo hicho ambacho kwa sasa kimekuwa na kutanuka karibu mikoa yote ya Tanzania.

Mbali na hayo pia meneja huyo aliongeza kuwa  kwa mwaka huu 2014 watakuwa na matamasha mengi lengo likiwa ni kutoa burudani na kuwa na desturi ya kukutana na mashabiki wao ikiwa ni moja ya kufahamu vitu gani wanaihitaji zaidi lakini pia kuwawezesha mashabiki wote kupata burudani zaidi hata wale wa hali ya chini kwa kuweka viingilio ambavyo havitawanyima mashabiki wengine kukosa burudani

“tutakuwa tunafanya mara kwa mara matamasha kwa mwaka huu tumejipanga lengo ni kutoa burudani zaidi nakuwawezesha wote kushiriki hata wale wa mashabiki wetu wasiojiweza nao ni sehemu yetu na ni lazima wapate burudani”alisema Vicky

Mbali na wasanii hao wa Jambo Squard kupiga ambayo ama kwa  hakika mashabiki waliridhika wasanii wengine wengi walipata fursa ya kuonesha vipaji vyao kama Spark,na Kundi la balance Diet linaloundwa na vijana watatu.
Mwisho,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

MWEKEZAJI MERU AVAMIWA



ZAIDI ya wananchi 200 kutoka katika Kijiji cha Karangai Kata ya Mbuguni Wilyani Meru Mkoani Arusha wamevamia shamba la Mwekezaji wa kampuni ya Tanzania Plantation na kuharibu mazao, sanjari na kuchoma nyumba moto nyumba  kwa madai kuwa wanataka kumiliki ardhi yao.

Akiongelea suala hilo Meneja wa kampuni hiyo ya Tanzania Plantatio Andrew Slaa alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa nne za usiku ambapo wananchi walivamia makazi ya mwekezaji wao na kisha kuharibu mali ambazo thamani yake bado haijajulikana mpaka sasa.

Slaa alisema kuwa hataivyo wananchi hao walikuwa na silaha za jadi waliweza kutekeleza ahadi walizopewa na viongozi mbalimbali wa Kata hiyo akiwepo Diwani wa kata hiyo kuwa wanatakiwa kupewa ardhi yao.

"hivi karibuni wanasiasa walidai kuwa muwekezaji huyu ambaye anafanya kilimo katika mashamba haya hayupo kwa mujibu wa sheria kwaiyo hii ardhi ni mali yao na kutokana na kauli hiyo wananchi sasa juzi waliamua kuingilia kati na kisha kuharibu mali za huyu mwekezaji huku wakidai kuwa ardhi yote ambayo ni zaidi ya hekari 2000 ni mali yao"aliongeza Slaa

Alisema kuwa wao kama watendaji wakuu wa kampuni hiyo tayari wanamipango lakini hata mikakati ya kuhakikisha kuwa wanakuwa na ujirani mwema na wananchi lakini wananchi nao wanakiuka sheria za uwekezaji na kisha kusababisha hasara kubwa

Aidha kwa upande wa Mwekezaji mkuu wa kampuni hiyo Tanzania Plantation,Bw Pkadeep Lodhia alisema kuwa wananchi hao wamesababisha uharibifu mkubwa sana wa kuchoma nyumba , lakini pia kuharibu mbogamboga ambazo zilikuwa zimerpandwa kwa makusudi ndani ya eneo hilo

Alisema kuwa mara nyingi sana amekuwa akitishiwa maisha na wananchi hao ambao wakati mwingine humwambia kuwa amepora ardhi yao na hivyo hata kufikia uamuzi wa kutaka kumchoma yeye na gari lake jambo ambalo ni shinikizo kubwa la wanasiasa.

"mimi naogopa hata wakati mwingine kufanya kazi zangu ndani ya shamba hili kwani kuna saa ambazo nanusurika kufa kwa ajili ya wananchi wananitishia maisha lakini sio mimi tu hadi wafanyakazi wangu lakini mpaka sasa nimeshapata hasara kubwa sana ya Mamilionhi ya fedha kutokana na uharibifu huu wa mali"aliongeza Lodhia

Pia alisema kuwa anaiomba mamlaka husika kuhakikisha kuwa wanafanya uchunguzi wa kikamilifu zaidi yake na shamba lake lakini pia hata kuweza kuwachukulia sheria kali wanaosababisha uharibifu huo wa mara kwa mara kwani yeye ni mmiliki wa shamba hilo kuanzia mwaka 1995.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Munasa Nyirembe alisema kuwa Mwekezaji huyo yupo kwa mujibu wa sheria ya wawekezaji hapa nchini lakini wananchi nao wanapaswa kujua na kutambua kuwa wanachokifanya ni makosa tena makubwa na hivyo sheria itaanza kuchukua mkondo wake.

Naye Diwani wa kata hiyo ya Mbuguni,Thomas Mollel alisema kuwa kamwe hawezi kusiistiza uvamizi kwa mwekezaji huyo na kwa kusema hivyo anamuonea kwani sheria haiwezi kumruhusu kufanya hivyo.

DC ARUSHA AWATAKA WANANCHI KUTOPENDELEA KUWAPELEKA WANFUNZI NJE YA NCHI

MKUU WA WILAYA YA ARUSHA AKIAPA KUWATUMIKIA WANANCHI WA ARUSHA,PICHA NA MAKTABA YETU


NA ,MWANDISHI WETU, ARUSHA
Watanzania wametakiwa kuondokana na dhana ya kuwwapeleka watoto wao
nje ya nchi kwa ajili ya kuweza kupata elimu jambo ambalo hata kwa
shule za Tanzania wana uwezo huo wa kuboresha zaidi elimu

Asilimia kubwa ya watanzania wanadhani kuwa kumpleka mtoto au
mwanafunzi nje ya  nchi ndio kumjenga jambo ambalo halina hata ukweli
ndani yake

hayo yameelezw ana mkuu wa Wilaya ya Arusha John Mongela kwa niaba ya
mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo wakati akiongea na umoja wa
wamiliki wa shule na vyuo binafsi kwa mkoa wa Arusha(TAMONGSCO) mapema
jana.

Mongela alisema kuwa dhana hiyo imeshapitwana wakati na hivyo wananchi
wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanaboresha shule zao na hivyo kuweza
kutoa fursa

Aisha alisema kuwa fedha ambazo wanazitumia nje ya nchi zingeweza
kusaidia baadhi ya shule katika michango na hivyo basi wanatakiwa kuwa
wazalendo

Amedai kuwa mzalendo wa nchi ni pamoja na kuhakikisha kuwa kwanza
unatoa vipaumbele kwa vitu ambavyo vipo ndani ya nchi lakini pia
unaweza kuvipenda

"pendeni sana shule za hapa tanzania kwani zipo baadhi ambazo kwa
kweli zinatoa elimu kwa wakati sana na zinafaa kuliko zile za nje ya
nchi, nakama mkiziboresha basi nanyi mtapata hata wanafunzi wenyewe
kutoka nje ya nchi na kwa hali hiyo mtakuwa mmenda sanjari na soko la
nchi za EAC'aliongeza Mongela

naye Mwenyekiti wa umoja huo Ester Lema alisema kuwa pamoja na kuwa
wana uwezo wa kuwasiaida wananchi kupunguza tatizo la kwenda nje ya
nchi lakini bado wanakabiliwa na changamoto nyingi

Ester alitaja changamoto ambazo wanakabiliana nazo kuwa ni pamoja na
kodi kubwa ambayo wanatozwa, lakini hata riba ambayo inatolewa na
asasi mbalimbali za kifedha.

KANISA LAAZISHA UTARATIBU WA KUOMBEA UCHAGUZI WA MWAKA 2015

Raisi Jakaya Kikwete



KANISA la T A G Patmo nkoanekoli lilopo Wilayani meru mkoani arusha limeweka mikakat mbalimbali ya kuombea uchaguzi wa taifa la  Tanzania ambao unatarajiwa kufanyika mapema mwakani 2015

Aidha uamuzi huo wa kufanya maombi ambayo yanafanyika kila mwanzo wa mwezi ili kuweza kuraishsisha uchaguzi huo wa wabunge pamoja na madiwani wa kata zote

 Akiongea kanisani hapo kwenye ibada ya siku ya jumapili ambayo iliongozwa na neno la mungu la kuwahimiza wakristo kutojiinua mchungaji kiongozi wa kanisa hilo Japheti Nanyaro alisema kuwa utararibu huo utaweza kuwasaidia sana taifa

nanyaro alisema kuwa,maombi hayo ambayo yanafanywa na kanisa hilo yanalenga sehemu mbalimbali ambazo ni muhimu sana kwenye maisha ya kiroho ya mkristo wa sasa


alitaja kuwa wakati wa uchaguzi na kampeni mbalimbali za nchi panakuwa na roho lukuki za kishetani ambazo zinaibuka ambapo pia wakati mwingine roho hizo husababisha hata baadhi ya damu ambazo hazina hatia kuweza kuibuka na kufanya kazi

aliongeza kuwa mbali na roho hizo kuweza kuibuka lakini pia wakati mwingine kuna kuwa na maroho ya kuwanyima haki wanyonge hasa wale ambao wameitwa na Mungu kutokana na watu ambao wapo kuweza kutumia veo vyao kuiba haki


pia aliongeza kuwa nayo makanisa mengine yanatakiwa kuhakikisha kuwa yanaweka utaratibu wa kuweza kuomba juu ya matukio ya kitafia ndanui ya nchi kwani wakati mwingine roho za kujiinua nazo zinachangia sana hata wananchi kukosa haki zao za msingi

mbali na hayo pia aliwataka nao wakristo kuhakikisha kuwa wananchana na tabia ya kujiinua kutokana na vyeo vyao vya kanisa lakini hata vile vya kidunia kwani hali hiyo imesababisha walio wengi sana hasa wale wenye tabia hizo kuangamia bila kujijua

"nawasihi sana hakikisheni kuwa kamwe hamujiinui bali mnainuliwa na bwana mwenyewe ili msiweze kushuka ila mkjiinua na kutumia njia za mkato kwenye maisha au uongozi wa maisha yenu ya kila siku ni lazima mtapata shida na mtadhalilika sana subirini neema ya bwana iweze kukufika kwenye kila jambo"aliongeza Nanyaro

MWISHO

Wednesday, February 12, 2014

TRA ARUSHA YAWATAKA WANAOHAMASISHA MIGOMO YA MADUKA KUACHA MARA MOJA

 Na mwandishi wetu, Arusha
 
 
MAMLAKA ya mapato TRA hapa nchini imetangaza vita kubwa kwa wafanyabiashara wadogo na wakubwa ambao wanashinikiza mgomo wa kufunga biashara kwenye maduka mbalimbali hapa nchini kwa visingizio vya kutotambua matumizi ya mashine za kulipia kodi
Aidha hatua hiyo inakuja wakati wafanyabiashara katika mikoa mbalimbali hapa nchini kufunga maduka na kisha kushinikiza kwa wenzao wasitoe huduma kwa ajili ya kupinga matumizi ya mashine hizo
Akitangaza rasmi vita hiyo ambayo itafanyika katika mikoa yote hapa nchini kaimu  Kamishna mkuu wa mamlaka hiyo Rishedi Bade alisema kuwa serikali kamwe haitaweza kuwafumbia macho wadanganyifu wa biashara ya aina yoyote ile
Alisema kuwa kwa wafanyabiashara wa aina yoyote ile atakayekamatwa kuwa anashinikiza mgomo basi wataweza kuchukuliwa sheria mbalimbali ambazo zitawagarimu kwa kiwango kikubwa sana
Pia aliwataka wafanyabiashara nao kutoingia kwenye mgomo ambao hauwahusu kwani wanajitengenezea harasa zao wenyewe wakati wanaohitajika kutumia mashine hizo za kielekroniki wamebainishwa kwenye sheri
"TRA tunashangaa sana kuona kuwa wafanyabiashara wasiohusika wanafunga biashara wakati wanaohusika ni wengine na kwa hali hiyo tunatangaa vita sasa na wale ambao wanahamasisha mgomo"aliongeza Bade
Wakati huo huo pia alisema kuwa watakaokamatwa wakiwa wanahasisha mgomo huo hatua watakazochukuliwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani lakini pia hata kuweza kuwafutia leseni zao za biashara

Katika hatua nyingine alisema kuwa matumizi ya mashine hizo ni muhimu sana kwa maendeleo ya taifa la Tanzania kwani zinaweka na kuanisha wazi juu ya mapato halisi ya mfanyabiashara
"nawasihii sana hakikisheni kuwa mashine hizi zinatumika ipasavyo alafu hizi zitawasaidia kuepuka makisio hata ya mapato na matumizi ambayo wakati mwingine yakikisiwa huwa hayawi sahihi kwaiyo hakikisheni mnazikubali na wafanyabiashara msiingie kwenye migogoro isiyo ya lazima"alisema Bade
Hataivyo pamoja na tamko hilo wafanyabiashara wa mkoa wa Arusha bado nao jana waliweza kuingia kwenye mgomo wa kugomea matumizi sahihi ya mashine hizo ambapo maduka ambayo yalifungiliwa yaliweza kuletewa fujo kubwa sana

MWISHO

Thursday, January 30, 2014

UKOSEFU WA VYOO WASABABISHA WANAFUNZI ZAIDI YA 300 KUJISAIDIA VICHAKANI

UKOSEFU WA VYOO WASABABISHA WANAFUNZI ZAIDI YA 300 KUJISAIDIA VICHAKANI

ZAIDI ya wanafunzi 300 kutoka katika shule ya msingi Engatani iliopo Kata ya MakibaWilayani Meru Mkoani Arusha wapo hatarini kupata magonjwa ya mlipuko kutokana na kuwa shule hiyo haina vyoo na hivyo wanafunzi wa shule hiyo wanalazimika kujisaidia kwenye vichaka.

Aidha tatizo hilo la ukosefu wa vyoo katika shule hiyo umedumu kwa miaka miwili sasa mara baada ya mvua kubwa kufukia matundu ya vyoo katika shule hiyo.

Akiongea na “majira “shuleni hapo mapema jana Mkuu wa shule hiyo Adamu Kapaya alisema kuwa shule hiyo haina vyoo kabisa na hivyo wanafunzi wanapojisikia kujisaidia wanalazmika kwenda kwenye vichaka au kwenye mazingira ambayo yamejificha kwaajili ya kuweza kujisaidia

Alidai tatizo hilo limeanza mwaka 2012 ambapo mvua kubwa ya masika ilionyesha iliweza kuziba matundu ya vyoo na hivyo kusababisha kutitia kwa vyoo hivyo na mpaka sasa hakuna huduma ya vyoo hali ambayo imesababisha madhara makubwa sana kutokea katika shule hiyo.

“baada ya kuona kuwa mvua zimesababisha shule yetu kukosa vyoo niliandika barua kwa mkurugenzi ambapo naye alihaidi kushugulikia tatizo hili na kwa uongozi wa serikali ya kijiji nlakini mpaka sasa hali ndio kama hii hakuna choo wanafunzi wanakimbilia zaidi kwenye Vichaka”alisema Adamu

Pia aliongeza kutokana na hali hiyo imesababisha hata mazingira ya shule kuwa machafu sana pamoja na kuwepo kwa hewa chafu kutokana na vinyesi ambavyo vimezagaa kwenye mazingira ya shule hiyo na pembezoni mwa shule hiyo hivyo jitiada za haraka sana zinatakiwa kufanyika

Awali diwani Viti maalumu wa Kata hiyo ya Makiba.Bi Joycye Odoko alisema kuwa ukosefu wa choo kwenye shule hiyo umesababishwa na baadhi ya watendaji kukwepa kuombea bajeti shule hiyo kwa lkuwa ipo mpakani mwa wilaya ya Meru hali ambayo inasababisha wanafunzi waishi mazingira magumu sana

Bi Joyce amesema kuwa asilimia kubwa ya wananchi katika eneo hilo ni wafugaaji lakini hawana uwezo kitu ambacho kama wangekuwa na uwezo basi wangeweza kuwasaidia wanafunzi hao

“wananchi wa hapa hawana uwezo ingawaje kwa sasa wameshaweka utartibu hata wa kukusanya mawe , na mchanga ili kuuanza rasmi zoezi hilo japokuwa bado hawataaweza kujenga mpaka kumalizika kwa matundu ya vyoo sassa tunaomba kuwepo  naushirikiano madhubuti baina yetu sisi viongozi ili tuweze kuwasaidia wanafunzi hawa kwani wapo kwwenye hatari kubwa sana ya kuweza kupata magonjwa ya mlipuko hasa kipindupindu”aliongeza Jocye

Akiongelea sakata hilo kwenye baraza la madiwani wa halmahauri ya Meru Mwenyekiti wa baraza hilo ambaye Goodson Majola alisema kuwa kwa sasa bajeti ya Halmashauri hiyo imelenga kutatua sehemu mbalimbali zenye kero na hivyo pindi watakapopata fedha kutoka Serikali kuu basi wataweza kutatua changamoto mbalimbali

Mwisho

KATA ZA WILAYA YA KARATU ZATAKIWA KUANZISHA MIRADI ILI KUONGEZA UCHUMI KUANZIA NGAZI YA KAYA



Na Queen Lema, KARATU


CHAMA cha mapinduzi Wilaya ya Karatu mkoa wa Arusha kimeagiza uongozi
wa kata zote ndani ya Wilaya hiyo kuhakikisha kuwa inabuni miradi ya
maendeleo ambayo itawasaidia wananchi kuweza kujiongezea kipato lakini
pia kuweza kuondokana na umaskini katika kata zao

Hayo yameelezwa na Katibu wa chama hicho kwa wilaya ya Karatu, Bi Elly
Minja wakati akiongea kwenye harambee ya ujenzi wa jengo la Kitega
uchumi ambalo lipo wilayani humo ambapo pia harambee hiyo ilienda
sanjari na mazoezi mengine mengi ya kuazimisha kuzaliwa kwa CCM hapa
nchini

Bi Elly alisema kuwa kuna haja sasa ya kila kata kuhakikisha kuwa
inakuwa na miradi tena endelevu ambayo itaweza kuwasaidia wananchi
kuondokana na dhana ya umaskini ambayo ikwa sasa ni tishio kubwa sana
kwenye baadhi ya familia.

Alifafanua kuwa miradi hiyo ambayo inatakiwa kubuniwa na wananchi kwa
kushirikiana na viongozi wa kata mbali na kuweza kuwaokoa wananchi
kwenye suala zima la umaskini lakini pia itachangia sana kuongezeka
kwa uchumi wa wilaya hiyo ya Karatu.

Mbali na uanzishwaji wa miradi kwenye kata zote za Karatu pia alisema
kuwa kwa upande wa Jengo la Kitega uchumi lililopo Karatu nalo
litaweza kuwasiaida sana wananchi katika kuboresha uchumi wao lakini
pia litakuwa na faida sana

"uwepo wa jengo hilo la kitega uchumi hapa Karatu ni ishara kuwa sasa
uchumi wa mji wa karatu utaongezeka sana na utaweza kuwasaidia sana
wananchi wa eneo hili hivyo basi wananchi wanatakiwa watumie fursa
ambazo zipo zaidi na sisi tutaendelea kuwa wabunifu zaidi kwa ajili ya
kuweza kuwasaidia wananchi wetu hususani kwenye suala zima la Uchumi
wao wa kila siku"aliongeza Bi Elly


Aliwataka wananchi wa Wilaya hiyo ya Karatu kuhakikisha kuwa
wanaendelea kutumia vema fursa za  maendeleo ambazo zinatolewa na
chama hicho lakini pia wasikubali kupotoshwa juu ya jitiada ambazo
zinafanywa na baadhi ya watu wasiope4nda maendeleo ya jamii nzima


Hataivyo Harambee hiyo ilienda sanjari na mazoezi mbalimbali kama vile
ya upandaji miti,ufanyaji wa usafi wa mazingira pamoja na matembezi
ikiwa ni maazimisho ya kuzaliwa kwa chama cha mapinduzi hapa nchini.

SERIKALI YAJITOSA ARUSHA KWA KULIPA FIDIA


Na Queen Lema, Arusha

SERIKALI imefanikiwa kutoa kiasi cha Bilioni moja na Milioni 750 kama fidia kwa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha mara baada ya kuchukua mradi wa Halmashauri hiyo ujulikao kama Laki Laki kwa ajili ya kujenga miji ya kisasa zaidi.

Akidhibitisha mbele ya kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri mkurugenzi mtendaji Bw Fidelis Lumato alisema kuwa mpaka sasa wameshapokea fidia hiyo ya mradi wa mashamba ya Laki laki ambao ulikuwa chini ya Halmashauri hiyo .

Lumato alisema kuwa pamoja na kuwa mpaka sasa wameshaweza kuachia mradi huo na kutoa kwa Serikali kuu lakini fidia hiyo itasaidia sana kuweza kufanya marekebisho ndani ya Halmashauri hiyo ikiwa ni pamoja na kununua mahitaji ya msingi.

Alidai kuwa fidia hiyo imeweza kurahisisha kazi mbalimbali za halmashauri kwa kuwa yapo mahitaji ya msingi ambayo yalikuwa yanahitajika lakini hapakuwa na jinsi ya kupata fedha kwa ajili ya kununua jambo ambalo wakati mwingine lilikuwa linasababisha malengo kukwama.

Aidha alitaja vitu ambavyo vitaweza kununuliwa kutokana na fidia hiyo kuwa ni pamoja na Gari kwa ajili ya matumizi ya shule za sekondari katika Halmashauri hiyo,tipper  kwa ajili ya shuguli za ujenzi ambapo pia nalo litachangia mapato ya halmashauri hiyo.

Vitu vingine ambavyo vitafanyika kutokana na fidia hiyo ni pamoja na ukarabati wa jengo la kisasa la Halmashuri hiyo ambalo bado halijaweza kukamilika rasmi kwa ajili ya matumizi ya Halmashauri hiyo.

“tunashukuru mungu serikali kutupa fidia ya mradi wa mashamba ya Lakilaki kwani kwa kipindi cha mwaka huu tutafanya vitu vingi na tunaimani kabisa hata mapato nayo yataweza kuongezeka zaidi na hivyo kuwasaidia hata wananchi wenyewe”aliongeza Lumato.

Awali Kaimu Mweka hazina wa Halmashauri hiyo ambaye ni bw Munguabella Kakulima alidai kuwa kwa sasa Halmashauri hiyo imeweka mikakati mbalimbali ya kuweza kuongeza vyanzo vya mapato kwani mpaka sasa kuna tofauti kubwa sana ya ongezeko la mapato katika Halmashauri hiyo ya Arusha Vijijini .

Kakulima alidai kuwa hapo awali waliaanza na mapato ya Milioni 400 lakini mpaka sasa wameweza kufikia ukusanyaji wa mapato wa zaidi ya Bilioni 2 jambo ambalo lengo lake ni kuhakikisha kuwa Halmashauri hiyo inaepukana na tabia ya kuwa tegemezi.

MWISHO.

DC AWATAKA MADIWANI KULIMA MASHAMBA YA MIFANO NA KUACHA KUONGEA BILA KUWA NA USHAHIDI WOWOTE WA KILIMO KWANZA



NaMWANDISHI WETU

MKUU wa wilaya ya Arumeru Munasa Nyirembe amewataka madiwani katika halmashauri ya Arusha Vijijini kuhakikisha kuwa wanakuwa wakulima na wafugaji wazuri ili waweze kuwa mfano wa kuigwa na jamii .
Hataivyo mbali na kuwa na mashamba lakini pia hata mifugo ya kufuga pia wanatakiwa kuunga mkono kauli ya kilimo kwanza kwa matendo na wala sio maneno kama ilivyozoeleka kwa baadhi ya viongozi wa kisiasa.

Munasa aliyasema hayo mapema jana wakati akiongea na madiwani katika baraza la madiwani ambalo lilifanyika jana katika halmashauri hiyo .

Alisema kuwa kudai na kusisitiza matumizi ya Kilimo kwanza pekee kwa njia ya mdomo bado hayatoshi kwani kwa sasa kinachohitajika zaidi ni vitendo na wala sio maneno ambayo wakati mwingine hayatekelezwi.

Aliendelea kwa kusema kuwa ili kuweza kuunga mkono kauli hiyo ya Kilimo kwanza ni lazima hata viongozi wenyewe wahakikishe kuwa wanaaanzan kulima lakini hata kufuga kama mfano ikiwa ni jitiaada zaidi za kuongeza na kuimarisha kilimo kwanza.

"inasikitisha sana kama sisi Madiwani hata wakuu wa wilaya tutasimama na kudai kuwa kilimo kwanza kinatakiwa kutekelezwa kwenye maeneo yetu alafu sisi hatuna hata shamba moja la mfano itakuwa ni aibu tupu ni lazima sasa tuanze kulima 'aliongeza zaidi Munasa.

Pia alidai kuwa kama madiwani wa Halmashauri hiyo ya Arusha Vijijini watawea kuweka utaratibu huo wa kulima basi itaweza kuwa kazi raisi sana ya kuweza kusisitiza kilimo kwanza kwani wananchi wataona umuhimu wa kulima lakini kufuga kwa kutumia mbinu za kisasa zaidi.


Alimalizia kwa kusema kuwa ili kilimo kwanza kiweze kuendelea ni lazima kuwepo na ushahidi kuanzia kwa viongozi wa aina zote lakini pia kuwepo na moyo wa uzalendo ambao utalenga kufanikisha zaidi sera za kilimo kwanza.

MWISHO

UJIO WA HELKOPTA YA CHADEMA ARUSHA WAZUA BALAA KWA CCM

Na Mwandishi wetu, Arusha

Chama cha mapinduzi (CCM)kimesema kuwa kinashangazwa na kitendo cha chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema)kutumia Helikpota kwenye chaguzi zake huku kikidai kuwa ni mkombozi wa wananchi jambo ambalo ni kujitafutia sifa na umaarufu pekee  kwa wananchi.
Hayo yameelezwa na Naibu Katibu mkuu wa CCM ambaye pia ni Naibu waziri wa fedha Mwigulu Nchemba wakati akifungua rasmi kampeni za  udiwani katika kata ya sombetini  mapema jana.
Mwigulu alisema kuwa CCM inashangaa sana Chadema kutumia Helikpota kwenye chaguzi nyingi hapa nchini jambo ambalo wanaonesha wazi kuwa wanatumia gharama kubwa kwa ajili ya kuongeza sifa kwani gharama ambazo zinatumika hadi kumalizika kwa kampeni ni zaidi ya Milioni 200.
Alisema kuwa Gharama ambayo inatumika kwenye uendeshaji wa Helkopta ni gharama ambayo ingeweza kuwasaidia wanachama  wao lakini hata matumizi mbalimbali ya chama hicho ambacho bado kinaonekana kukabiliwa na changamoto nyingi sana
Pia aliwataka wananchi kuhakikisha kuwa kamwe hawatumiki kwenye siasa za sifa na ushahbiki kwani siasa hizo wakati mwingine zinasababisha hata vifo vya watu ambao hawana hatia ya kufa ovyo
Awali Mgombea Udiwani katika kata hiyo ya Sombetini kwa tiketi ya CCM alisema Bw David Mollel alisema kuwa ana mikakati mingi sana ya kuhakikisha kuwa anasaidia kata hiyo endapo kama atapata ridhaa ya kuongoza rasmi kama diwani
David alisema kuwa changamoto ambazo atahakikisha kuwa ameweza kuzitatua ni pamoja na urekebishaji wa barabara, uboreshaji wa masoko, kna uimarishaji wa vikundi vya wanawake na jamii kwa ujumla.
MWISHO

MANYARA WAPEWA JEZI

Na GLADNESS MUSHI, Manyara

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Babati Mkoani Manyara, Mohamed Omary Farah, amegawa vifaa vya michezo vyenye thamani ya sh600,000 kwa timu mbili za soka za Mrara FC na Waangwaray FC za kata ya Babati.
 
Akigawa vifaa hivyo jana kwenye uwanja wa Mrara uliopo mjini Babati, Farah ambaye pia ni Diwani wa kata ya Babati alisema lengo la kugawa vifaa hivyo ni kuhakikisha sekta ya michezo inapiga hatua katika eneo hilo.
 
Alisema anatoa msaada huo wa vifaa vya michezo kwa lengo la kuwaendeleza ambapo timu hizo mbili zilipatiwa kila moja seti moja ya sare za michezo ikiwemo tisheti, bukta na soksi pamoja na mpira mmoja.
 
Alisema kupitia michezo vijana wataweza kujinufaisha kwani hivi sasa michezo ni ajira na pia wataweza kujiweka pembeni na mambo mabaya ikiwemo tabia za uhuni na uvutaji dawa za kulevya.
 
Alisema atahakikisha anakuwa nao sambamba katika michezo kwenye kuwaunga mkono ili timu hizo ziweze kufika madaraja ya juu na kuzileta timu kubwa kwenye mji huo wa Babati.
 
Hata hivyo, mwakilishi wa timu ya Mrara FC Gerald Romly akitoa shukrani kwa niaba ya timu hizo alisema watatumia msaada huo wa vifaa vya michezo kwa kuzitumia ipasavyo kwa ajili ya lengo la kufanikisha michezo.
 
Romly alimshukuru Farah kwa kuwapa msaada huo wa michezo na kuwaomba viongozi wengine kuiga mfano wake, kwani ameonyesha moyo na kujali michezo inayofanywa na vijana wa eneo hilo.
 
MWISHO.

WASOMI VYUO VIKUU ARUSHA WATAKA SERIKALI KUWEKA MTAALA WA MABADILIKO YA TABIA NCHI



NA MWANDISHI WETU, ARUSHA

SERIKALI imeshauriwa kuhakikisha kuwa inaweka mtaala wa mabadiliko ya tabia ya nchi kuanzia ngazi ya shule za msingi ili kuweza kukabiliana na majanga mbalimbali ambayo yanaikumbaa nchi ya Tanzania lakini pia ulimwengu mzima kwa sasa.

Kauli hiyo imetolewa na Bw Peter Mroso ambaye ni Mwenyekiti wa Klabu ya Green Social education(GRESOE) kutoka katika chuo kikuu cha Mt Meru wakati akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wa chuo hicho katika mdahalo wa wanafunzi wa vyuo vikuu Arusha uliofanyika chuoni hapo mapema jana.

Mroso alisema kuwa kwa sasa asilimia kubwa ya wasomi wanafanya kujisomea mambo mbalimbali ambayo yanahusu mabadliko tabia nchi ingawaje kwa sasa nchi inateketea kutokana na majanga hayo hivyo kuna umuhimu mkubwa sana wa kuwepo na mitaala ambayo inahusu mabadiliko tabia Nchi

Aliendelea kwa kusema kuwa endapo kama mitaala ya Tanzania ingeweza kuwa na somo la mabadiliko ya tabia ya nchi basi hata wanafunzi wenyewe wangweza kuwa mabalozi wazuri sana wa masuala hayo ya mabadiliko tabia ya nchi

Amebainisha kuwa njia hiyo ya kuongeza somo la mabadiliko ya tabia ya nchi litaweza kuifanya Tanzania kuepukana na majanga yanayotokana na mabadiliko ya tabia nchi na hivyo kuweza kurudisha hali kama ilivyokuwa hapo mwanzo


Mbali na hayo alidai kuwa nayo serikali inatakiwa kuhakikisha kuwa inaweka mikakati mbalimbali ya kuweza kuwasaidia wananchi wake kwani tafiti mbalimbali zinaonesha kuwa asilimia kubwa ya wananchi bado hawajajua vema masuala ya mabadiliko tabia nchi


Alimalizia kwa kuwataka nao wasomi kutoka katika vyuo vikuu mbalimbali kuweza kujiweka utaratibuw a kufanya midhalo lakini kuelimisha umma juu ya hatua ambazo zinaweza kutumika ili kupambana na mabadiliko tabia nchi ambayo wakati mwingine ndiyo chanzo cha umaskini hata kwenye vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini.

Mwisho

Saturday, January 4, 2014

MWILI WA WAZIRI MGIMWA WAWASILI NCHINI

PICHANI NI MWILI WA ALIYEKUWA WAZIRI WA FEDHA DKT WILLIAM MGIMWA UKIWA UMEWASILI NCHINI BAADA YA KULETWA NA NDEGE YA KENYA
 

KIJANA MMOJA AFUKIWA NA KIFUSI,ASKARI WATATU WAJERULIWA KWENYE MAPAMBANO DHIDI YAO NA RAIA KWENYE MKESHA WA MWAKA MPYA




Na Gladness Mushi, Arusha


KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida kijana mmoja aliyetambulika kwa jina
la Joseph Solomon Mkazi wa Terrat Kwa Muorombo jijini Arusha amefariki
dunia mara baada ya kuangukiwa na kifusi cha moramu katika machimbo ya
Terrat

Akiongea na waandishi wa habari mapema leo kamanda wa polisi mkoa wa
Arusha Liberatus sabas alisema kuwa tukio hilo lilitokea leo (Jana}
majira ya saa tatu na nusu za asubuhi huko Terrat

Alidai kuwa marehemu huyo alifikwa na mauti wakati akiwa anajaribu
kukata kifusi kwa kutumia jembe la kulima ambapo pia wakati anakata
kifusi hicho Lori la kubebea mchanga lilikuja kwa nyuma na kasha
kuangusha kifusi kwa haraka

Kamanda Sabasi alifafanua kuwa wakati Lori hilo linaegeshwa ghafla
liliporomoa kifusi hicho ambacho klilimfukia kijana huyo aliyekuwa
anachimba kwa kutimia jembe na kisha kufariki dunia papo hapo



Aliendelea kwa kusema kuwa mara baada ya dereva huyo wa lori kuona
kuwa kifusi kimeanguka ndani ya machimbo hayo aliamua kugeuza gari na
kisha kukimbia huku akiwa ametelekeza mwili wa kijana huyo



“alipoona kuwa ame[egesha gari vibaya na kusababisha mauti alikimbia
lakini wasamaria wema waliweza kuokoa mwili huo ingtawaje mpaka sasa
tunamtafuta dereva wa lori hilo kwani hata namba ya gari nayo bado
hatujaweza kuijua ila jitiada za haraka zinafanyika’aliongeza Kamanda
Sabasi



Pia alidai kuwa wamiliki wa machimbo ya kuchimba Moramu ndani ya mkoa
wa Arusha wanatakiwa kuwa makini sana lakini pia hata wachimbaji ,
madereva nao wanatakiwa kuchukua tahadhari juu ya kazi hiyo kwani
wakati mwingine uzembe unachangia sana vifo visivyo na hatia.



Wakati huo huo Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha inawashikilia vijana
wanne wakazi wa Wilaya ya Meru kwa kosa la kusababishia askari polisi
majeraha pamoja na raia wema kwenye mkesha wa mwaka mpya

Sabasi alisema kuwa wanaoshililiwa ni pamoja na Selemani
Khamisi,Patrick Richard,Jabu Yasini,pamoja nha Khamisi Juma wote
wakazi wa Meru ambapo siku ya December 31 mwaka jana katika eneo la
Ngarasero Usariver,vijana hao waliweza kuongoza kundi kubwa la
wananchi katika kupingana na Serikali dhdii ya kusherkea kwa amani na
utulivu mwaka mpya

Alidai kuwa askari waliokuwa doria katika maeneo hayo walilazimika
kupambana na vijana hao lakini hawakuskia kwa kuwa tayari walikuwa
wameshawasha moto na kuhamasiaha zaidi vurugu jambo ambalo ni kinyume
cha sheria



“wakati polisi wanapambana kutuliza vurugu kundi kubwa la watu
wakiongozwa na vijana hawa walianza kuwarushia mawe polisi na kufanya
fujo kali ambazo pia zilisababisha askari weru kujeruliwa vibaya
sana”alifafanua hivyo kamanda Sabasi



Aidha aliwataja askari walijeruliwa vibaya kuwa ni pamoja na Mkaguzi
msaidizi wa polisi ambaye ni Athumani,Askari namba G 3475
D/CRamadhani,pamoja na askari mgambo ambaye ana namba 97658 Jacob
wakati kwa upande wa Raia ni Aneth Baltazar,Mary Kwayu ambapo pia
Majerui  wote  wamelazwa katika hospitali ya West Meru kwa ajili ya
matibabu



                MWISHO

Monday, December 16, 2013

VIJANA WA MERU WATAKAOKIUKA MAADILI NA KUIGA TAMADUNI ZA NJE YA NCHI KUCHAPWA VIBOKO 60 HADHARANI

VIJANA WA MERU WATAKAOKIUKA MAADILI NA KUIGA TAMADUNI ZA NJE YA NCHI KUCHAPWA VIBOKO 60 HADHARANI
 
Na Queen Lema, Meru
 
UONGOZI wa Kimila ujulikanao kama Rika la Kilovio kutoka katika kabila la Kimeru
 umepitisha sheria kali ya kudhibiti maadili kwa vijana wa kike na wa kiume hasa wale ambao wanaiga tamaduni  za mataifa ya nje ya nchi ambapo kwa kijana atakayebainika kuiga au kukiuka maadili ya Kitanzania basi atalazimika kuchapwa viboko 60 hadharani
 
Hatua hiyo inakuja mara baada ya baadhi ya vijana katika eneo hilo la Meru kuanza tabia ya kuiga tamaduni lakini hata madili ya mataifa ya nje hali ambayo inachangia kwa kiwango kikubwa maadili kuendelea kuporomoka.
 
Hayo yameelezwa na Bw Akundaely Mbisse ambaye ni kiongozi wa marika ya vijana katika kabila hilo wajulikao kama “Kilovio”wakati wakimsimika na kumuingiza rasmi kiongozi wa vijana katika eneo hilo la Mareu Bw Herieli Mafie mapema jana.
 
Mbisse alisema kuwa utaratibu huo wa kuwapa vijana adhabu ya viboko 60 utaweza kurudisha maana halisi ya kijana wa kabila hilo ambapo kwa sasa jamii ya Mkoa wa Arusha bado inaonekana kuendelea kulelemewa na tatizo la vijana wengi kuiga tamaduni za nje ya nchi huku hali hiyo nayo ikichangia sana hata ubaribifu wa amani ya Kaya,hadi mkoa.
 
Alifafanua kuwa adhabu hiyo ya viboko 60 hadharani itaenda sanjari na vijana wote wenye tabia mbalimbali ambazo hazina tija kwenye jamii hiyo ya Meru kama vile Uzinzi, ulevi wa kupindukia saa za kazi, wizi, Mavazi yanaonesha maumbile,ukosefu wa adabu pamoja na makosa mengine ambayo chanzo chake ni kuiga maadili yasiyokuwa na tija kwennye jamii.
 
“tumejipanga kuhakikisha kuwa wilaya hii ya Meru inakuwa na utofauti wa hali ya juu sana kwani tunao uwezo wa kuwaweka vijana wetu wawe katika maadili mazuri, na masuala kama vile uvaaji wa nguo za ajabu utaisha na kwa hali hiyo jamii itaweza kupungza hata ujinga unaofanywa na baadhi ya vijana wachache huku wakisingizia umaskini’aliongeza Mbisse.
 
Hataivyo Mgeni rasmi katika sherehe hizo ambaye ni Mjumbe wa kamati ya siasa ya mkoa wa Arusha John Palangyo alisema kuwa kuna umuhimu mkubwa sana wa maadili ya kila kabila kurudiwa ili kuweza kuwajengea vijana uwezo wa kufanikiwa zaidi kwenye maisha yao ya kila siku.
 
Palangyo alisema kuwa suala hilo la ulindaji wa maadili lina manufaa sana sio kwa vijana kwani hata kwa taifa kwani kwa sasa wapo baadhi ya vijana ambao wanaharib na kuvunja amani ya Nchi kwa kuwa hawana maadili ambayo yanaanzia ngazi za marika hadi taifa.
 
‘hili jambo la kuweza kuwaweka vijana katika mazingira mazuri ya kimaadili linawezekana kabisa na sisi watanzania tunatakiwa kuondokana na dhana potofu kuwa eti vijana wa sasa hawana maadili wa kuwafundisha maadili ni sisi wazee wa ukoo,rika, na hata wana siasa hivyo basi kila mtu anatakiwa kuzingatia hili lakini pia kuona kuwa kijana wa mwenzake ni wa kwake na hata kama ataharibikiwa basi atachangia uharibifu bila kujali anaharibu kwa nani”aliongeza Palangyo.
 
MWISHO

`WIVU WA KIMAPENZI WASABABISHA MWALIMU KUMWAGIWA MAJI YA MOTO MITHILI YA KUKU

PICHANI NI MWALIMU NEEMA AKIWA AMELALA KWENYE CHUMBA CHA MAJERUI KWENYE HOSPITALI YA MKOA WA ARUSHA MT MERU,PICHA NA QUEEN LEMA

MWALIMU AMWAGIWA MAJI YA MOTO NA KUUNGUWA VIBAYA KWA KUHOFIWA KUWA ANAMAHUSIANO NA MUME WA MTU

Na Queen Lema, Arusha

KATIKA hali isiyokuwa ya awaida Mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Neema Teti ambaye pia ni mwalimu,mkazi wa Shangarai mkoa wa Arusha amepata majeraha makubwa sana mara baada ya kumwagiwa maji ya moto sehemu zote za mwili wake mara baada ya kuhofiwa kuwa anatembea na mume wa mtu

Aidha tukio hilo lilitokea December tisa majira ya asubui katika eneo la Shangarai ambapo  Bi Neema alimwagiwa maji ya moto na rafiki yake kwa kuhofiwa kuwa anatembea na mume wake

Akiongea na “MALKIA WA MATUKIO ”mapema jana katika hospitali ya Mt Meru ambapo anapatiwa matibabu Bi Neema alisema kuwa siku hiyo ya December tisa rafiki yake ambaye bi Tatu  Msuya alienda nyumbani kwake na kumuomba kuwa waweze kwenda kwa pamoja kwani kuna matatizo na hivyo yeye ndio anatakiwa kusimamia familia yake.

Neema alidai kuwa mara baada ya kufika nyumbani kwa rafiki yake  kwa malengo ya kumsaidia shida aliyonayo ambayo alidai ni msiba lakini walipofika mambo hayakuwa hivyo

Aliongeza kuwa mara baaada ya hapo rafiki yake ambaye ni Bi Tatu alimtaka aingie ndani ili waweze kupanga mambo yao ya jinsi ya kusaidia familia kwa kipindi hicho cha msiba jambo ambalo hakuwa na wasiwasi nalo kwa kuwa walikuwa wanaaminiana sana

“baada ya hapo nilishangaa sana kwani alifunga milango yote na kuongeza makofuli jambo ambalo lilinipa shida kwa haraka kwani niliwaza labada anataka mazungumzo yawe siri”aliongeza Neema

Alidai kuwa mara baada ya tukio hilo la kufungwa milango,yote ya nyumba ya rafiki yake ndipo alipomtaka aweze kunywa soda lakini alikataa kwani ilikuwa ni asubui sana  lakini pia soda hiyo ilikuwa na chupa ndogondogo jambo ambalo halikuwa na ishara nzuri

“niloishangaa kwa kuwa aliniletea soda ambayo ilikuwa na chupa ndogondogo ndani lakini nilijiuliza kwanini huyu rafiki yangu ananilazimisha zaidi ninywe soda asubui na inaonekana inasumu machale yalinicheza lakini sikuweza kutoka kwa kuwa alikuwa tayari ameshafunga milango yote huku baadhi ya watu wa familia yake nao wakiwa wamefungiwa ndani”aliongeza zaidi Neema

Pia alidai baaada ya muda  mfupi rafiki yake alikuja na maji ya moto ambayo yamechemka sana na kuanza kumwagia bila kujali kuwa ni rafiki yake jambo ambalo pia lilifanya ashindwe kupata msaada wa haraka kwa kuwa milango yote alikuwa ameifunga

“alinimwagia maji ya moto kama kuku bila hata kunionea huruma huku akidai kuwa analipiza kwa kuwa ameambiwa mimi natembea na mume wake na nina mimba ya mume wake jambo ambalo sio kweli na alidai anachotaka ni kunitoa roho”aliongeza Neema

Alidai kuwa baada ya tukio hilo alifungua mkilango na kisha kuchukua mizigo yake haraka na kisha kukimbia kusikojulikana jambo nalo liliwafanya majirani wa eneo hilo kuweza kukusanyika na kisha kumpa msaada wa kwenda kituo cha polisi kwa ajili ya kutoa taarifa lakini pia kumfikisha hospitalini

Awali Muuguzi wa zamu katika hospitali hiyo ya Mte Mt Meru  ambaye ni Bi Neema Baya alisema kuwa hali ya mgonjwa huyo inaendelea vizuri japokuwa bado ana maumivu makali na pia ametoa wito kwa wanawake wengine kuacha tabia ya ukatili kama hiyo kwani inaweza kusababisha vifo.

Wakati huohuo Jeshi la polisi mkoa wa Arusha kupitia Kitengo cha dawati la jinsia limedai kuwa bado linamtafuta Bi Tatu kwa kosa ambalo amelifanya kwani tukio hilo ni la kinyama na nituykio ambalo halipaswi kutokea tena kwenye jamii

Akiongea kwa niaba ya Jeshi hilo Maria  alisema kuwa kwa kuwa jeshi hilo lina mkono mrefu basi litahakikisha kuwa linamtafuta Bi tatu na kisha kumfikisha mahakamani kwa kuwa amefanya kitendo kibaya sana kwa mwenzake baada ya kumuhisi kuwa anamahusiano ya kimapenzi na Mume wake

MWISHO


UKOSEFU WA HUDUMA ZA MAJI ZA UHAKIKA CHANZO CHA NDAO NYINGI KUVUNJIKA, PIA CHANZO CHA MIMBA ZA UTOTONI





IMELEZWA kuwa ukosefu wa huduma za uhakika za maji hasa maeneo ya vijijini ni chanzo mojawapo cha ongezeko la mimba  za utotoni lakini pia uvunjikaji wa ndoa nyingi huku hali hizo zikisababisha pia ongezeko la watoto mitaani ndani ya mji wa Arusha

Pia hali hiyo ya ukosefu wa maji kwenye kaya pia inasababisha umaskini wa hali ya juu sana ingawaje Serikali kwa sasa inaweka mikakati mbalimbali ya kupambana nao.

Hayo yameelezwa na Bi Asha Shabani ambaye ni Katibu wa Mradi wa maji ujulikanao kama Mangole uliopo maeneo ya Kisongo jijini hapa,wakati akielezea mradi huo lakini pia umuhimu wa miradi ya uhakika ya maji hasa kwa maeneo ambayo yapo nje ya miji

Asha alisema kuwa ukosefu wa maji ya uhakika hasa katika maeno ambayo yapo nje kidogo ya miji ni changamoto kubwa sana kwa wanawake kwa kuwa asilimia kubwa huambulia uchovu lakini pia hata kipigo kutoka kwa wenza wao kwa kuwa hutumia muda mrefu kwa ajili ya kusaka maji

Mbali na hayo alisema kuwa ukosefu huo hauathiri pekee wanawake bali hata mabinti wadogo ambao baadhi ya vijana hutumia mwanya huo katika kuwadanganya ili waweze kuwapa maji au kuwasaidia kubeba maji kwa uraisi jambo ambalo nalo ni chanzo kikubwa cha mimba za utotoni lakini pia mdondoko wa elimu kwa watoto wa kike

Akiongelea Mradi huo wa MANGOLE ambao unawasaidia wananchi kutoka katika kata za Matevesi,Ngorobobu, na Lemguru alisema kuwa umekuwa ni faida kubwa sana kwenye jamii hiyo kwani hapo awali kulikuwa na matatizio mengi sana

Alitaja matatizo hayo ni pamoja na baadhi ya wanawake kukosa ndoa,huku wengine wakiambulia wajukuukabla ya wakati kutokana na udanganyifu ambao ulikuwa uanendelea kwa watoto wa kike na vijana pia.

“hapo awali tulikuwa tunalazimika kwenda kilomita mpaka 20 kwa siku ili kutafuta maji lakini toka mradi huu uletwe kwa hisani ya Word Vision umekuwa na faida kubwa sana na hivyo tunataka tuhakikishe kuwa hata wanawake wa maeneo mengine ndani ya mkoa wa Arusha nao wanaweza kufaidika na miradi kama hii ili waweze kuepukana na changamoto za uhaba wa maji”aliongeza Asha

Wakati huohuo Mwenyekiti wa Mradi huo ambaye ni Profesa Calvin Marealle alisema kuwa pamoja na kuwa mradi huo umekuwa ni faida kubwa sana kwa jamii lakini bado unakabiliwa na changamoto mbalimbali kama vile Ukosefu wa umeme wa uhakika hali ambayo wakati mwingine inasababisha baadhi ya wananchi kutoka katika vijiji hivyo vitatu kukosa maji ya uhakika

Profesa Marealle aliongeza changamoto nyingine ni pamouja na baadhi ya wananchi kuiba na kuharibu miundombinu ya maji hali ambayo ni chanzo kikubwa sana cha hasara kwenye miradi hiyo.

MWISHO

WATENDAJI 17 KUTOKA KATIKA KATA 17 MERU HAWANA SIFA ZA KUWA NA CHEO HICHO

WATENDAJI 17 KUTOKA KATIKA KATA 17 MERU HAWANA SIFA ZA KUWA NA CHEO HICHO


IMEELEZWA kuwa watendaji wa kata 17 kutoka katika Wilaya ya Meru mkoa
wa Arusha hawana sifa za kuwa watendaji kutokana na kuwa na elimu
chini ya kiwango hivyo wanatakiwa kuacha kukaidi amri ya Serikali
iliyowataka waende shule kwa ajili ya kujiendeleza



Aidha Serikali ilishatoa waraka toka July mosi mwaka 2003 kuwa
watendaji wanatakiwa kwenda shule lakini mpaka sasa watendaji hao
hawajaweza kwenda shule kutokana na sababu mbalimbali



Hayo yameelezwa na Afisa utumishi wa Wilaya hiyo Anord bureta wakati
akielezea kazi mbalimbali za watendaji hao kwenye baraza la madiwani
wa Halmashauri hiyo kwa malengo ya kuelezea changamoto mbalimbali
ambazo zinawakabili watendaji hao mapema jana


Bureta alisema kuwa July Mosi 2013 Serikali iilitoa tamko ambalo
liliwataka watumishi hao kuweza kwenda mashuleni lakini mpaka sasa
tunaweza kusema kuwa agizo hilo halijaweza kutimizwa jambo ambalo ni
madhara makubwa kwa ajili ya utendaji kazi lakini pia hata kwa ajili
ya maslahi ya umma



Pia alisema kuwa ili kuweza kukabiliana na hali hiyo kwa sasa wameweka
utaratibu wa watendaji hao kuweza kwenda kusoma ili kuweza kukidhi
matakwa ya sheria hiyo ambayo inawataka kuwa na elimu lakini kuweza
kwenda sanjari na mpango wa serikali wa sasa yaani Big Result


Akiongelea suala hilo kwa niaba ya madiwani wa halmashauri hiyo Makamu
Mwenyekiti Frida Kaaya alisema kuwa  ni lazima watendaji hao waweze
kwenda shule lakini pia hata Halmashauri ihakikishe kuwa inasimamia na
kutatua changamoto zao ambazo zinajali maslahi


‘hapa ni lazima tujiulize kuwa hawa watendaji walikosa fedha au fursa
za kwenda kusoma au walikaidi agizo hilo lakini pia kuanzia sasa
maslahi ya watendaji yawekwe hadharani na pia waweze kupewa kwa
wakati ili nao pia waweze kupata moyo wa kufanya kazi”aliongeza Frida



Pia  Bi Frida alidai kuwa kama Halmashauri lakini pia Serikali
itashindwa kuwajali watendaji ni wazi kuwa lawama zitakuwa nyingi sana
kwani wao ndio wapo na wananchi kila siku ingawaje kwa sasa zipo
changamoto lukuki ambazo zinasababishwa na watendaji hao.



MWISHO

WANAWAKE 200,WATOTO 1000 WAFANIKIWA KUPEWA ELIMU PAMOJA NA UWEZESHWAJI KIUCHUMI KWA AJILI YA KUPAMBANA NA UMASKINI



Na Queen Lema, Arusha

ZAIDI  ya watoto elfu pamoja na wanawake mia mbili kutoka jijini
Arusha wamefanikiwa kuwezeshwa kiuchumi pamoja na kupatiwa elimu
mbalimbali ili kupunguza kasi ya ongezeko la watoto mijini lakini pia
kwenye vituo vya kulelea watoto yatima

Hataivyo watoto hao pamoja na wanawake hao wamefanikikiwa kupatiwa
elimu pamoja na uwezeshwaji hali mabyo mpaka sasa imeweza kuonesha
mafanikio ya hali ya juu sana.

Wanawake hao pamoja na watoto wamewezeshwa na Kijiji kinachotoa malezi
mbadala ya watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu(SoS)chini ya mradi
wa kuimarisha familia(FSP)unaotekelezwa sehemu mbalimballi nchini.

Hayo yamelezwa na Mratibu wa utetezi kutoka katika kijiji hicho cha
SOS ambaye ni John Batista wakati akiongea kwenye maazimisho ya
ukatili wa kijinsia kwa wanwake na watoto yaliyofanyiika katika eneo
la Kimnyaki Jijini Arusha mapema wiki hii

Batista alisema wanawake hao 200 pamoja na watoto elfu moja wameweza
kusaidiwa kutokan ana kampeni ambayo inaendeshwa chini ya SOS ya
kupinga nakutokomeza suala zima la unyanyasaji kwenye kwenye jamii.


Alisema kuwa kwa kuwawezesha wanawake hao pamoja na watoto kutasaidia
sana kupungua kwa umaskini kwenye jamii kwani umaskini unapokithiri
basi unachangia hata suala zima la malezi nalo kuwa duni sana.


Mbali na hayo Batista pia alitoa wito kwa jamii kuhakikisha kuwa
wanachana na ukatili dhidi ya wanawake lakini pia kwa watoto kwani
hali hiyo ndiyo chanzo cha ongezeko la watoto wa mitaani

SHULE ZA SEKONDARI AMBAZO ZINA MAABARA KUPEWA HUDUMA YA INTERNET BURE

SHULE ZA SEKONDARI AMBAZO ZINA MAABARA KUPEWA HUDUMA YA INTERNET BURE

Na Queen Lema, Arusha

KAMPUNI ya Smile ya mawasiliano ya Smile imeweka mikakati ya kusaidia
shule za Serikali ambazo zina maabara kwa kutoa huduma ya
mawasiliano(internet)bure itakayowawezesha wanafunzi waweze kusoma kwa
kupitia mitandao.

Hayo yameelezwa na Deo Ndejembe ambaye ni meneja kitengo cha mauzo
katika kampuni hiyo wakati akiongea kwenye uzinduzi wa mtandao wa
smile kwa mkoa wa Arusha mapema leo.

Deo alisema kuwampango huo unalenga kuimarisha huduma za maabara
katika shule za sekondari za serikali kwani wanafunzi wakiwa na huduma
hizo wataweza kusoma na kwenda pamoja na soko la dunia ambalo
linategemea zaidi huduma za mitandao.

Alidai kuwa mpango huo utaweza kuwanufaisha zaidi shule ambazo zina
maabara pamoja na kompyuta hivyo basi hata kwa shule ambazo hazina
maabara zinatakiwa kuweka mara moja ili ziweze kunufaika na mpango huo
ambao umeshaanza

“tunataka kuona kuwa lile lengo la serikali ambalo lililenga shule
ziwe na maabara linatimia lakini pia maabara ziwe za kisasa zaidi na
ziweze kupata teknolojia ya mawasiliano bure kwani itasaidia hata
ufaulu wa masomo kama sayansi kuweza kuongezeka’alisisitiza Deo

Wakati huo huo alidai kuwa mpango huo wa kutoa huduma za Tekonlojia
umeshaanza kwa shule 10 ndani ya Jiji la Dar es saalam lakini kwa mkoa
wa Arusha shule ya Arusha School tayari imeshanufaika na mpango huo
ambao ni bure

Naye Afisa mawasiliano wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania
(TCRA)Innocent Mongi alidai kuwa bado mkoa wa arusha unahitaji huduma
za mawasiliano zaidi kutokana na mwingiliano wa huduma kama vile
uchumi, na utalii

Mongi alidai kuwa uwepo wa mtandao huo wa Smile kwa mkoa wa arusha pia
utachangia wafanyabiashara  wakubwa na wadogo kuweza kufanya biashra
kutoka katika masoko mbalimbali duniani .

“napenda kuwasihi wakazi wa Arusha kuhakikisha kuwa wanatumia vema
mtandao huo ili kuraisisha shuguli mbalimbali za maendeleo kwa mkoa wa
arusha na kutokana na hili tunaamini kuwa Arusha itapata mabadiliko
makubwa”alisema Mongi

WAZIRI AZITAKA NCHI ZA AFRIKA ZIUNGANE ILI KUPAMBANA NA RUSHWA


WAZIRI wa nchi ofisi ya rais anayeshughulikian utawala bora George
Mkuchika amezitaka nchi za Afrika  kujenga umoja na kupeana uzoefu
katika vita vya kupambana na rushwa huku  nchi hizo z ikitakiwa
kujenga sera za uwazi kwenye sekta nzima ya rasilimali ili waweze
kunufaika nazo ikiwa ni pamoja na kupaza sauti moja kuomba kurejeshwa
kwa fedha zilizoko nje ya bara la afrika.

Mkuchika alitoa kauli hiyo jana  alipokuwa akifunga na kusherehekea
maadhimisho ya siku ya umoja wa mataifa ya mapambano dhidi ya rushwa
yaliyofanyika jini hapa

Alisema kuwa umoja una  nguvu katika kupambana na rushwa hivyo ili
kuhakikisha kuwa swala hilo linatokomezwam nchi za afrika zinapaswa
kutekelza kwa vitendo mkataba wa umoja wa afrika dhidi ya rushwa kwa
kila nchi kujiunga moja kwa moja kwa kutoa uzoefu juu ya mapambano
dhidi ya rushwa ambayo yameonekana kurudisha nyuma maendeleo ya bara
la afrka.

Alieleza kuwa pamoja na chi za Ulaya kuwa mstari wa mbele katika
mapambano dhidi ya rushwa lakini nchi hizo zimekuwa zikikumbatia
Uhamishaji wa fedha kutoka bara la afrika na kukaa kimya
kilawanapotakiwa urejeshwaji wa fedha zilizopo kwenye mataifa hayo


Aidha alifafanua kuwa nchi 30  zimesaini mkataba wa umoja wa mataifa
wa mapambano dhidi ya rushwa kati ya nchi 44 zinazotakiwa kusain
mkataba huo hivyo kuzitaka nchi zilizobaki kujiunga na umoja huo ili
kuliletea maendeleo bara la afrika na kuwa na sauti moja ya mapambano
dhidi ya rushwa huku akizitaka nchi za bara la afrika kutambua kuwa
mapambano si ya rushwa si ya mtu moja bali ya watu wote.

Nae mkurugenzi wa takukuru nchini Drt Edward Hosea alisema kuwa bara
la afrika bado lina safari ndefu katika mapambano ya vita vya rushwa
kwani kati ya nchi za afrika 34 kati ya 44 ndizo amabzo zimesaini
mkataba wa mapambano ya rushwa huku akidai kuwa mikataba mingi
inaingia kwenye rasilimali za nchi za bara la afrka haina uwazi na
sheria zinazotumika  hazimnufaishi mwananchi wa kawaida dhidi
yamapambano ya rushwa.

Aidha aliitaka serikali kuweka sera ya uwazi kwenye mikataba ya
wawekezaji wa rasilimali ya gesi ili iweze kuwanufaisha watanzania na
sheria zitakazotungwa iwe ya uwazi na yenye faida kwa watanzania
hukuakizishawishi nchi ambazo hazijatakeleza mkataba wa umoja wa
mataifazifanye hivyo mara moja kwani bara la afrka ndilo linalohitaji
maendeleo makubwa hivyo bila kuungana hawataweza kufanikiwa.

MWISHO.

KIKUNDI CHA OLGILAI CHANGAMKENI YOUTH GROUP CHAFANIKIWA KUTOA MSAADA WA MADAWATI,NA VIFAA VYA SHULE YA OLGILAI


KIKUNDI CHA OLGILAI CHANGAMKENI YOUTH GROUP CHAFANIKIWA KUTOA MSAADA WA MADAWATI,NA VIFAA VYA SHULE YA OLGILAI

Na Queen Lema, Arusha


KIKUNDI cha Olgilai Changamkeni Youth Group kilichopo maeneo ya Olgilai mkoani Arusha kwa kushirikiana na wadau wengine wa elimu wameweza kutoa msaada wa madawati zaidi ya 50 pamoja na vifaa vingine kama vile meza, kabati, na viti  kwa shule ya msingi Olgilai huku lengo likiwa ni punguza changamoto za kielimu shuleni hapo

Hataivyo msaada huo ambao ulitolewa mapema jana ulienda sanjari na uzinduzi wa kikundi hicho ambacho kimelenga kutatua changamoto mbalimbali katika kijiji hicho cha Olgilai na Mkoa wa Arusha kwa ujumla.

Akiongea mara baada ya kukabidhi msaada huo kwa shule ya msingo Olgilai Mwenyekiti wa kikundi hicho Benjamini Justin alisema kuwa wameamua kuchangia zoezi zima la elimu ili kwenda sanjari na mpango wa serikali wa matokeo ya haraka(BRN)

Benjamini alidai kuwa hapo awali shule hiyo ilikuwa inakabiliwa na changamoto kubwa sana ya ukosefu wa madawati na vifaa vingine hali ambayo ilifanya wazazi wa eneo hilo ambao ni wanakikundi kuhakikisha kuwa wanatafuta mbinu ya kukabiliana na changamoto hiyo.

Alifafanua kuwa baada ya kuweka mikakati mbalimbali waliweza kuwashirikisha wadau wengine ambao nao waliweza kuungamkono na kuhakikisha kuwa wanapunguza tatizo la uhaba wa madawati kwenye shule hiyo ya Olgilai.


Wakati huo huo alidai kuwa pamoja na kuwa wameweza kufanikisha kutoa msaada huo wa madawati, meza,viti, madaftari, na kalamu lakini bado wanakabiliwa na changamoto lukuki ambazo wakati mwingine zinakwamisha jitiada zao

Alitaja changamoto hiyo kuwa ni pamoja na baadhi ya fursa za mikopo ni finyu kwa kuwa taasisi hizo hazitoi mikopo kwa vikundi jambo ambalo linakwamisha jitiada za maendeleo ya vikundi hasa vile vya mitaa.

“pamoja na kuwa leo tumeweza kutoa msaada huu kwa shule hii pamoja na kuzindua rasmi kikundi chetu bado changamoto hii tunaifikiria sana hivyo basi tunaomba taasisi za Fedha kuhakikisha kuwa zinatuangalia ili nasi tuweze kusaidia jamii kama tulivyofanya leo”aliongeza Benjamini

Wakati huo huo akiongea kwa niaba ya wanafunzi ambao ndio walengwa wa msaada huo Irene Peter alidai kuwa msaada huo wa madawati utasaidia sana kuongeza ufanisi wa elimu kwani hapo awali wanafunzi shuleni hapo walikuwa wanalazimika kuandika Miandiko mibaya kwa kuwa hawakuwa na madawati.

WAZEE ARUSHA WAPATIWA MSAADA


Asasi ya Informal Sector team(INSERT)imefanikiwa kutoa msaada wa Mablanketi yenye thamani ya zaidi ya milioni moja na nusu kwa Jukwaa la wazee wa mkoa wa Arusha (JUWA)huku lengo halisi likiwa ni kuhakikisha kuwa wazee wote wanaendelea kusihi maisha ya upendo na amani

Akiongea na wazee hao mara baada ya kuwapa msaada mratibu wa asasi hiyo ya INSERT,Japhet Saruni alisema kuwa msaada huo unalenga kuhakikisha kuwa afya za wazee zinaendelea kuboreka zaidi

Aidha Saruni alisema kuwa kwa sasa wazee wengi sana wamekuwa wakisahulika kwenye maslahi yao hali ambayo inachangia sana kuzorotesha hata afya zao ingawaje sera za wazee bado zipo

Alifafanua kwa kusema kuwa hali hiyo imechangia kwa kiwango kikubwa sana wazee wengi kupoteza maisha kabla ya siku zao hivyo basi ndio maana Asasi hiyo ya INSERT ikaweza kuona kuwa kuna umuhimu wa kuwasaidia wazee

Pia alisema kuwa kuna umuhimu wa jamii kuhakikisha kuwa wanatatua kero za jamii kila mara kwani kwa sasa jamii imeacha kabisa kuwasaidia wazee huku wazee nao wakikabiliwa na changamoto kubwa sana

Hataivyo alifafanua kuwa kama jamii itaweza kuwakumbuka wazee kila mara basi kasi ya ongezeko la vifo visivyo vya lazima hasa vya wazee vitaweza kupungua kwa kiwango kwani takwimu zinaonesha kuwa wazee wengi wanakufa kutokana na kuwa hawana msaada wa kuwasaidia.


Awali wazee waliopewa msaada walisema kuwa pamoja na kuwa wamepewa msaada huo bado kuna umuhimu wa sera za wazee kuweza kutekelezwa hasa kwenye sekta muhimu kwani sera hizo zipo lakini hazitekelezwi na baadhi ya watendaji tena wwa Serikali.

MWISHO

WASANII ARUSHA WAHIDIWA NEEMA


KAMPUNI ya Mkundi Production yenye makao makuu Jijini Arusha imeahidi kuibua lakini pia kuwezza kuendeleza vipaji vya  mbalimbali vya vijana ikiwa ni pamoja na kuweza kuwasaida kurekodi na kusambaza kazi zao

Aidha kwa sasa asilimia kubwa ya vijana wenye vipaji vya uimbaji wanashindwa kufikia malengo yao mbalimbali kwa kuwa hawana uwezo wa kuingia studio lakini pia kutoa na kughramikia baadhi ya gharama hali ambayo inachangia sana kupoteza vipaji vingi

Hayo yameelzezwa na mkurugenzi jmtendaji wa kampuni hiyo Carlos Mkundi mapema jana mara baada ya kuzindua Album ijulikanayo kama “NIMETOKA  MBALI”ambayo imejumuisha vijna mbalimbali wa mkoa wa Arusha

Mkundi alisema kuwa kampuni yakeimejidhatiti kuhakikisha kuwa kila msanii mwenye uwezo wa kuimba aweze kunufaika na kipaji chake na kamwe kisingizo kuwa ghrama ni chanzo kisiwepo

Aidha alidai kwa sasa wasanii wa nyimbo mbalimbali ndani ya mkoa wa Arusha wanashindwa kuimba na kutoa album zao kwa kuwa kuna changamoto lukuki sana ambazo ndizo chanzo kikubwa cha wao kushindwa kufanya vema zaidi

Wakati huo huo alisema kuwa kwa kipindi cha mwaka huu Kampuni yake tayari imeshwaweza kuwasaidia wasanii saba kuweza kurekodi album zao na hivyo mikakati zaidi bado itaendelea kuwekwa

Pia alidai kwa kila mwaka wasanii saba kutoka Jijini Arusha wataweza kurekodi kwa msaada wa kampuni hiyo lakini hata wale ambao bado hawajaweza kurekodi basi watapewa misaada mbalimbali ambayo inalenga kuinua vipaji vyao zaidi

MWISHO

Wednesday, December 4, 2013

HALMASHARI YAURARUSHA VIJIJINI WAFANIKIWA KUKUSANYA MILIONI 682 KUTOKA KATIKA VYANZO VYAKE VYA MAPATO


Wilaya ya Arusha Vijijini imefanikiwa kukusanya kiasi cha Milioni 682
sawa na asilimia 31.8 kutoka katika vyanzo vyake vya mapato ingawaje
kwa kipindi cha mwaka 2013,2014 wanatarajai kukusanya kiasi cha zaidi
ya bilioni mbili sanjari na kuibua vyanzo vya mapato ambavyo
vitaimarisha zaidi uchumi wa wananchi wake.

Hayo yamelezwa mapema jana na Kaimu mweka wa Halmashauri hiyo bw
Munguabela Kakulima wakati akielezea Vyanzo vya mapato ambavyo
vitakwenda sanjari na mpango wa matokeo makubwa (Big Result Now)kwenye
wilaya hiyo

Kakulima alidai kuwa kupatikana kwa fedha hizo kunatokana na jitoada
mbalimbali ambazo zinafanywa na idara yake ambapo ndipo zilipochangia
mafanikio hayo

Aidha alidai mpaka mwaka wa fedha wa sasa uweze kuisha wanatarajia
kuvuka hata lengo ambalo walikuwa wameliweka na hivyo kukusanya fedha
nyingi zaidi hali ambayo itachangia shuguli mbalimbali za maendeleo
kuweza kufanyika kwa haraka

Mbali na hayo alidai kuwa kwa sasa wanamikakati mbalimbali ya
kuhakikisha kuwa wanaweka uwezekano wa kubaini vyanzo vipya vya mapato
ambavyo navyo vitaweza kuweka halmashauri hiyo kwenye kiwango cha juu
sana

Mkakati mwingine ambao nao aliweza kuutaja ni pamoja na kuweza kuwapa
wananchi elimu ya kuweza kulinda vyanzo vya mapato lakini kuweza
kuonesha umoja baina ya watendaji wa halmashauri hiyo ili kuweza
kuharakisha shuguli mbalimbali za ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri

Awali alisema kuwa pamoja na mikakati na jitiada ambazo zinafanywa na
idara ya fedha katika Halmashauri hiyo zipo changamoto ambazo nazo
zinachangia kukwamisha malengo mbalimbali ya ukusanyaji wa mapato
kutoka katika vyanzo

Kakulima alidai kuwa changamoto hizo ni pamoja na baadhi ya wanasiasa
kuingilia shuguli pamoja na vyanzo vya mapato hali ambayo wakati
mwingine inasababisha waone kuwa halmashauri hiyo inachangia sana
kuwadidimiza.

Naye mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo alisema kuwa ili matokeo ya
haraka yaweze kuja katika Halmashauri hiyo vyanzo vya mapato
vinatakiwa kulindwa lakini nao watendaji wa idara ya fedha wanatakiwa
kufuata wajibu wao wa kulinda na kuitetea halmashauri hiyo.

MWISHO

ACHENI UKIRITIMBA USIOKUWA WA LAZIMA

MKUU wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, amewataka watumishi wa
serikali na taasisi zake kuondoa ukiritimba usio wa lazima katika
kutoa huduma kwa wadau wa maendeleo, hususani, wanaowafundisha
wakulima wadogo wadogo  kilimo cha kibiashara ili waweze kujipatia
maendeleo.




Alitoa maagizo hayo wakati akifungua maonesho ya vikundi vya wakulima
zaidi ya 21 kutoka mikoa ya Arusha na Kilimanjaro, yaliyoandaliwa na
Shirika lisilo la kiserikali la Farm Concern International (FCI)
wakishirikiana na World Vision Tanzania, World Vision Canada na
Shirika la Maendeleo la Canada (CIDA), jijini hapa jana.




Mkurugenzi wa FCI Afrika, David Richiu, alisema shirika lake ambalo ni
wakala wa masoko kwa wakulima wadogo wadogo, limejikita kuwafundisha
kilimo cha kibiashara, uongozi katika vikundi kupitia mfumo kijiji
biashara, wanawapa mbinu za kutafuta masoko ya mazao, utunzaji wa
mazingira, elimu ya lishe bora kwa familia, uhifadhi wa mazao,
huwaunganisha na watu wa pembejeo na huduma za ugani.



Alisema maonesho hayo ya kilimo yenye kauli mbiu, “Jua mahitaji ya
soko zalisha kibiashara,” yamedhaminiwa na mradi wa SMART (Sustainable
Market led Agriculture Resource) na wanafanya kazi katika wilaya za
Arusha, Monduli, Siha, Arumeru na Hai.



Baadhi ya miradi ambayo shirika lake linatekeleza nchini ni pamoja na
kukuza uzalishaji na ulaji wa mboga mboga za kiasili unaotekelezwa
katika wilaya za Arusha, Arumeru, Hai, Siha, Same na Karatu, lishe kwa
wakulima wa kahawa unaotekelezwa wilaya za Arusha, Arumeru, Siha na
Hai.



Mingine ni mradi wa muhogo ulioanzia kijiji cha Mbuguni wilayani
Arumeru, mradi wa ndizi na viazi vitamu hasa viazi lishe vyenye
asilimia nyingi ya vitamin A ambao wanatarajia kuupanua kwenye mikoa
mingine nchini.



Kwa upande wake, Kiongozi mkazi wa FCI nchini, Wiston Mwombeki,
alisema ili mkulima aweze kupata soko yampasa kwanza ajue mahitaji ya
soko kama vile mazao yanayohitajika sokoni, ubora, mahali walipo
wanunuzi, kiwango kinachotakiwa, ufungashaji, uhifadhi na usafirishaji
wa mazao, kilimo bora na pembejeo bora.


MWISHO.

OFISI ZA CHADEMA ARUSHA ZACHOMWA MOTO NA WATU WASIOFAHAMIKA

Na Queen Lema, Arusha



KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida watu wasiofahamika jana(leo)wamevamia ofisi ya Chadema Kanda ya kaskazini iliopo Jijini Arusha na kisha kuanza kuwasha moto ambao ulisababisha hasara kubwa sana.

Akizungumza na “Majira”katibu wa kanda ambaye pia ni katibu wa mkoa wa Arusha Chadema, Amani golugwa alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya asubuhi katika ofisi za kanda zilizopo eneo la Ngarenaro mjini Arusha.

Golugwa alisema kuwa watu hao waliingia mara baada ya mlinzi kutoka zamu ya kulinda usiku ambapo walilazimika kuvunja kioo kikubwa na kisha kuingia ndani ili kufanya lile walilolikusudia.

Aliendelea kwa kusema kuwa baada ya kuingia ndani walipanda kwenye dari la nyumba hiyo ambapo walianza kutafuta uwiano wa chumba ambacho kinahifadhi nyaraka mbalimbali za Chama na kisha kuwasha moto

Alidai kuwa wakati wanawasha moto huo ghafla uliweza kulipuka hivyo lengo halisi halikuweza kutimia kwa haraka na badala yake walishuka na kuanza kukimbia wakati jingo letu likiwa linateketea kwa moto
Pia alisema baada ya watu hao kuona kuwa hawawezi kuchoma chumba hicho walitengeza shoti kubwa ya umeme ambayo iliweza kusababisha vyumba vya choo na bafu kuunguwa na hatimaye walishuka wakiwa wanakimbia huku moto ukiendelea kutapakaa kwenye jingo la ofisi hiyo.

“kilichofanya tuweza kusema kuwa walikuwa na lengo la kuchoma chumba hiki ambacho kinahifadhi nyaraka muhimu za chama ni baada ya kuona kuwa wameacha maeneo yote na kisha kuingia hapa na inavyoonekana lengo lao ni kupoteza ushahidi wa vitu mbalimbali ambavyo tunapambana navyo”aliongeza Golugwa

Katika hatua nyingine Golugwa alisema kuwa tukio hilo la kuchoma ofisi linaonesha kuwa wapo baadhi ya watu ambao wanatumia muda na fikra zao nyingi kuwawinda viongozi wa Chadema na kuingilia hata kwenye maisha yao ya kila siku

Aidha aliwataja watu ambao wanawindwa sana kwa ajili ya kujeruliwa ni pamoja nay eye ,mbunge wa jimbo la Arusha Mjini Goodbless Lema, pamoja na mwenyekiti wa wilaya ambaye ni Ephata Nanyaro
‘mpaka sasa tunawahisi watu watatu katika sakata hili na kwa maana hiyo tumesharipoti polisi ili waanze mara moja upelelezi wao lakini jingo letu tumeliwekea ulinzi mkubwa sana na kumbukumbu zote zipo ingawaje mpaka sasa bado hatujaweza kujua kwanza ni hasara ya shilingi ngapi tumeipata’aliongeza Golugwa

POLISI ARUSHA WASHIKILIA SILAHA ILIYOKUWA IKITUMIKA KWENYE MATUKIO YA UHALIFU



JESHI la Polisi mkoani Arusha,linashikilia silaha aina ya short gun
WINCHESTER  yenye namba za usajili c.056900 pamoja na mmiliki wake
ambaye alikuwa anaitumia kwenye matukio mbalimbali ya uhalifu kwa mkoa
wa Arusha na nje ya mkoa wa Arusha

Pia Polisi mkoa wa Arusha ilifanikiwa kumkamata mmiliki wa silaha hiyo
ambaye ni Jumanne Abadlaha(25) maarufu kama babu G

Akiongea na vyombo vya habari mapema leo kamanda wa polisi mkoa wa
Arusha Liberatus Sabas alisema kuwa silaha hiyo pamoja na jambazi
huyo walifanikiwa kumkamata September 27 majira ya asubuhi.

Sabas alisema kuwa Polisi waliokuwa katika doria waliweza kumkamata
jambazi huyo na silaha yake  katika eneo la Ungalmtd ambapo ndipo
makazi ya jambazi huyo mara baada ya kupewa taarifa na raia wema kuwa
anamiliki silaha kinyume cha sheria lakini pia anatumia kwenye matukio
mbalimbali ya uhalifu.

Aidha alidai kuwa mara baada ya kumkamata jambazi huyo na silaha yake
waliweza kugundua kuwa silaha hiyo tayari ilikuwa imeshakatwa kitako
lakini ndani ilikuwa na risasi 13

Sabasi aliendelea kwa kusema kuwa mara baada ya kumkamata jambazi huyo
pamoja na silaha yake waliweza kumuhoji na alikiri kuwa amehusika na
matukio mbalimbaliya uhalifu kama vile unyanganyi wa kutumia nguvu na
silaha, lakini pia anamiliki silaha hiyo kiyume cha sheria.

Pia alidai kuwa mbali na kuweza kugundua kuwa anamiliki silaha hiyo
kinyume cha sheria lakini pia silaha hiyo imekuwa ikitumika kwenye
matukio mbalimbali  ya uhalifu ambayo yameweza kutokea katika mkoa wa
Arusha na nje ya mkoa wa Arusha.

Hataivyo kamanda huyo amedai kuwa upelelezi zaidi bado unaendelea na
mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani pindi upelelezi utakapokamilika.

Wakati huohuo kamanda huyo aliwataka wakazi wa mkoa wa Arusha
kuhakikisha kuwa wanatoa taarifa za siri hasa za wale wananchi wasio
waaminifu wanaojihusisha na matukio ya uhalifu kwani matukio hayo ya
ualifu yamechangia sana kushuka kwa amani ya nchi ya mkoa wa Arusha.
Mwisho.

SHULE ZA SEKONDARI AMBAZO ZINA MAABARA KUPEWA HUDUMA YA INTERNET BURE



Na Queen Lema, Arusha

KAMPUNI ya Smile ya mawasiliano ya Smile imeweka mikakati ya kusaidia
shule za Serikali ambazo zina maabara kwa kutoa huduma ya
mawasiliano(internet)bure itakayowawezesha wanafunzi waweze kusoma kwa
kupitia mitandao.

Hayo yameelezwa na Deo Ndejembe ambaye ni meneja kitengo cha mauzo
katika kampuni hiyo wakati akiongea kwenye uzinduzi wa mtandao wa
smile kwa mkoa wa Arusha mapema leo.

Deo alisema kuwampango huo unalenga kuimarisha huduma za maabara
katika shule za sekondari za serikali kwani wanafunzi wakiwa na huduma
hizo wataweza kusoma na kwenda pamoja na soko la dunia ambalo
linategemea zaidi huduma za mitandao.

Alidai kuwa mpango huo utaweza kuwanufaisha zaidi shule ambazo zina
maabara pamoja na kompyuta hivyo basi hata kwa shule ambazo hazina
maabara zinatakiwa kuweka mara moja ili ziweze kunufaika na mpango huo
ambao umeshaanza

“tunataka kuona kuwa lile lengo la serikali ambalo lililenga shule
ziwe na maabara linatimia lakini pia maabara ziwe za kisasa zaidi na
ziweze kupata teknolojia ya mawasiliano bure kwani itasaidia hata
ufaulu wa masomo kama sayansi kuweza kuongezeka’alisisitiza Deo

Wakati huo huo alidai kuwa mpango huo wa kutoa huduma za Tekonlojia
umeshaanza kwa shule 10 ndani ya Jiji la Dar es saalam lakini kwa mkoa
wa Arusha shule ya Arusha School tayari imeshanufaika na mpango huo
ambao ni bure

Naye Afisa mawasiliano wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania
(TCRA)Innocent Mongi alidai kuwa bado mkoa wa arusha unahitaji huduma
za mawasiliano zaidi kutokana na mwingiliano wa huduma kama vile
uchumi, na utalii

Mongi alidai kuwa uwepo wa mtandao huo wa Smile kwa mkoa wa arusha pia
utachangia wafanyabiashara  wakubwa na wadogo kuweza kufanya biashra
kutoka katika masoko mbalimbali duniani .

“napenda kuwasihi wakazi wa Arusha kuhakikisha kuwa wanatumia vema
mtandao huo ili kuraisisha shuguli mbalimbali za maendeleo kwa mkoa wa
arusha na kutokana na hili tunaamini kuwa Arusha itapata mabadiliko
makubwa”alisema Mongi

KANISA LATANGAZA NEEMA KWA WAHUDMU,WAHADIWA KUPEWA MASAMBA YA KILIMO KWA AJILI YA MSIMU MPYA WA KILIMO UJAO

NA BETY ALEX, ARUSHA


HUDUMA ya Maisha ya Yesu iliopo maeneo ya Kisongo jijini Arusha imesema kuwa kwa kutambua mchango wa wahudumu lakini pia wazee wa kanisa hilo wanatarajia kuwagawia mashamba ya kulima ili waweze kujiendeleza kwenye maisha yao ya kila siku na kuachana na tabia ya kuwa tegemezi

Aidha mpango huo unakuja mara baada ya kanisa hilo kuanza kutoa na kusisitiza masomo ya upendo ambayo yanalenga kumuinua zaidi Mungu kuliko mwanadamu

Akitangaza msimamo huo wa kuwasaidia wahudumu hao mchungaji kiongozi wa huduma hiyo Eliakimu molel”Channel”alisema kuwa mpango huo utasaidia sana kuongeza ufanisi wa kazi za kila siku lakini hata za kanisa

Alisema kuwa kwa kufanya hivyo wahudumu hao hasa wale ambao hawana kazi wataweza kuepukana na dhambi mbalimbali ambazo zinasababishwa na ukosefu wa kazi za kufanya

“ukiwa kama muhudumu hapa kanisani kwangu nilazima nihakikishe kuwa mnatoka siwezi kutoboa mimi mwenyewe halafu ninyi mkabaki mkiwa hamna lolote nasema nitagawa mashamba ya kulima na kila atakayweze akulima katika mashamba hayo ni lazima atoke”aliongeza Channel

Pia alisema kwa kanisa lolote lile ili liweze kusimama vema wahudumu lakini pia hatawazee wa kanisa wanapaswa kuwa makini kuanzia kiroho hadi kimwili hivyo ni wajibu wa viongozi wa makanisa kuhakikisha kuwa wanawaangalia makundi hayo

Alidai kuwa kama wakiwa dhaifu kwenye nyanja yoyote ile ni lazima kuwepo na kasoro kwenye huduma hiyo na badala yake badala ya kusonga mbele kwenye wokovu basi hata waumini watakuwa wanarudi nyuma kwenye wokovu

“wahudmu, wazee wa kansiani watu muhimu sana kwenye maendeleo ya kanisa la leo tusiwaache wakawa legelege bali tuwainue juu hata hali zao za maisha ziweze kubadilika ni faraja sana kama mhudumu wa kanisa akapanda daraja kwenye kiwango cha juu alafu pia akawa na imani basi hata mimi mchungaji nitafanya kazi yangu bila shaka ila kama akiwa legelege pepo likija linaanza nay eye kwanza”aliongeza Channel

Wakati huo huo alisema kuwa pia kanisa hilo limejiwekea hata utaratibu wa kuweza kuwasaidia wale wasiojweza kwa kuwa msaada wa vyakula ili wasiwe wakrisro wenye imani lakini pia wawe na uwezo kuamini kuwa hata kama hawana kitu bado mchungaji wao anawapenda na anaweza kufunga na kuomba juu yao ili hali za maisha ziweze kubadilika.

MWISHO